Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w14 1/12 uku. 16
  • Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Tunaweza Kupata Wapi Majibu ya Maulizo ya Maana Sana Juu ya Maisha?
    Tunaweza Kupata Wapi Majibu ya Maulizo ya Maana Sana Juu ya Maisha?
  • Musaada Zaidi Kwa Ajili Ya Familia
    Amuka!—2018
  • Kuko Siku Mateso Itaisha?
    Kuko Siku Mateso Itaisha?
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
w14 1/12 uku. 16

MAULIZO JUU YA HABARI ZA BIBLIA YANAJIBIWA

Namna gani watoto wanaweza kujifunza kumupenda Mungu?

Muzazi anayemufundisha mutoto wake kwa kutumia habari za uumbaji

Tumikisha habari za uumbaji ili kusaidia watoto wako wamujue Mungu na kumupenda

Watoto wako wanaweza kujifunza kumupenda Mungu ikiwa tu wako hakika kuwa Mungu iko na kuwa anawapenda. Ili kumupenda Mungu, wana lazima ya kumujua. (1 Yohana 4:8) Kwa mufano, wana lazima ya kujua: Mungu alikuwa na kusudi gani alipoumba mutu? Sababu gani Mungu anaacha watu wateseke? Mungu atafanyia watu nini wakati unaokuja?—Soma Wafilipi 1:9.

Ili kusaidia watoto wako wamupende Mungu, unapaswa kuwaonyesha kuwa wewe mwenyewe unamupenda. Wakati wanaona hivyo, labda watafuata mufano wako.—Soma Kumbukumbu la Torati 6:5-7; Methali 22:6.

Namna gani unaweza kugusa mioyo ya watoto wako?

Neno la Mungu liko na nguvu. (Waebrania 4:12) Kwa hiyo, saidia watoto wako wajue mafundisho ya musingi ya Neno la Mungu. Ili kugusa mioyo ya watu, Yesu aliuliza maulizo, alisikiliza, na kufasiria Maandiko. Ili kugusa mioyo ya watoto wako, unaweza kuiga njia ya Yesu ya kufundisha.—Soma Luka 24:15-19, 27, 32.

Tena, habari za Biblia juu ya namna Mungu alitendea watu zinaweza kusaidia watoto wamujue Mungu na kumupenda. Vitabu vinavyoweza kusaidia kufanya hivyo vinapatikana kwenye adresi yetu ya Internete www.jw.org.—Soma 2 Timotheo 3:16.

Ili kupata habari zingine, soma sura ya 14 ya kitabu hiki, kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova

Unaweza kupata kitabu hiki kwenye adresi yetu ya Internete www.jw.org, ao tuma ombi lako kwenye adresi iliyo kwenye ukurasa wa 2

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine