Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w13 1/6 uku. 16
  • Maulizo juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Maulizo juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Juu ya Nini Wanadamu Wanashindwa Kuleta Amani?​—Biblia Inasema Nini?
    Habari Zingine
  • Juu ya Nini Hakuna Amani mu Dunia?
    Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
  • Amani—Namna Gani Unaweza Kuipata?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2018
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
w13 1/6 uku. 16

MAULIZO JUU YA HABARI ZA BIBLIA YANAJIBIWA

Sababu gani amani imekosekana kabisa duniani?

[Picha katika ukurasa wa 16]

Ni serikali tu inayoweza kubadilisha mioyo ya watu ndiyo italeta amani duniani

Biblia inaonyesha sababu mbili. Sababu ya kwanza, hata ikiwa wanadamu wametimiza mambo ya ajabu, hawakuumbwa wakiwa na uwezo wa kuongoza hatua zao wenyewe. Sababu ya pili, mipango ya wanadamu imeshindwa kwa sababu ‘ulimwengu muzima unakaa katika nguvu za yule muovu,’ Shetani Ibilisi. Kwa hiyo, hata ikiwa wanadamu wamejikaza sana, hawajaweza kuleta amani duniani.​—Soma Yeremia 10:23; 1 Yohana 5:19.

Hali ya wanadamu ya kutafuta faida zao wenyewe na kutafuta mambo makubwa imefanya pia amani ikosekane kabisa duniani. Serikali moja tu ya duniani pote ambayo inaweza kufundisha watu kupenda mema na kuhangaikiana ndiyo italeta amani duniani.​—Soma Isaya 32:17; 48:18, 22.

Ni nani atakayeleta amani duniani?

Mungu Mweza-Yote ameahidi kuweka serikali moja tu duniani ili itawale wanadamu wote. Serikali hiyo itachukua nafasi ya serikali za wanadamu. (Danieli 2:44) Yesu, Mwana wa Mungu, atatawala akiwa Mukubwa wa Amani. Ataondoa mambo yote maovu duniani na atafundisha watu njia ya amani.​—Soma Isaya 9:6, 7; 11:4, 9.

Hata leo, chini ya uongozi wa Yesu, mamilioni ya watu duniani wanatumia Neno la Mungu, Biblia, ili kufundisha watu namna ya kuishi kwa amani pamoja na wengine. Hivi karibuni, amani itapatikana kabisa duniani.​—Soma Isaya 2:3, 4; 54:13.

Ili kupata habari zingine, soma sura ya 3 ya kitabu hiki: Biblia Inafundisha Kabisa Nini?, kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine