Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • wp16 na. 2 uku. 3-4
  • Mambo Hayo Yalitokea Kabisa?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Mambo Hayo Yalitokea Kabisa?
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2016
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • MAMBO YA HAKIKA YANAONYESHA NINI?
  • TUSEME NINI JUU YA UFUFUO WA YESU?
  • Ufufuo wa Yesu Una Maana Gani Kwetu?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Je, Kweli Yesu Alifufuliwa?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Ufufuo Ni Tumaini la Kweli!
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2020
  • Yesu Kristo—Maswali Yetu Yajibiwa
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2016
wp16 na. 2 uku. 3-4

HABARI KUBWA | SABABU GANI YESU ALITESEKA NA KUFA?

Mambo Hayo Yalitokea Kabisa?

Katika mwaka wa 33, Yesu wa Nazarethi aliuawa. Alishitakiwa kwa uongo kama anachochea watu kupinga serikali, alipigwa kama nyama, na kutundikwa kwenye muti. Alikufa katika maumivu makali sana. Lakini Mungu alimufufua, na kisha siku 40, alipanda mbinguni.

Habari hiyo ya pekee inazungumuziwa katika vitabu ine vya Injili vya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo, yenye watu wengi wanaita Agano Jipya. Mambo hayo yalitokea kabisa? Hilo ni ulizo nzito, pia lenye kufaa. Kama mambo hayo hayakutokea, imani ya Wakristo haina faida na tumaini la uzima wa milele katika Paradiso ni ndoto tu. (1 Wakorintho 15:14) Lakini kama mambo hayo yalitokea kabisa, wanadamu wako na tumaini la muzuri juu ya wakati unaokuja; wewe pia unaweza kuishi wakati huo. Kwa hiyo, habari za vitabu vya Injili ni za kweli ao ni za kuwazia tu?

MAMBO YA HAKIKA YANAONYESHA NINI?

Tofauti na habari za kuwazia, maandishi ya vitabu vya Injili yanaeleza habari za kweli kabisa na hata mambo madogo-madogo. Kwa mufano, maandishi hayo ya Injili yanajaa majina ya nafasi za kweli, na nafasi nyingi kati ya hizo zinaweza kutembelewa leo. Yanazungumuzia watu wa kweli, na wanahistoria wa ulimwengu wanahakikisha kama watu hao waliishi.—Luka 3:1, 2, 23.

Yesu mwenyewe anazungumuziwa na waandikaji wa ulimwengu wa mwaka kati ya 1 na 200.a Namna Yesu aliuawa, kama vile inaonyeshwa katika vitabu vya Injili, inapatana na namna Waroma walikuwa wanaua watu wakati huo. Tena, mambo yenye yalitokea yanaelezwa kwa uaminifu na kwa ukweli; hata makosa ya wanafunzi fulani wa Yesu yanaonyeshwa. (Mathayo 26:56; Luka 22:24-26; Yohana 18:10, 11) Mambo hayo yote yanaonyesha kabisa kama waandikaji wa vitabu vya Injili walikuwa waaminifu na hawakukosea kuhusu mambo waliandika juu ya Yesu.

TUSEME NINI JUU YA UFUFUO WA YESU?

Hata kama watu wengi wanaitika kuwa Yesu aliishi na alikufa, wengine wanaweza kuwa na mashaka juu ya ufufuo wake. Hata mitume wake hawakuamini wakati waliambiwa kwa mara ya kwanza kama Yesu alifufuka. (Luka 24:11) Lakini, mashaka yote yaliisha wakati watu fulani na wanafunzi wengine walimuona kwa wakati mbalimbali Yesu mwenye alikuwa amefufuliwa. Kwa kweli, wakati fulani kulikuwa watu zaidi ya 500 wenye walimuona.—1 Wakorintho 15:6.

Hata kama wanafunzi wa Yesu walikuwa katika hatari ya kufungwa na kuuawa, walitangaza kwa ujasiri ufufuo wa Yesu kwa watu wote, na kwa wenye walimuua. (Matendo 4:1-3, 10, 19, 20; 5:27-32) Wanafunzi hao wengi wangekuwa na ujasiri ikiwa hawakukuwa hakika kama Yesu alifufuliwa kabisa? Kusema kweli, ufufuo wa Yesu ulitokea kabisa, hilo ndilo jambo lenye lilifanya Ukristo ukuwe na matokeo makubwa wakati huo na hata leo.

Habari za vitabu vya Injili kuhusu kifo cha Yesu na ufufuo wake ziko na ushuhuda wote wenye kuonyesha kama ni habari za kihistoria za kweli kabisa. Kusoma kwa uangalifu habari hizo, kutakuhakikishia kama mambo hayo yalitokea kabisa. Tena, utakuwa hakika zaidi wakati unaelewa sababu gani mambo hayo yalitokea. Habari yenye kufuata itazungumuzia jambo hilo.

a Tasito, mwenye alizaliwa mwaka wa 55 hivi kisha kuzaliwa kwa Yesu, aliandika kama “Kristo, mwenye jina [Wakristo] lilitokana na jina lake, aliuawa katika mikono ya Pontio Pilato, mumoja kati ya magavana wetu, wakati wa utawala wa Tiberio.” Yesu anatajwa tena na mwanahistoria Suetonius (mwenye alizaliwa katika mwaka wa 69); mwanahistoria Muyahudi Joseph (mwenye alizaliwa katika mwaka wa 37 ao 38); na Plini Mudogo, gavana wa Bithinia (mwenye alizaliwa katika mwaka wa 61 ao 62).

Sababu Gani Hakuna Maandishi Mengi ya Ulimwengu Yenye Kushuhudia Juu Yake?

Kwa sababu Yesu anajulikana sana katika ulimwengu, ni lazima tutazamie maandishi mengi ya kati ya mwaka wa 1 na 100, zaidi ya Biblia, yashuhudie kama Yesu alikuwa mutu wa kweli na kama alifufuliwa? Haiko lazima. Kwanza, vitabu hivyo vya Injili viliandikwa kumepita miaka zaidi ya 2 000. Ni maandishi kidogo tu ya wakati huo ndio yangali mupaka leo. (1 Petro 1:24, 25) Tena, inawezekana maadui wa Yesu hawangeandika jambo lolote lenye lingesaidia watu kumuamini.

Juu ya ufufuo wa Yesu, Petro, mumoja kati ya mitume wake, alisema hivi: ‘Mungu alimufufua huyu katika siku ya tatu na kumufunua, si kwa watu wote, bali [lakini] kwa mashahidi waliowekwa kimbele na Mungu, kwetu sisi, tuliokula na kunywa pamoja naye baada ya kufufuliwa kwake kutoka kwa wafu.’ (Matendo 10:40, 41) Sababu gani Mungu hakumufunua Yesu kwa watu wote? Injili ya Mathayo inatuambia kama wakati maadui wa Yesu walisikia habari ya ufufuo wake, walijaribu kuzuia habari hiyo isienee.—Mathayo 28:11-15.

Hilo linamaanisha kama Yesu alipenda habari juu ya ufufuo wake ibakie siri? Hapana, kwa sababu Petro aliendelea kusema hivi: ‘Alituagiza sisi tuwahubirie watu na kutoa ushahidi kamili kwamba huyu ndiye aliyeagizwa na Mungu kuwa muamuzi wa walio hai [wazima] na wafu.’ Wakristo wa kweli walifanya vile na wanaendelea kufanya vile kabisa.—Matendo 10:42.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine