Tuongoze Mafunzo Ya Biblia Yenye Kufanya Maendeleo
1 Mganga mmoja wa kike mtanzania, binti mmoja mwajentina na mama mmoja wa familia mletoni wana mambo gani yenye kufanana? Kitabu-Mwaka 1997 (uku. 8, 46 na 56) kinaripoti kwamba wote watatu walifanya maendeleo ya haraka walipojifunza Biblia kwani walitamani kuchunguza kitabu Ujuzi zaidi ya mara moja kwa juma. Wahubiri walitiwa moyo, kwa kadiri iwezekanavyo, kujikaza kujifunza sura moja kwa kila somo. Hata hivyo, wamoja wanaona kwamba silo jambo rahisi. Ijapokuwa hilo linatokana kwa kadiri kubwa na hali na uwezo wa akili wa kila mwanafunzi, walimu wenye ujuzi walipata matokeo mazuri kwa kutumikisha madokezo yafuatayo.
2 Kama ilivyofasiriwa na nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Julai 1996, inafaa kufundisha wanafunzi kujitayarisha kwa ajili ya funzo. Mwanzoni kabisa, ingekuwa vizuri kufasiria na kuonyesha jinsi ya kufanya. Uwaonyeshe nakala yako binafsi ya kitabu Ujuzi. Tayarisheni pamoja somo la kwanza. Saidia wanafunzi kupata maneno makuu na misemwa inayojibu moja kwa moja ulizo la kitabu, kisha piga mistari au tia mistari kwa kalamu ya rangi. Wahubiri waliwatolea hata wanafunzi kalamu kwa ajili ya kupiga mistari. Watie moyo kutafuta maandiko yote wakati wa kujitayarisha kwao. Kwa kufanya hivyo, utawafundisha kujitayarisha ili kuhudhuria kwenye funzo la kitabu la kutaniko na kwenye funzo la Mnara wa Mlinzi.—Lk. 6:40.
3 Mwalimu mzuri hasemi sana, lakini anafanya mwanafunzi aseme. Anaepuka kutawanya mawazo juu ya nukta za ziada. Angepaswa kutoa maelezo ya ziada ikiwa tu hilo ni lazima, na badala yake atakazia nukta kubwa za somo. Wamoja waliwatolea wanafunzi wao vichapo ambavyo vilijibu maulizo yao. Zaidi ya hilo, watu walio tayari kujifunza wataweza kukamilisha ujuzi wao kwa kuhudhuria kwenye mikutano ya kutaniko.
4 Si lazima kusoma maandiko yote yanayotajwa. Tunaweza kufasiria nukta fulani kubwa kutokana na maandiko yanayonukuliwa katika fungu. Wakati wa kujikumbusha, kazia maandiko ya muhimu yaliyochunguzwa na mtie mwanafunzi moyo kuyalinda akilini.
5 Kila Somo Lingepaswa Kudumu Muda Gani?: Usiweke kikomo kwamba funzo ni lazima liendeshwe tu kwa muda wa saa moja. Wamoja wana wakati na labda wanatamani kujifunza kwa muda mrefu zaidi, au zaidi ya mara moja kwa juma. Mwanafunzi ambaye anajiweza atapatia ndani faida.
6 Leo, mamia ya maelfu ya wapya wanamsifu Yehova na, kama inavyoonyeshwa na Isaya 60:8, “wanakuja wakiruka kama wingu, na kama njiwa kwa madirisha yao” katika makutaniko ya watu wake. Tutimize hivyo sote sehemu yetu na tushirikiane kwa ukaribu na Yehova, huku akichochea kukusanywa kwa watu wanaofanana na kondoo.—Is. 60:22.