Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w14 1/8 uku. 16
  • Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Namna Gani Unaweza Kujua Dini ya Kweli?
    Habari Njema Yenye Inatoka kwa Mungu!
  • Kuko Habari Gani Njema Juu ya Dini?
    Habari Njema Yenye Inatoka kwa Mungu!
  • Unaweza Kuitambua Ibada ya Kweli Jinsi Gani?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Dini Inayokubaliwa na Mungu
    Biblia Inafundisha Kabisa Nini?
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
w14 1/8 uku. 16
Mashahidi wa Yehova wa mataifa mbalimbali wanakusanyika pamoja kwenye Jumba la Ufalme

Maulizo Juu Ya Habari Za Biblia Yanajibiwa

Dini zote zinamuheshimu Mungu?

Unaposikiliza habari za ulimwengu, labda umetambua kwamba wakati fulani watu wamefanya mabaya katika jina la dini. Dini zote hazitokane na Mungu wa kweli. (Mathayo 7:15) Kwa kweli, hilo linafanya wanadamu wengi wadanganywe.—Soma 1 Yohana 5:19.

Hata hivyo, Mungu anatambua watu wenye mioyo mizuri wanaopenda mambo mazuri na ya kweli. (Yohana 4:23) Mungu anaalika watu kama hao wajifunze kweli kutoka katika Neno lake, Biblia.—Soma 1 Timotheo 2:3-5.

Namna gani unaweza kuitambua dini ya kweli?

Yehova Mungu anaunganisha watu kutoka katika dini nyingi kwa kuwafundisha kweli na kuwafundisha kupendana. (Mika 4:2, 3) Kwa hiyo, unaweza kutambua waabudu wa dini ya kweli kupitia namna wanatendeana kati yao.—Soma Yohana 13:35.

Yehova Mungu anaunganisha watu wa namna zote kupitia ibada ya kweli.—Zaburi 133:1

Imani ya waabudu wa kweli na namna yao ya kuishi inategemea Biblia. (2 Timotheo 3:16) Wanaheshimu pia jina la Mungu. (Zaburi 83:18) Na wanatetea Ufalme wa Mungu kuwa tumaini pekee la wanadamu. (Danieli 2:44) Wanamuiga Yesu kwa kuacha ‘nuru yao iangaze,’ kwa kuwatendea majirani wao mema. (Mathayo 5:16) Wakristo wa kweli wanatembelea watu nyumbani kwao wakiwa na kusudi la kuwatangazia habari njema ya Ufalme wa Mungu na hilo linasaidia watu wawatambue.—Soma Mathayo 24:14; Matendo 5:42; 20:20.

Ili kupata habari zingine, soma sura ya 15 ya kitabu hiki, kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova

Unaweza kupata kitabu hiki kwenye adresi yetu ya Internete www.jw.org

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine