Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w13 1/11 uku. 16
  • Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Je, Wakristo Wote Waaminifu Wanaenda Mbinguni?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Ufalme wa Mungu Ni Nini?
    Biblia Inafundisha Kabisa Nini?
  • Ufalme wa Mungu Ni Nini?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
w13 1/11 uku. 16

MAULIZO JUU YA HABARI ZA BIBLIA YANAJIBIWA

Ni nani ambao wataenda mbinguni, na sababu gani?

Watu wengi wanatamani kuenda kuishi mbinguni. Yesu alisema kwamba mitume wake waaminifu wataishi huko. Mbele ya kufa, aliwaahidi kwamba atawatayarishia nafasi kwa Baba yake huko mbinguni.​—Soma Yohana 14:2.

Sababu gani watu watafufuliwa duniani ili kuenda kuishi mbinguni? Wataenda kufanya nini huko? Yesu aliwaambia mitume wake kwamba watakuwa wafalme na watatawala juu ya dunia.​—Soma Luka 22:28-30; Ufunuo 5:10.

Je, watu wote wazuri wanaenda mbinguni?

Katika inchi nyingi, ni watu wachache tu ndio watawala. Kwa kuwa Yesu anafufua watu kuenda kuishi mbinguni ili waweze kutawala juu ya dunia, tungetazamia wale wanaochaguliwa kuenda kutawala mbinguni wawe wachache. (Luka 12:32) Biblia inasema waziwazi hesabu ya watu ambao watatawala pamoja na Yesu.​—Soma Ufunuo 14:1.

Yesu amewatayarishia wafuasi wake fulani nafasi mbinguni. Je, unajua mambo ambayo watafanya huko?

Si wale wanaoenda mbinguni ndio tu ambao wanapokea zawadi. Raia waaminifu wa Ufalme wa Yesu watafurahia uzima usiokuwa na mwisho katika Paradiso ambayo itarudishwa duniani. (Yohana 3:16) Watu fulani wataingia katika Paradiso kwa kuokoka uharibifu wa dunia hii mbovu. Wengine wataingia katika Paradiso kupitia ufufuo.​—Soma Zaburi 37:29; Yohana 5:28, 29.

Ili kupata habari zingine, soma sura ya 8 ya kitabu hiki, kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova

Unaweza kuchukua kitabu hiki kwenye adresi yetu ya Internete www.jw.org

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine