Kumbusho kwa Mwandishi na Mwangalizi wa Utumishi
Kila mwaka, tangazo linatolewa katika Huduma Yetu ya Ufalme ya Februari, linalomwomba mwandishi na mwangalizi wa utumishi ‘kuchunguza utendaji wa mapainia wa kawaida wote.’ Uchunguzi huo unaopaswa kufanywa katika mwezi huu wa Machi una kusudi gani? Kuamua ni nani anayehitaji msaada ili kufikia kiwango chake cha saa tangu sasa hadi mwishoni mwa mwaka.
Mapainia wa kawaida wanapaswa kupitisha saa 1 000 kila mwaka katika huduma. Mwishoni mwa mwezi wa Februari, wengine wanafikia kutambua kwamba wanapungukiwa na kiasi fulani cha saa, jambo hilo linaweza kuwavunja moyo. Mara nyingi wazee wanakuwa na uwezo wa kuwasaidia mapainia, kwa kuwatia moyo na kwa kuwatolea mashauri yenye kutenda kazi. Msaada huo wa wazee unaweza kuwa wa maana sana na pia kumtolea painia nafasi ya kufikia kiwango chake cha wakati, badala ya kuacha utumishi wake.
Mapainia watakuwa wenye shukrani kwa ufikirio wa kutoka moyoni ambao wazee wanawaonyesha kwa upande huo. Kutaniko litafaidika pia na kuwapo kwa mapainia wenye furaha katika huduma na ambao wanatimiza kiaminifu kazi yao.