Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • wp19 na. 1 uku. 3
  • Mungu Ni Nani?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Mungu Ni Nani?
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2019
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Mungu Ni Nani?
    Biblia Inatufundisha Nini?
  • Biblia Inafundisha Nini juu ya Mungu?
    Biblia Inafundisha Kabisa Nini?
  • Unahitaji Kujifunza Juu Ya Mungu
    Unaweza Kuwa Rafiki ya Mungu!
  • Dini, Mungu, ao Biblia, Vinaweza Kunisaidia Niwe na Furaha?
    Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2019
wp19 na. 1 uku. 3
Mwanaume mumoja anaangalia eneo fulani lenye kupendeza

Mungu Ni Nani?

Watu wengi wanasema kama wanamuamini Mungu. Lakini ukiwauliza Mungu ni nani, utapata majibu yenye kuwa tofauti. Watu fulani wanaona kuwa Mungu ni muamuzi mukali, mwenye anapenda tu kupatia watu malipizi juu ya makosa yao. Wengine wanamuona kuwa mwenye upendo sikuzote na mwenye kusamehe, hata wafanye nini. Na wengine wanaamini kama Mungu iko mbali sana na kama hatuhangaikie. Kwa sababu ya ile mawazo yenye kupingana, watu wengi wanaweza kuona tu kama haiwezekane kujua Mungu ni nani.

Ni jambo la maana kumujua Mungu? Ndiyo kabisa. Kumujua Mungu muzuri zaidi kunaweza kukusaidia ukuwe na maisha yenye kusudi na yenye maana. (Matendo 17:26-28) Kadiri unamukaribia Mungu, ni vile atakupenda na kukusaidia. (Yakobo 4:8) Mwishowe, kuwa na ujuzi wa kweli juu ya Mungu, kunaweza kukusaidia upate uzima wenye hauna mwisho.​—Yohana 17:3.

Namna gani unaweza kumujua Mungu? Fikiria mutu fulani mwenye unajua muzuri, kwa mufano, rafiki yako wa karibu. Namna gani ule urafiki ulikomaa? Bila shaka, ulijua jina la ule mutu, sifa zake, mambo yenye anapenda na mambo yenye anachukia, na pia mambo yenye alifanya na mambo yenye anapanga kufanya, na mambo ingine. Ni ile mambo njo ilikufanya umukaribie​—ulijifunza kumuhusu.

Vilevile, tunaweza kumujua Mungu kwa kuchunguza mambo yenye kufuata:

  • JINA LA MUNGU NI NANI?

  • YEYE NI MUTU WA NAMNA GANI?

  • NI MAMBO GANI YENYE MUNGU AMEFANYA?

  • ATAFANYA NINI?

  • KUMUJUA MUNGU KUNAWEZA KUKULETEA FAIDA GANI?

Gazeti hili limetayarishwa ili kukutolea majibu ya Biblia kwa ile maulizo. Habari zenye kuwa ndani zitakusaidia kumujua Mungu, lakini pia zitakusaidia kujua faida yenye utapata kama unakuwa na uhusiano wa pekee pamoja naye.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine