Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 8/99 uku. 1
  • Elimu ya kimwili na miradi yako ya kiroho

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Elimu ya kimwili na miradi yako ya kiroho
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1999
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Faidika Kikamilifu na Shule Yako
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Namna ya Kujiwekea na Kufikia Miradi ya Kiroho
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2022
Huduma Yetu ya Ufalme—1999
km 8/99 uku. 1

Elimu ya kimwili na miradi yako ya kiroho

1 Kupata elimu nzuri ya msingi wakati unapokuwa kijana kunaweza kukutolea ustadi wa shule unaohitajiwa ili usome na kuandika vizuri, na kuwa na uelewevu wa jumla wa jiografia, historia, hesabu, na sayansi. Kwa kufanya hivyo, unaweza kujifunza jinsi ya kufikiri bila matatizo, kuchanganua matukio, kutatua matatizo, na kuanzisha mawazo yenye kuzaa matunda. Masomo kama hayo yatakuwa yenye mafaa katika maisha yako yote. Elimu yako ya kimwili inawezaje kuhusiana na miradi yako ya kiroho katika maisha na kukusaidia kupata “hekima nzuri na busara”?—Mez. 3:21, 22.

2 Uwe mwenye mafaa katika utumishi wa Mungu: Unapokuwa shuleni, uwe mwangalifu darasani na utimize migawo yako ya kazi za kufanya nyumbani vizuri. Ikiwa mazoea ya kusoma na kujifunza yanakuwa rahisi kwako, unaweza kuchunguza Neno la Mungu kwa urahisi zaidi na kujifanya ubaki mwenye nguvu kiroho. (Mdo. 17:11) Ujuzi wenye kupanuka utakusaidia kusimulia na watu wa malezi, mapendezi, na imani mbalimbali unapokutana nao katika huduma. Elimu unayoipata shuleni itakuwa yenye mafaa kadiri unavyotimiza madaraka yako ya Kikristo katika tengenezo la Mungu.—Linganisha 2 Timotheo 2:21; 4:11.

3 Jifunze kujitegemeza: Ikiwa unajikaza, unaweza kujifunza ufundi unaohitajiwa ili kupata riziki baada ya kumaliza masomo. (Linganisha 1 Timotheo 5:8.) Chagua kwa makini mambo ya kujifunza. Badala ya kukaza fikira juu ya mambo yanayotoa nafasi ndogo kwa ajili ya kazi, fikiria kujifunza kazi ya mikono au ufundi utakaokuwezesha kupata kazi yenye kufaa. (Mez. 22:29) Mazoezi kama hayo yatafanya iwezekane kwako kujitegemeza ikiwa unaamua kutumikia mahali ambapo uhitaji ni mwingi zaidi.—Linganisha Matendo 18:1-4.

4 Kupata elimu nzuri ya msingi wakati unapokuwa shuleni kunaweza kukusaidia kupanua huduma yako. Tumika kwa bidii ili kupata ufundi unaohitajiwa ili kujitegemeza huku ukienda mbele katika utumishi wa Yehova. Hivyo, masomo yako yatatumika ili kukusaidia ufikie miradi yako ya kiroho.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine