Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • wp17 na. 6 uku. 12-14
  • Biblia—Sababu Gani Ni Nyingi?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Biblia—Sababu Gani Ni Nyingi?
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2017
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • BIBLIA YA KWANZA
  • SEPTANTE YA KIGIRIKI
  • VULGATE YA KILATINI
  • KUONGEZEKA KWA TAFSIRI ZA MUPYA
  • Yehova Mungu, Anazungumuza na Watu Wake
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • “Neno la Mungu Wetu Litadumu” Milele
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2017
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2017
wp17 na. 6 uku. 12-14
Biblia mbalimbali: yenye kuandikwa, zenye kuchapishwa, na za kielektroniki

Biblia​—Sababu Gani Ni Nyingi?

Sababu gani leo kuko tafsiri nyingi za Biblia? Unaona tafsiri za mupya kuwa musaada ao kizuizi cha kuelewa Biblia? Kujifunza kuhusu chanzo cha tafsiri hizo kunaweza kukusaidia kuzitumia kwa njia ya hekima

Hata hivyo, ni nani waliandika Biblia kwa mara ya kwanza, na walifanya hivyo wakati gani?

BIBLIA YA KWANZA

Kwa kawaida, Biblia inagawanywa katika sehemu mbili. Sehemu ya kwanza iko na vitabu 39 vyenye kuwa na “maneno matakatifu ya Mungu.” (Waroma 3:2) Kupitia roho yake, Mungu aliongoza wanaume waaminifu ili kuandika vitabu hivyo katika kipindi kirefu cha wakati, karibu miaka 1100, kuanzia 1513 mbele ya kuzaliwa kwa Yesu mupaka kisha mwaka 443 hivi mbele ya kuzaliwa kwa Yesu. Waliandika zaidi sana katika Kiebrania, ndiyo sababu tunaita sehemu hiyo Maandiko ya Kiebrania, inajulikana pia kuwa Agano la Kale.

Sehemu ya pili iko na vitabu 27 vyenye kuwa pia “neno la Mungu.” (1 Wathesalonike 2:13) Kupitia roho yake, Mungu aliongoza wanafunzi waaminifu wa Yesu Kristo waandike vitabu hivyo kwa muda mufupi zaidi​—karibu miaka 60 kuanzia mwaka wa 41 kisha kuzaliwa kwa Yesu mupaka mwaka wa 98 kisha kuzaliwa kwa Yesu. Waliandika zaidi sana katika Kigiriki, ndiyo sababu tunaita sehemu hiyo Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo, inajulikana pia kuwa Agano Jipya.

Vikiwa pamoja, vitabu hivyo 66 vyenye kuongozwa na roho ya Mungu vinafanyiza Biblia kamili​—ujumbe wa Mungu kwa wanadamu. Lakini, sababu gani tafsiri nyingine za Biblia zilifanywa? Tuone sababu kubwa tatu.

  • Kusaidia watu wasome Biblia katika luga yao.

  • Kuondoa makosa yenye yaliingizwa na watu wenye kufanya kopi, na kurudisha maandishi ya Biblia ya kwanza.

  • Kubadilisha maneno ya zamani yenye hayatumiwe tena.

Ona ni katika njia gani mambo hayo yalihusika katika tafsiri mbili za kwanza.

SEPTANTE YA KIGIRIKI

Miaka 300 hivi mbele ya kuzaliwa kwa Yesu, Wayahudi wenye elimu walianza kutafsiri Maandiko ya Kiebrania katika Kigiriki. Tafsiri hiyo ilifikia kujulikana kwa jina Septante ya Kigiriki. Sababu gani tafsiri hiyo ilifanywa? Ili kusaidia Wayahudi wengi, wenye wakati huo walisema Kigiriki kuliko Kiebrania, waendelee kujua “maandishi [yao] matakatifu”.​—2 Timotheo 3:15.

Tafsiri ya Septante ilisaidia pia mamilioni ya watu wenye hawakuwa Wayahudi, ni kusema, watu wenye kusema Kigiriki wajue mambo yenye Biblia ilifundisha. Namna gani? Profesa Wilbert Francis Howard anasema hivi: “Kuanzia mwaka wa 50 hivi, ilifikia kuwa Biblia ya Kanisa la Kikristo, na wamisionere wa kanisa hilo, walienda sinagogi kwa sinagogi ili ‘kusibitisha kwa maandiko kwamba Mesiya alikuwa Yesu.’” (Matendo 17:3, 4; 20:20) Kulingana na Frederick Fyvie Bruce, mutu wa elimu ya Biblia, hiyo ndiyo sababu Wayahudi wengi walifikia “kupoteza upendezi katika Septante.”

Kadiri wanafunzi wa Yesu waliendelea kupokea vitabu vya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo, walivitia vyote pamoja na tafsiri ya Septante ya Maandiko ya Kiebrania, na ikafikia kuwa Biblia kamili yenye tuko nayo leo.

VULGATE YA KILATINI

Karibu miaka 300 hivi kisha Biblia kumalizwa kuandikwa, Jerome, mutu wa elimu ya dini, alitokeza tafsiri ya Kilatini ya Biblia, ambayo ilifikia kuitwa Vulgate ya Kilatini. Tayari kulikuwa tafsiri mbalimbali za Kilatini, sasa, sababu gani ilikuwa lazima kuwe tafsiri mupya? Kitabu kimoja kinasema kwamba Jerome alipenda kurekebisha “mawazo yenye yalitafsiriwa mubaya, makosa yenye kuwa wazi na mambo yenye yaliongezwa ao kuondolewa bila sababu.”​—The International Standard Bible Encyclopedia.

Jerome alirekebisha mengi kati ya makosa hayo. Lakini kisha, wakubwa wa Kanisa walifanya kosa kubwa sana! Walisema kwamba Vulgate ya Kilatini ndiyo ilikuwa tafsiri moja tu ya Biblia yenye kukubaliwa na waliendelea kufanya hivyo kwa mamia ya miaka. Kuliko kusaidia watu wa hali ya chini waelewe Biblia, Vulgate ilifanya Biblia ikuwe kitabu chenye mutu yeyote hangeweza kuelewa kwa sababu watu wengi hawakujua Kilatini hata kidogo.

KUONGEZEKA KWA TAFSIRI ZA MUPYA

Wakati huohuo, watu waliendelea kutokeza tafsiri zingine za Biblia, kama vile Peshitta ya Kisiria yenye kujulikana sana katika miaka ya 400 hivi kisha kuzaliwa kwa Yesu. Ni kufikia tu miaka ya 1300, ndiyo bidii zilifanywa tena ili kupatia watu wa kawaida Maandiko katika luga za kienyeji.

Katika sehemu ya mwisho ya miaka ya 1300, katika Uingereza, John Wycliffe alianza mupango wa kuacha luga yenye haitumiwe na watu kwa kutokeza Biblia katika Kiingereza, luga yenye watu wa inchi yake walikuwa wanaelewa wakati huo. Muda kidogo kisha, njia za kuchapisha za Johannes Gutenberg ziliwezesha watu wa elimu ya Biblia kutokeza na kugawanya tafsiri za Biblia katika luga nyingi zenye watu walizungumuza katika Ulaya.

Wakati tafsiri za Kiingereza ziliendelea kutokezwa, wachambuzi walijiuliza kama ilikuwa lazima kabisa kuwa na tafsiri mbalimbali katika luga moja. John Lewis, padri mwenye aliishi katika miaka ya 1700 katika Uingereza, aliandika hivi: “Luga inazeeka na maneno yake yanakosa kueleweka muzuri, kwa hiyo, ni lazima kurekebisha Tafsiri za zamani ili kuzifanya zipatane na Luga yenye kutumiwa, na zieleweke na kizazi chenye kuishi.”

Leo, ni mwepesi kuliko zamani kwa watu wa elimu ya Biblia kurekebisha tafsiri za zamani. Wanaelewa sasa muzuri luga yenye ilitumiwa zamani ili kuandika Biblia, na wako na maandishi ya zamani ya maana ya Biblia yenye walivumbua hivi karibuni. Mambo hayo yanasaidia kujua kama maandishi ya zamani ya Biblia yalisema nini kabisa.

Kwa hiyo, ni muzuri kabisa kuwa na tafsiri za mupya za Biblia. Bila shaka, ni lazima kuwa muangalifu kuhusu tafsiri fulani kati yazo.a Lakini kama watu wenye kurekebisha Biblia wamechochewa na upendo wa kweli kwa Mungu ili kutokeza tafsiri mupya ya Biblia, kazi yao inaweza kutuletea faida kubwa.

Ili kusoma Biblia katika luga mbalimbali ao kwenye chombo chako cha kielektroniki, fungua www.jw.org. Fungua kichwa MACHAPISHO > BIBLIA.

a Ona habari “Jinsi ya Kuchagua Tafsiri Nzuri ya Biblia” katika Munara wa Mulinzi wa tarehe 1 Mwezi wa 5, 2008.

JINA TAKATIFU LA MUNGU KATIKA BIBLIA

Jina la Mungu katika kipande cha maandishi ya Septante ya tangu wakati wa Yesu

Jina la Mungu katika kipande cha Septante cha tangu siku za Yesu

Biblia Takatifu Tafsiri ya Ulimwengu Mpya inatumia jina takatifu la Mungu, Yehova, katika Maandiko ya Kiebrania na Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo. Biblia nyingi za leo hazifanye hivyo. Lakini zinatumia “Bwana” kuliko Yehova. Watafsiri fulani wanasema kwamba, sababu moja ya kufanya hivyo ni kwamba Tetragramatoni (YHWH), jina la pekee la Mungu, haikupatikana katika tafsiri ya Kigiriki ya Septante ya Maandiko ya Kiebrania. Lakini, hiyo ni kweli?

Kati ya mwaka wa 1940 na mwaka wa 1950, vipande fulani vya zamani sana vya Septante vyenye vilikuwa katika siku za Yesu vilipatikana. Viko na jina takatifu la Mungu lenye kuandikwa katika herufi za Kiebrania. Inaonekana kwamba, kisha miaka kupita, watu wenye kufanya kopi, waliondoa jina la Mungu na kulibadilisha na Kyʹri·os, neno la Kigiriki lenye kumaanisha “Bwana.” Tafsiri ya Ulimwengu Mpya inarudisha jina la Mungu kwenye nafasi zake zenye kufaa katika Maandiko.

MAKOSA YAMEINGIA KATIKA BIBLIA?

Kitabu cha Kunjwa cha Isaya cha Bahari ya Chumvi

Kitabu cha Kukunjwa cha Isaya cha Bahari ya Chumvi chenye kuwa na miaka 2000. Kinafanana sana na kitabu cha Isaya chenye kuwa katika Biblia leo

Ni kweli kwamba watu wenye kufanya kopi za Biblia walifanya makosa. Lakini, hakuna hata moja kati ya makosa hayo yenye imeharibu ujumbe wa Biblia. “Hakuna fundisho la imani ya Kikristo lenye linategemea mabishano katika namna ya kuelewa mambo.”​—Our Bible and the Ancient Manuscripts.

Waandishi Wayahudi walifanya makosa madogo tu. “Waandishi Wayahudi wa mamia ya miaka ya kwanza ya Ukristo walifanya kopi na kurudilia upya kopi ya maandishi ya Biblia ya Kiebrania kwa uaminifu mukubwa sana.”​—Second Thoughts on the Dead Sea Scrolls.

Kwa mufano, kitabu cha kukunjwa cha Isaya chenye kilipatikana kati ya Vitabu vya Kukunjwa vya Bahari ya Chumvi ni cha miaka 1 000 mbele ya maandishi yenye yalikuwa yamekwisha kupatikana. Tunaweza kuona nini kama tunakilinganisha na maandishi yenye tuko nayo leo? “Ni mara chache tu ndio neno moja linaongezwa ao kuondolewa.”​—The Book. A History of the Bible.

Sasa ni mwepesi kuona na kurekebisha makosa​—kama vile kubadilisha utaratibu wa herufi, maneno, ao misemwa​—yenye yalifanywa na watu wenye kufanya kopi wenye hawakuwa waangalifu. “Hakuna vitabu vya zamani katika ulimwengu vyenye kushuhudia utajiri kama huo wa maandishi mazuri kama vile Agano Jipya.”​—The Books and the Parchments.

“Waamini wenye kusamini Biblia wanaweza kupata uhakika zaidi kupitia upatano kamili wenye kuonekana kati ya vipande vya maandishi ya Biblia vya zamani zaidi vya Misri, na maandishi yenye kupatikana mupaka sasa hata kama yalifanyiwa kopi katika mahali mbalimbali pa kufanyia kopi kwa mukono na pa kuchapishia katika Ulaya.”​—The Book. A History of the Bible.

Kwa hiyo, ujumbe wa Biblia umebadilishwa? Bila shaka, hapana!

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine