Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w14 15/1 uku. 7-11
  • Tumuabudu Yehova, Mufalme wa Umilele

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Tumuabudu Yehova, Mufalme wa Umilele
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • MUFALME WA UMILELE ANATOKEZA FAMILIA MOJA YA ULIMWENGUNI POTE
  • WANA WA MUNGU WANAUKATAA UTAWALA WAKE
  • UTAWALA WA YEHOVA KISHA GARIKA
  • YEHOVA ANAKUWA MUFALME JUU YA ISRAELI
  • YEHOVA ANAWEKA MUFALME MUPYA
  • TUMUABUDU MUFALME WA UMILELE
  • Yehova Anafunua Kusudi Lake
    Ufalme wa Mungu Unatawala!
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
w14 15/1 uku. 7-11
Yehova Mungu anatawala akiwa kwenye kiti chake cha ufalme huko mbinguni

Tumuabudu Yehova, Mufalme wa Umilele

‘Kwa Mufalme wa umilele . . . kuwe na heshima na utukufu milele.’​—1 TIM. 1:17.

UNAWEZA KUJIBU NAMNA GANI?

  • Sababu gani namna ya Yehova ya kutawala inatufanya tumukaribie?

  • Namna gani Yehova ameendelea kuonyesha kwamba anahangaikia familia ya kibinadamu kwa upendo?

  • Ni nini inakuchochea umuabudu Mufalme wa umilele?

1, 2. (a) Ni nani aliye ‘Mufalme wa umilele,’ na sababu gani anastahili kuitwa hivyo? (Ona picha mwanzoni mwa habari hii.) (b) Kuhusiana na utawala wa Mungu, ni jambo gani linalotufanya tumukaribie?

MUFALME SOBHUZA WA 2 wa Swazilandi alitawala kwa miaka 61 hivi. Ni yeye aliyekuwa wa kwanza kutawala miaka mingi kuliko wafalme wote wa siku zetu. Hata ikiwa hilo ni jambo lenye kushangaza, kuna mufalme ambaye utawala wake hauna mwisho. Biblia inamuita ‘Mufalme wa umilele.’ (1 Tim. 1:17) Mutunga-zaburi anataja jina la Mufalme huyo anapotangaza hivi: ‘Yehova ni Mufalme mupaka wakati usio na kipimo, naam, milele.’​—Zab. 10:16.

2 Utawala wa Mungu hauna mwisho, hilo linaufanya uwe tofauti na utawala wowote wa wanadamu. Lakini, jambo linalotufanya tumukaribie Yehova ni namna yake ya kutawala. Mufalme mumoja aliyetawala Israeli kwa miaka 40 alimusifu Mungu kwa maneno yafuatayo: ‘Yehova ni mwenye rehema na mwenye neema, si mwepesi wa hasira na ni mwingi wa fazili zenye upendo. Yehova amekifanya imara kiti chake cha ufalme mbinguni; nao ufalme wake mwenyewe umetawala juu ya kila kitu.’ (Zab. 103:8, 19) Zaidi ya kuwa Mufalme wetu, Yehova ni Baba yetu wa mbinguni anayetupenda. Kujua jambo hilo kunatokeza maulizo mawili: Ni katika njia gani Yehova ametenda kama Baba yetu? Namna gani Yehova ametumia mamlaka yake tangu uasi katika Edeni? Majibu ya maulizo hayo yatatuchochea tumukaribie Yehova zaidi na kumuabudu kwa moyo wetu wote.

MUFALME WA UMILELE ANATOKEZA FAMILIA MOJA YA ULIMWENGUNI POTE

3. Ni nani aliyekuwa mushiriki wa kwanza wa familia ya Yehova ya ulimwenguni pote, na ni nani wengine walioumbwa na kuitwa “wana” wa Mungu?

3 Bila shaka Yehova alifurahi sana alipomuumba Mwana wake muzaliwa-pekee! Mungu hakumutendea muzaliwa wake wa kwanza kama mutu wa hali ya chini. Lakini, alimupenda na alimuomba ashiriki katika furaha ya kuumba viumbe wengine wakamilifu. (Kol. 1:15-17) Mamilioni ya malaika walikuwa kati ya viumbe hao. Malaika hao wanaitwa “wahudumu [wa Mungu] wanaofanya mapenzi yake.” Wanamutumikia Mungu kwa furaha, naye anawaheshimu kwa kuwaita “wana” wake na wako katika familia yake ya ulimwenguni pote.​—Zab. 103:20-22; Ayu. 38:7.

4. Namna gani wanadamu waliingia katika familia ya Mungu ya ulimwenguni pote?

4 Kisha kuumba mbingu na dunia, Yehova alipanua familia yake ya ulimwenguni pote. Kisha kutayarisha dunia kuwa makao mazuri na yaliyo na uwezo wa kuendelea kujitengeneza, Yehova alimalizia kazi zake za uumbaji kwa kumuumba mutu wa kwanza, Adamu, kwa mufano wake. (Mwa. 1:26-28) Kwa kuwa Yehova ndiye aliyemuumba, alikuwa na haki ya kutazamia kwamba Adamu atamutii. Kama Baba, Yehova alitoa maagizo yake yote kwa upendo na kwa upole. Maagizo hayo hayakumunyanganya Adamu uhuru hata kidogo.​—Soma Mwanzo 2:15-17.

5. Mungu alifanya nini ili dunia ijae wanadamu?

5 Tofauti na watawala wengi wa kibinadamu, Yehova anafurahi kutolea watu wake madaraka; anawatumainia washiriki wa familia yake ya ulimwenguni pote. Kwa mufano, alimutolea Adamu mamlaka juu ya kila kiumbe kinachoishi, na alimupatia hata kazi ambayo haikuwa rahisi lakini yenye kufurahisha ya kupatia wanyama majina. (Mwa. 1:26; 2:19, 20) Mungu hakuumba mara moja mamilioni ya watu wakamilifu ambao wangejaza dunia yote. Lakini, alimuumbia Adamu mwanamuke, Eva. (Mwa. 2:21, 22) Kisha, aliwatolea Adamu na Eva amri ya kuzaa na kujaza dunia. Wakiwa katika hali zenye ukamilifu, pole kwa pole wanadamu wangeifanya dunia yote iwe Paradiso. Wanadamu na malaika wangeendelea kwa umoja kumuabudu Yehova milele wakiwa familia yake ya ulimwenguni pote. Hilo lingekuwa jambo nzuri kabisa. Na lilionyesha kabisa kwamba Yehova ni Baba mwenye upendo.

WANA WA MUNGU WANAUKATAA UTAWALA WAKE

6. (a) Uasi ulianza namna gani katika familia ya Mungu? (b) Sababu gani uasi huo haukumaanisha kwamba Yehova alikuwa ameacha kuongoza mambo?

6 Jambo la kuhuzunisha ni kwamba Adamu na Eva hawakufurahia kuendelea kutawaliwa na Yehova. Lakini, walichagua kumusikiliza Shetani, aliyemuasi Mungu. (Mwa. 3:1-6) Kukataa utawala wa Mungu kuliwaletea wao na watoto wao uchungu, mateso, na kifo. (Mwa. 3:16-19; Rom. 5:12) Mungu hakuwa tena na watu watiifu duniani. Je, hilo linamaanisha kwamba alikuwa ameacha kuongoza mambo, ni kusema, hakuwa tena na mamlaka juu ya dunia na wanadamu? Bila shaka hapana! Aliendelea kutumia mamlaka yake kwa kuondoa Adamu na Eva katika bustani ya Edeni, na alichukua mipango ili wasirudi tena katika bustani hiyo kwa kutuma makerubi ili walinde mwingilio wa bustani hiyo. (Mwa. 3:23, 24) Wakati uleule, Mungu alionyesha kwamba yeye ni baba mwenye upendo kwa kuhakikisha kwamba kusudi lake la kuwa na familia moja ya ulimwenguni pote yenye kufanyizwa na viumbe wa kiroho na wanadamu litatimia. Aliahidi kwamba angetokeza “uzao” ambao ungemuharibu Shetani na kumaliza mambo yote mabaya yaliyoletwa na zambi ya Adamu.​—Soma Mwanzo 3:15.

7, 8. (a) Hali ilikuwa mbaya namna gani katika siku za Noa? (b) Yehova alifanya nini ili kusafisha dunia na kulinda familia ya wanadamu?

7 Katika miaka iliyofuata, watu fulani waliamua kuwa waaminifu kwa Yehova. Abeli na Enoka walikuwa kati ya watu hao. Lakini, watu wengi walimukataa Baba na Mufalme wao Yehova. Katika siku za Noa, dunia ‘ilijaa jeuri.’ (Mwa. 6:11) Je, hilo lilimaanisha kwamba Yehova hakuwa tena na mamlaka juu ya dunia? Historia inaonyesha nini?

8 Tuzungumuzie habari ya Noa. Yehova alimutolea maagizo kuhusu kujenga safina kubwa ambamo Noa na familia yake wangeokolewa. Mungu alionyesha pia upendo wake mukubwa kwa familia yote ya wanadamu alipomufanya Noa kuwa ‘muhubiri wa uadilifu.’ (2 Pet. 2:5) Noa aliwaomba watu watubu na aliwaonya kuhusu hukumu iliyokuwa karibu, lakini hawakumusikiliza. Kwa miaka mingi, Noa na familia yake waliishi kati ya watu wakali na wenye mwenendo muchafu sana. Yehova, Baba mwenye kuhangaikia wanadamu, alilinda na kubariki watu hao waaminifu wanane. Kwa kuleta Garika kubwa, Yehova alionyesha kwamba ana mamlaka juu ya wanadamu na malaika waasi. Bila shaka, Yehova alikuwa angali anaongoza mambo.​—Mwa. 7:17-24.

Matukio yanayoonyesha kwamba siku zote Yehova ameendelea kuongoza mambo

Siku zote Yehova ameendelea kuongoza mambo (Ona fungu la 6, 8, 10, 12, 17)

UTAWALA WA YEHOVA KISHA GARIKA

9. Ni nafasi gani ambayo Yehova alitolea wanadamu kisha Garika?

9 Noa na familia yake walipotoka katika safina na kutembea tena juu ya dunia iliyokuwa imesafishwa na walipovuta hewa safi, bila shaka mioyo yao ilijaa shukrani kwa Yehova kwa sababu aliwahangaikia na kuwalinda. Mara moja, Noa alijenga mazabahu na kutoa zabihu ili kumuabudu Yehova. Mungu alimubariki Noa na familia yake na kuwaagiza ‘wazae, wawe wengi, wajaze dunia.’ (Mwa. 8:20–9:1) Wanadamu walipata tena nafasi nyingine ya kumuabudu Yehova kwa umoja na kuijaza dunia.

10. (a) Kisha Garika, watu walimuasi tena Yehova namna gani na wapi? (b) Yehova alifanya nini ili kusudi lake litimie?

10 Lakini, Garika haikumaliza kutokamilika, na Shetani na malaika wake waliendelea kudanganya wanadamu. Kisha muda fulani, wanadamu walikataa tena utawala muzuri wa Yehova. Kwa mufano, Nimrodi, mujukuu wa Noa aliasi mamlaka ya Yehova kwa kiasi kikubwa. Nimrodi anaitwa ‘mwindaji mwenye nguvu kwa kumupinga Yehova.’ Alijenga miji mikubwa, kama vile Babeli, na alijifanya mufalme ‘katika inchi ya Shinari.’ (Mwa. 10:8-12) Mufalme wa umilele angemutendea namna gani muasi huyo aliyetaka kuvuruga kusudi la Mungu la ‘kujaza dunia’? Mungu alivuruga luga za watu na kuwatawanya “juu ya uso wote wa dunia” wale waliomuunga Nimrodi mukono. Walitawanyika na ibada yao ya uongo na ile roho ya kutawala wanadamu wenzao.​—Mwa. 11:1-9.

11. Namna gani Yehova alionyesha ushikamanifu wake kwa rafiki yake Abrahamu?

11 Hata ikiwa watu wengi waliabudu miungu ya uongo kisha Garika, watu fulani washikamanifu waliendelea kumuabudu Yehova. Mumoja wao alikuwa Abrahamu, ambaye kwa sababu ya kumutii Mungu, aliacha makao yake mazuri katika muji wa Uru na kwenda kuishi katika mahema kwa miaka mingi. (Mwa. 11:31; Ebr. 11:8, 9) Katika maisha yake ya kuhama​-hama, Abrahamu aliishi katika miji iliyotawaliwa na wafalme. Wengi kati ya wafalme hao waliishi katika miji yenye kuzungukwa na kuta. Lakini Yehova alilinda Abrahamu na familia yake. Kuhusiana na ulinzi ambao Baba yetu Yehova aliwatolea watu wake, mutunga-zaburi alisema hivi: ‘[Mungu] hakumuruhusu yeyote awaonee, bali aliwakaripia wafalme kwa sababu yao.’ (Zab. 105:13, 14) Ili kuonyesha ushikamanifu kwa rafiki yake Abrahamu, Yehova alimuahidi hivi: “Wafalme watatoka kwako.”​—Mwa. 17:6; Yak. 2:23.

12. Namna gani Yehova alimuonyesha Farao kwamba yeye ni Mutawala Mukubwa wa Ulimwengu Wote Muzima, na hilo lilikuwa na matokeo gani juu ya watu wake?

12 Mungu aliahidi pia Isaka mwana wa Abrahamu na mujukuu wake Yakobo kwamba atawabariki; baraka hiyo ilitia ndani kutokeza wafalme katika uzao wao. (Mwa. 26:3-5; 35:11) Lakini, mbele ya kutokeza wafalme hao, wazao wa Yakobo walikuwa watumwa huko Misri. Je, hilo lilimaanisha kwamba Yehova hangetimiza ahadi yake ao hakuwa tena na mamlaka juu ya dunia? Hapana kabisa! Kwa wakati wake, Yehova alionyesha uwezo wake na kumuonyesha Farao mwenye kiburi kwamba yeye ni Mutawala Mukubwa wa Ulimwengu Wote Muzima. Waisraeli waliokuwa watumwa walimutumainia Yehova, naye aliwakomboa kwa njia ya ajabu, kwa kuwavukisha Bahari Nyekundu. Ni wazi kwamba, Yehova alikuwa angali Mutawala Mukubwa wa Ulimwengu Wote Muzima, na akiwa Baba mwenye kujali, alitumia uwezo wake mukubwa ili kuwalinda watu wake.​—Soma Kutoka 14:13, 14.

YEHOVA ANAKUWA MUFALME JUU YA ISRAELI

13, 14. (a) Waisraeli walitangaza nini kuhusu utawala wa Yehova katika wimbo wao? (b) Ni ahadi gani kuhusu ufalme ambayo Mungu alimutolea Daudi?

13 Kisha tu kukombolewa kwa njia ya muujiza kutoka Misri, Waisraeli waliimba wimbo wa ushindi ili kumusifu Yehova. Wimbo huo ulioandikwa katika Kutoka sura ya 15, unatia ndani maneno haya katika mustari wa 18: ‘Yehova atatawala akiwa Mufalme mupaka wakati usio na kipimo, naam, milele.’ Bila shaka, Yehova alikuwa Mufalme wa taifa hilo jipya. (Kum. 33:5) Hata hivyo, watu hawakufurahia kutawaliwa na Yehova, Mutawala asiyeonekana. Karibu miaka 400 kisha kutoka Misri, Waisraeli walimuomba Mungu awapatie mufalme wa kibinadamu ili wafanane na mataifa jirani ambayo hayakuwa yanamuabudu Yehova. (1 Sam. 8:5) Ijapokuwa hivyo, Yehova alikuwa angali Mufalme, na alionyesha jambo hilo wakati wa utawala wa Daudi, mufalme wa pili wa kibinadamu aliyetawala Israeli.

14 Daudi alipeleka sanduku takatifu la agano huko Yerusalemu. Wakati wa kipindi hicho chenye shangwe, Walawi waliimba wimbo wa sifa uliokuwa na maneno haya ya maana sana yanayopatikana katika 1 Mambo ya Nyakati 16:31: “Sema kati ya mataifa: ‘Yehova amekuwa Mufalme!’” Mutu anaweza kujiuliza, ‘Kwa kuwa Yehova ni Mufalme wa umilele, namna gani alikuwa Mufalme wakati huo?’ Yehova anakuwa Mufalme anapotumia mamlaka yake ao anapomuchagua mutu fulani ili amuwakilishe ao ashugulikie hali fulani ya pekee. Ni jambo la maana sana kujua hilo. Mbele Daudi akufe, Yehova alimuahidi kwamba utawala wake ungeendelea milele, alimuambia hivi: ‘Nitainua uzao wako baada yako, mwana wako; na kwa kweli nitaufanya imara ufalme wake.’ (2 Sam. 7:12, 13) Mwishowe, “uzao” huo wa Daudi ulitokea miaka zaidi 1 000 baadaye. Uzao huo ulikuwa nani, na ungeanza kutawala wakati gani?

YEHOVA ANAWEKA MUFALME MUPYA

15, 16. Ni wakati gani Yesu alitiwa mafuta akiwa Mufalme wa wakati ujao, na alifanya nini kuhusiana na utawala wake alipokuwa duniani?

15 Katika mwaka wa 29, Yohana Mubatizaji alianza kuhubiri kwamba “Ufalme wa mbinguni [ulikuwa] umekaribia.” (Mt. 3:2) Yohana alipomubatiza Yesu, Yehova alimutia mafuta ili awe Masiya aliyeahidiwa na Mufalme wa wakati ujao wa Ufalme wa Mungu. Yehova alimuonyesha mwana wake upendo aliposema hivi: ‘Huyu ni Mwanangu, mupendwa, ambaye nimemukubali.’​—Mt. 3:17.

16 Katika huduma yake yote hapa duniani, Yesu alimutukuza Baba yake. (Yoh. 17:4) Alifanya hivyo kwa kuhubiri Ufalme wa Mungu. (Lu. 4:43) Hata aliwafundisha wafuasi wake wasali Ufalme huo uje. (Mt. 6:10) Akiwa Mufalme Aliyechaguliwa, Yesu aliwaambia hivi maadui wake: ‘Ufalme wa Mungu uko katikati yenu.’ (Lu. 17:21) Baadaye, mangaribi moja mbele auawe, Yesu alifanya ‘agano kwa ajili ya ufalme’ pamoja na wafuasi wake. Hilo lilitolea wanafunzi fulani wa Yesu tumaini la kutawala pamoja naye mbinguni katika Ufalme wa Mungu.​—Soma Luka 22:28-30.

17. Yesu alianza kutawala nani wakati wa mitume, lakini alipaswa kungojea nini?

17 Yesu angeanza kutawala wakati gani? Hangeanza kutawala mara moja. Katika kipindi cha muchana cha siku iliyofuata, Yesu aliuawa na wanafunzi wake walitawanyika. (Yoh. 16:32) Lakini kama vile zamani, Yehova aliendelea kuongoza mambo. Kisha siku tatu, alimufufua Mwana wake, na kwenye Pentekoste ya mwaka wa 33, Yesu alianza kutawala kutaniko la Kikristo la ndugu zake watiwa-mafuta. (Kol. 1:13) Lakini, Yesu, “uzao” ulioahidiwa, alipaswa kungojea wakati ambapo angepewa mamlaka juu ya dunia yote. Yehova alimuambia Mwana wake hivi: ‘Keti kwenye mukono wangu wa kuume mupaka niwaweke adui zako kuwa kiti cha miguu yako.’​—Zab. 110:1.

TUMUABUDU MUFALME WA UMILELE

18, 19. Tunachochewa kufanya nini, na ni maulizo gani yatakayojibiwa katika habari inayofuata?

18 Utawala wa Yehova ulipingwa kwa miaka mingi mbinguni na duniani. Lakini, siku zote Yehova ni Mutawala Mukubwa wa Ulimwengu Wote Muzima, na ameendelea kuongoza mambo. Akiwa Baba mwenye upendo, alilinda na kuhangaikia watumishi wake waaminifu kama vile Noa, Abrahamu, na Daudi. Je, hilo halituchochee tujitiishe kwa Mufalme wetu na kumukaribia zaidi?

19 Lakini tunaweza kujiuliza hivi: Namna gani Yehova amekuwa Mufalme katika siku zetu? Namna gani tunaweza kuonyesha kwamba sisi ni raia waaminifu wa Ufalme wa Yehova na kufikia ukamilifu katika familia ya Mungu ya ulimwenguni pote? Tunapoomba Ufalme wa Mungu uje, tunamaanisha nini? Maulizo hayo yatajibiwa katika habari inayofuata.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine