Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • wp16 na. 1 uku. 4-5
  • Kukosa Uaminifu Kunakuletea Matokeo Gani?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Kukosa Uaminifu Kunakuletea Matokeo Gani?
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2016
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • KUKOSA UAMINIFU KUNAVUNJA KUTUMAINIANA
  • KUKOSA UAMINIFU KUNAAMBUKIZA
  • Kuwa Muaminifu Kuko na Faida?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2016
  • Njia Mbalimbali za Kuanzisha Mazungumuzo
    Huduma Yetu ya Ufalme—2011
  • Ukuwe Munyoofu Katika Mambo Yote
    Namna ya Kubakia Katika Upendo wa Mungu
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2016
wp16 na. 1 uku. 4-5

HABARI KUBWA | SABABU GANI NI MUZURI KUWA MUAMINIFU?

Kukosa Uaminifu Kunakuletea Matokeo Gani?

“Sikuzote, kuko hali ngumu zenye zinaomba kukosa uaminifu kidogo ili kuzimaliza.”—Samantha, inchi ya Afrika Kusini.

Unaitika maneno hayo? Kama Samantha, sisi wote tumekwisha kupambana na hali ngumu wakati fulani. Namna tunatenda katika hali hizo zenye kutuchochea kukosa uaminifu inaweza kufunua ni kanuni gani tunaona kuwa za maana. Kwa mufano, ikiwa tunaona kulinda heshima yetu ili tusipate haya kuwa jambo la lazima, tutaona kukosa uaminifu kuwa jambo la lazima pia. Lakini, mara nyingi wakati watu wengine wanavumbua kweli, kukosa uaminifu kunaleta matokeo ya mubaya. Ona matokeo yenye kufuata.

KUKOSA UAMINIFU KUNAVUNJA KUTUMAINIANA

Musingi wa urafiki wa kweli ni kutumainiana. Wakati watu wawili wanatumainiana, wanajisikia salama kabisa. Lakini kutumainiana hakujilete kwa muujiza. Watu wanaanza kutumainiana kwa kupitisha wakati pamoja, kuzungumuza waziwazi na kutendeana bila uchoyo. Hata hivyo, tendo moja tu la kukosa uaminifu linaweza kuvunja kutumainiana. Na wakati kutumainiana kunavunjika, inaweza kuwa nguvu sana kutumainiana tena.

Umekwisha kudanganywa na mutu fulani mwenye uliwazia kuwa rafiki wa muzuri? Kama ni vile, ulijisikia namna gani? Pengine ulijisikia kuwa mwenye kuumizwa, ao hata kusalitiwa. Jambo hilo linaeleweka kabisa. Kwa kweli, kukosa uaminifu kunaweza kuvunja musingi wa urafiki wa kweli.

KUKOSA UAMINIFU KUNAAMBUKIZA

Katika uchunguzi moja, Robert Innes, profesa wa mambo ya feza kwenye Masomo ya Juu ya Kalifornia, alivumbua kama, “kwa kweli, kukosa uaminifu kunaambukiza.” Kwa hiyo, kukosa uaminifu kunaweza kufananishwa na ugonjwa wenye kuambukiza. Ikiwa unazoea kujiunga na mutu mwenye tabia ya kudanganya, uko katika hatari kubwa ya “kuambukizwa” na tabia hiyo.

Namna gani unaweza kuepuka kuangukia katika mutego wa kukosa uaminifu? Biblia inaweza kukusaidia. Tafazali, chunguza kanuni fulani za Biblia..

Namna Mbalimbali za Kukosa Uaminifu

Kusema uongo

KUSEMA UONGO KUNAMAANISHA NINI? Kudanganya mutu mwenye kuwa na haki ya kujua kweli. Kunaweza pia kumaanisha kubadilisha habari ili kuongoza mutu mubaya, kuepuka kueleza habari ya lazima ili kudanganya mutu, na kutilia chumvi mambo ya kweli ili mutu aone mambo namna hayako.

MAMBO BIBLIA INASEMA: ‘Mutu mwenye hila [ujanja] ni chukizo kwa Yehova, lakini urafiki Wake uko pamoja na watu wanyoofu [waaminifu].’ (Methali 3:32) ‘Sasa kwa kuwa mumeuondolea mbali uongo, museme kweli kila mumoja wenu na jirani yake.’—Waefeso 4:25.

Kuchongea

KUCHONGEA KUNAMAANISHA NINI? Kusema habari za uongo na za ujanja ili kuharibisha sifa ya mutu mwengine.

MAMBO BIBLIA INASEMA: ‘Mutu mwenye hila anaendelea kutokeza ugomvi nyakati zote, na muchongezi anawatenganisha wale wanaofahamiana.’ (Methali 16:28) ‘Pasipo na kuni moto unazimika, na pasipo na muchongezi ugomvi unatulia.’—Methali 26:20.

Ulagai

ULAGAI UNAMAANISHA NINI? Kutumia maneno ya uongo ili kumushawishi mutu atoe feza ao kitu chake.

MAMBO BIBLIA INASEMA: ‘Haupaswe kumupunja mufanyakazi wa kukodiwa aliye katika taabu na aliye masikini.’ (Kumbukumbu la Torati 24:14, 15) ‘Yeye anayemupunja mutu wa hali ya chini amemuletea shutuma Mutengenezaji wake, lakini anayemuonyesha masikini kibali anamutukuza Yeye.’—Methali 14:31.

Kuiba

KUIBA KUNAMAANISHA NINI? Kukamata kitu cha mutu fulani bila ruhusa.

MAMBO BIBLIA INASEMA: ‘Mwizi asiibe tena, bali afanye kazi ya bidii, akifanya kwa mikono yake kazi iliyo njema, ili akuwe na kitu cha kumugawia mutu aliye na uhitaji [lazima].’ (Waefeso 4:28) ‘Musipotoshwe [musidanganywe]. . . . Wala wezi, wala watu wenye pupa [tamaa ya mubaya], wala walevi, wala watukanaji, wala wanyanganyi hawatauriti ufalme wa Mungu.’—1 Wakorintho 6:9, 10.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine