Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • wp17 na. 5 uku. 7-8
  • Namna Gani Malaika Wanaweza Kukusaidia?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Namna Gani Malaika Wanaweza Kukusaidia?
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2017
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • MALAIKA WALITEGEMEZA KUTANIKO LA KWANZA LA KIKRISTO
  • NAMNA GANI MALAIKA WANAWEZA KUKUSAIDIA?
  • Iga Mufano wa Malaika Waaminifu
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
  • Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Malaika
    Amuka!—2017
  • Ukweli Kuhusu Malaika
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2017
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2017
wp17 na. 5 uku. 7-8

HABARI KUBWA | MALAIKA​—WAKO KABISA? SABABU GANI TUFIKIRIE JAMBO HILO?

Namna Gani Malaika Wanaweza Kukusaidia?

Malaika waaminifu wanapendezwa sana na mambo ya wanadamu na wanashiriki kwa bidii katika kutimiza mapenzi ya Yehova. Wakati Mungu aliumba dunia, malaika ‘walipiga vigelegele pamoja kwa shangwe, na wana wote wa Mungu wakaanza kupaaza sauti kwa kushangilia.’ (Ayubu 38:4, 7) Katika historia, malaika wametamani “kuchungulia” katika maneno ya kiunabii kuhusu mambo yenye yatatokea wakati wenye kuja katika dunia.​—1 Petro 1:11, 12.

Biblia inaonyesha kwamba katika kutimiza mapenzi ya Mungu, wakati fulani malaika wamelinda kwa kadiri fulani waabudu wa kweli. (Zaburi 34:7) Kwa mufano:

  • Wakati Yehova alileta uharibifu juu ya miji yenye kujaa uovu ya Sodoma na Gomora, malaika walimusaidia Loti mwadilifu na familia yake kuponyoka.​—Mwanzo 19:1, 15-26.

  • Wakati vijana watatu Waebrania wenye walikuwa katika Babiloni ya zamani walihukumiwa kifo katika tanuru yenye kuwaka moto, Mungu ‘alimutuma malaika wake na kuwaokoa watumishi wake.’​—Danieli 3:19-28.

  • Kisha kupitisha usiku muzima katika shimo la simba wenye njaa kali, Danieli alionyesha kwamba aliokoka kwa sababu ‘Mungu [wake] mwenyewe alimutuma malaika wake na kufunga vinywa vya simba.’​—Danieli 6:16, 22.

Malaika mumoja analinda Danieli asikuliwe na simba

Malaika wamesaidia watu waaminifu tangu zamani sana

MALAIKA WALITEGEMEZA KUTANIKO LA KWANZA LA KIKRISTO

Wakati fulani, malaika wa Mungu walitenda katika kutaniko la kwanza la Kikristo wakati ilikuwa lazima kufanya hivyo ili kutimiza mapenzi ya Yehova. Kwa mufano:

  • Malaika mumoja alifungua milango ya gereza na kuongoza mitume wenye walifungwa humo ili waendelee kuhubiri katika hekalu.​—Matendo 5:17-21.

  • Malaika mumoja alimuagiza Filipo mweneza-injili aende kwenye barabara ya jangwani yenye kushuka kutoka Yerusalemu mupaka Gaza ili ahubirie Mwethiopia mwenye alikuwa ameenda Yerusalemu ili kuabudu.​—Matendo 8:26-33.

  • Ulipofika wakati wa Mungu ili watu wa mataifa wakuwe Wakristo, katika maono, malaika mumoja alimutokelea Kornelio, ofisa Muroma, na kumuagiza aite mutume Petro katika nyumba yake.​—Matendo 10:3-5.

  • Wakati mutume Petro alifungwa, malaika mumoja alimutokelea na kumuongoza inje ya gereza.​—Matendo 12:1-11.

NAMNA GANI MALAIKA WANAWEZA KUKUSAIDIA?

Hakuna ushuhuda wenye kuonyesha kama Mungu anatumia malaika leo ili kusaidia watu kimuujiza kama vile inazungumuziwa katika Biblia. Hata hivyo, kuhusu wakati wetu, Yesu alisema hivi: “Na hii habari njema ya ufalme itahubiriwa katika dunia yote inayokaliwa ili kuwa ushahidi kwa mataifa yote; na ndipo ule mwisho utakapokuja.” (Mathayo 24:14) Ulijua kwamba wanafunzi wa Kristo wanafanya kazi hiyo chini ya uongozi wa malaika?

Watu wanatembea karibu na chombo cha kuonyesha vichapo

Malaika wanasaidia kutangaza habari njema katika dunia yote

Kitabu cha Ufunuo kinaonyesha kwamba malaika wangesaidia kwa bidii watu katika dunia yote ili wajifunze kuhusu Yehova Mungu na mapenzi yake kwa ajili ya wanadamu. Mutume Yohana aliandika hivi: ‘Nami nikamuona malaika mwingine akiruka katikati ya mbingu, naye alikuwa na habari njema ya milele ili aitangaze kuwa habari za furaha kwa wale wanaokaa duniani, na kwa kila taifa na kabila na luga na watu, akisema kwa sauti kubwa: Muogopeni Mungu na kumupa utukufu, kwa sababu saa ya hukumu yake imefika, na kwa hiyo muabuduni Yeye aliyezifanya mbingu na dunia na bahari na chemchemi za maji.’ (Ufunuo 14:6, 7) Ushuhuda mwingi wa siku zetu unaonyesha kwamba malaika wanategemeza kazi ya kuhubiri Ufalme katika dunia yote. Kwa kweli, wakati mutenda-zambi hata mumoja anatubu na kumurudilia Yehova, “shangwe hutokea kati ya malaika za Mungu.”​—Luka 15:10.

Ni nini itatokea wakati kazi ya kuhubiri itamalizika? “Majeshi [ya malaika] mbinguni” yatamuunga Yesu Kristo mukono, Mufalme wa wafalme, ili kupigana “vita vya ile siku kuu ya Mungu Mweza-Yote” kwenye Har-Magedoni. (Ufunuo 16:14-16; 19:14-16) Malaika wenye nguvu watakamilisha hukumu ya Mungu wakati Bwana Yesu “anapoleta kisasi juu ya wale . . . wasiotii habari njema juu ya Bwana wetu Yesu.”​—2 Wathesalonike 1:7, 8.

Kwa hiyo, ukuwe hakika kwamba malaika wanapendezwa na wewe kipekee. Wanahangaikia kabisa hali nzuri ya wale wote wenye kutamani kumutumikia Mungu, na mara nyingi, Yehova amewatumia ili kuwatia nguvu na kuwalinda watumishi wake waaminifu duniani.​—Waebrania 1:14.

Kila moja kati yetu iko na uamuzi mukubwa wa kukamata. Tutasikiliza na kutii habari njema yenye kutangazwa katika dunia yote? Mashahidi wa Yehova wa eneo lenu watafurahi kukusaidia ufaidike na musaada wenye upendo wa malaika wa Mungu wenye nguvu.

Ili kupata habari zaidi kuhusu mambo yenye Biblia inasema kuhusu malaika waaminifu na wenye hawako waaminifu, ona sura ya 10 ya kitabu Biblia Inafundisha Kabisa Nini? chenye kuchapishwa na Mashahidi wa Yehova. Kinapatikana pia kwenye jw.org ao tumia chombo cha kusoma alama hii.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine