Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w13 1/5 uku. 15
  • Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Mungu Anapotusamehe, je, Anasahau?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Yehova Ni Mungu Mwenye Anasameheaka Sana
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2022
  • Musamaha wa Yehova Unakuletea Faida Gani
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
  • Wakati Yehova Anasamehe, Anasahau?
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2017
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
w13 1/5 uku. 15

Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa

Je, zambi zetu zinaweza kusamehewa?

[Picha katika ukurasa wa 15]

Kukubaliwa na Mungu si jambo ngumu sana

Kulingana na Biblia, wanadamu wote ni wenye zambi. Tuliriti muelekeo wa kufanya zambi kutoka kwa Adamu, mutu wa kwanza. Kwa hiyo, wakati fulani tunafanya mambo mabaya ambayo tunaweza kusikitikia baadaye. Yesu Kristo, Mwana wa Mungu, alitulipia deni la zambi kwa kufa kwa ajili yetu. Zabihu yake ya ukombozi iliwezesha tusamehewe zambi zetu. Ni zawadi kutoka kwa Mungu.​—Soma Waroma 3:23, 24.

Watu fulani wamefanya zambi nzito na wanajiuliza ikiwa Mungu anaweza kusamehe zambi zao. Jambo la kufurahisha ni kwamba Neno la Mungu linasema hivi: ‘Damu ya Yesu Mwana wake inatusafisha kutoka katika zambi yote.’ (1 Yohana 1:7) Yehova anasamehe bila kulazimishwa hata zambi nzito ikiwa tuna mutazamo unaofaa na ikiwa tunatubu.​—Soma Isaya 1:18.

Tunapaswa kufanya nini ili tusamehewe?

Ikiwa tunataka Yehova Mungu atusamehe, tunahitaji kujifunza juu yake, ni kusema, kuelewa njia zake, mashauri yake, na mambo ambayo anataka tufanye. (Yohana 17:3) Yehova anasamehe kabisa wale wanaotubu makosa yao na kujikaza kubadilika.​—Soma Matendo 3:19.

Kukubaliwa na Mungu si jambo ngumu sana kwetu. Yehova anaelewa uzaifu wetu. Yeye ni mwema na mwenye rehema. Fazili zake zenye upendo zinakuchochea utake kujifunza mengi juu ya namna unaweza kumupendeza, sivyo?​—Soma Zaburi 103:13, 14.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine