Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • wp19 na. 1 uku. 4-5
  • Jina la Mungu Ni Nani?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Jina la Mungu Ni Nani?
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2019
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • JUU YA NINI JINA LA MUNGU NI LA MAANA?
  • JINA LA MUNGU LINAONYESHA NINI?
  • Jina la Mungu
    Amuka!—2017
  • Sababu Gani Tunapaswa Kulitumia Jina la Mungu?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Tuliheshimu Jina Kubwa la Mungu
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Jina la Mungu—Je, Inafaa Tulitumie? Maana ya Jina Hilo Ni Nini
    Biblia Inafundisha Kabisa Nini?
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2019
wp19 na. 1 uku. 4-5

Jina la Mungu Ni Nani?

Wakati unatafuta ujue mutu fulani, pengine jambo la kwanza lenye ungependa kufanya ni kumuuliza, “Jina lako ni nani?” Kama ungemuuliza Mungu ile ulizo, atakupatia jibu gani?

“Mimi ni Yehova. Hilo ndilo jina langu.”​—Isaya 42:8.

Lile jina ni la mupya kwako? Inaweza kuwa vile, juu watafsiri wengi wa Biblia wanatumia jina la Mungu mara kidogo sana, ao hawalitumie. Mara mingi wanatumia jina la cheo “BWANA” pa nafasi ya lile jina. Lakini, jina la Mungu linapatikana mara 7 000 hivi mu maandiko ya kwanza-kwanza ya Biblia. Lile jina linafanyizwa na herufi ine za Kiebrania, ni kusema, YHWH, na tangu miaka mingi linaandikwa Yehova katika Kiswahili.

Jina la Mungu mu Kiebrania katika Kitabu cha Kukunjwa cha Bahari ya Chumvi

Kitabu cha Kukunjwa cha Zaburi cha Bahari ya Chumvi Karne ya kwanza K.K.Y., KIEBRANIA

Jina la Mungu katika tafsri ya Biblia ya Kiingereza ya Tyndale

Tafsiri ya Tyndale 1530, KIINGEREZA

Jina la Mungu katika tafsiri ya Biblia ya Reina-Valera katika Kihispania

Tafsiri ya Reina-Valera 1602, KIHISPANIA

Jina la Mungu katika Biblia ya Union Version katika Kichina

Union Version 1919, KICHINA

Jina la Mungu linapatikana mara mingi mu maandishi ya Kiebrania na mu tafsiri mingi za Biblia

JUU YA NINI JINA LA MUNGU NI LA MAANA?

Mungu mwenyewe anaona jina lake kuwa la maana. Hakuna mutu alimupatia Mungu lile jina; alijichagulia yeye mwenyewe. Yehova alisema hivi: “Hilo ndilo jina langu milele, na ni vile ninapaswa kukumbukwa kutoka kizazi mupaka kizazi.” (Kutoka 3:15) Mu Biblia, jina la Mungu linatajwa mara mingi zaidi kuliko majina yake ya cheo, kama vile Mweza-Yote, Baba, Bwana, ao Mungu, na linatajwa mara mingi zaidi kuliko jina lolote la pekee, kama vile Abrahamu, Musa, Daudi, ao Yesu. Pia, mapenzi ya Yehova ni kwamba jina lake lijulikane. Biblia inasema hivi: “Wajue kwamba wewe, mwenye jina lako ni Yehova, wewe peke yako ndiye Mwenye Kuwa Juu Zaidi, juu ya dunia yote.”​—Zaburi 83:18.

Yesu anaona lile jina kuwa la maana. Mu ile sala yenye kuitwa Baba Yetu ao Sala ya Bwana, Yesu alifundisha wanafunzi wake wamuombe Mungu hivi: “Jina lako litakaswe.” (Matayo 6:9) Yesu mwenyewe alisali kwa Mungu hivi: “Baba, tukuza jina lako.” (Yohana 12:28) Jambo lenye Yesu alitia pa nafasi ya kwanza mu maisha yake, ni kutukuza jina la Mungu; njo maana alisali hivi: “Nimewajulisha jina lako na nitalijulisha.”​—Yohana 17:26.

Watu wenye kumujua Mungu wanaona lile jina kuwa la maana. Zamani, watu wa Mungu walielewa kama ulinzi na wokovu wao ulikuwa na uhusiano na jina la pekee la Mungu. “Jina la Yehova ni munara wenye nguvu. Mwenye haki anakimbilia ndani na kupata ulinzi.” (Mezali 18:10) “Kila mutu mwenye anaitia jina la Yehova ataokolewa.” (Yoeli 2:32) Biblia inaonyesha kama jina la Mungu lingetambulisha wale wenye kumutumikia. “Kwa maana vikundi vya watu vitatembea, kila mutu katika jina la mungu wake, lakini sisi tutatembea katika jina la Yehova Mungu wetu milele na milele.”​—Mika 4:5; Matendo 15:14.

JINA LA MUNGU LINAONYESHA NINI?

Lile jina linamutambulisha Mungu peke yake. Wasomi wengi wamefikia kusema kama jina Yehova linamaanisha “Yeye Anafanya Kuwa.” Yehova alisaidia watu waelewe maana ya jina lake wakati alizungumuza na Musa juu yake mwenyewe kwa kusema hivi: “Nitakuwa Kile Ninachagua Kuwa.” (Kutoka 3:14) Kwa hiyo, jina la Mungu linamaanisha mambo mingi zaidi ya cheo chake akiwa Muumbaji wa vitu vyote. Jina lake linaonyesha uwezo wake wa kujifanya yeye mwenyewe kuwa ao kufanya uumbaji wake ukuwe kitu chochote chenye anataka ili kutimiza kusudi lake. Hata kama majina ya cheo inaweza kuonyesha daraka la Mungu, mamlaka, ao nguvu zake, ni jina lake tu, Yehova, njo linaonyesha yeye ni nani na kile chenye anaweza kuwa.

Jina la Mungu linaonyesha kuwa anapendezwa na sisi. Maana ya jina la Mungu inaonyesha kuwa anaendelea kuonyesha upendo kwa uumbaji wake, kutia ndani sisi. Zaidi ya ile, kwa kufanya jina lake lijulikane, anapenda tumujue. Kwa kweli, ni yeye njo alikuwa wa kwanza kutuambia jina lake mbele hata tuanze kulifikiria. Ni wazi kuwa, Mungu hapendi tuwaze kuwa yeye ni roho fulani mwenye kuwa mbali na sisi na mwenye hatuwezi kuelewa, lakini anapenda tumuone kuwa Mutu wa kweli mwenye tunaweza kukaribia.​—Zaburi 73:28.

Kutumia jina la Mungu kunaonyesha kama tunapendezwa naye. Kwa mufano, unaweza kuomba mutu mwenye unapenda akuwe rafiki yako akuite mu jina lako la pekee. Utajisikia namna gani ikiwa ule mutu anaendelea kukataa kutumia jina lako? Bila shaka, unaweza kufikia kujiuliza kama ule mutu anapenda kabisa kuwa rafiki yako. Ni vile pia kumuhusu Mungu. Yehova ameambia wanadamu jina lake, na anatutia moyo tulitumie. Wakati tunafanya vile, tunamuonyesha Yehova kama tunapenda kumukaribia. Anatambua hata wale wenye “kufikiri sana juu [ao, “kusamini,” maelezo ya chini] ya jina lake”!​—Malaki 3:16.

Kujua jina la Mungu ni hatua ya kwanza ya maana yenye inatusaidia tumujue. Lakini ile haitoshe. Tunapaswa kutambua Mutu mwenye kuitwa kwa lile jina. Tunapaswa kujua yeye ni mutu wa namna gani.

JINA LA MUNGU NI NANI? Jina la Mungu ni Yehova. Lile jina linaonyesha kama ni Mungu tu njo Mutu mwenye anaweza kutimiza kusudi lake

MUNGU ALITOKA WAPI?

Ile ni ulizo yenye watu wengi wamejiuliza. Pengine wewe pia umekwisha kujiuliza vile. Ile ulizo inaweza kuulizwa tena hivi: Kama kuko mwenye alitokeza ao kuumba ulimwengu na kila kitu chenye kuwa ndani yake, Mungu alitoka wapi?

Wanasayansi wengi wanakubali kama ulimwengu ulikuwa na mwanzo. Kupatana na wazo hili la musingi, mustari wa kwanza wa Biblia unasema hivi: “Hapo mwanzo Mungu aliumba mbingu na dunia.”​—Mwanzo 1:1.

Ulimwengu haungeweza kujiumba wenyewe; haungetokea bila kutokezwa. Kitu hakiwezi kutokea pasipo kitu kingine. Kama hakukuwa kitu mbele ulimwengu ukuwe, ulimwengu haungekuwako leo. Hata kama haiko mwepesi kwetu kuelewa kabisa, kunapaswa kuwa muumbaji mwenye amekuwako sikuzote. Yehova Mungu, mwenye nguvu zenye hazina mipaka, mwenye ni roho yenye hekima, njo ule Muumbaji.​—Yohana 4:24.

Biblia inasema hivi kumuhusu Mungu: “Mbele milima haijazaliwa ao mbele haujatokeza dunia na inchi yenye kuzaa, tangu milele mupaka milele, wewe ni Mungu.” (Zaburi 90:2) Kwa hiyo, Mungu amekuwako sikuzote. Njo maana, “hapo mwanzo” aliumba ulimwengu.​—Ufunuo 4:11.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine