Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 8/99 uku. 7
  • Programu mpya ya mkusanyiko wa pekee wa siku moja

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Programu mpya ya mkusanyiko wa pekee wa siku moja
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1999
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Programu mpya ya kusanyiko la pekee la siku moja
    Huduma Yetu ya Ufalme—2000
  • Programu Ya Kusanyiko La Pekee La Siku Moja Lijalo
    Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Programu Ya Kusanyiko La Mzunguko Lijalo
    Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Programu Mpya ya Kusanyiko la Pekee la Siku Moja
    Huduma Yetu ya Ufalme—2001
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1999
km 8/99 uku. 7

Programu mpya ya mkusanyiko wa pekee wa siku moja

Programu ya mkusanyiko wa pekee wa siku moja kuanzia Septemba 1999 ni yenye kichwa: “Kuchunguza Ndani ya Mambo Yenye Kina Kirefu ya Mungu.” (1 Kor. 2:10) Ni mambo gani ya thamani tutakayojifunza?

Katika kutafuta kwao ujuzi, watu wengi hawaburudishwi na yale wanayopata. Biblia hututia nguvu, kama itakavyoonyeshwa na mwangalizi wa mzunguko katika hotuba yake yenye kichwa “Kuchunguza Neno la Mungu Huleta Burudisho.” Msemaji mgeni ataonyesha uhusiano kati ya kuchunguza ndani ya mambo yenye kina kirefu ya Mungu na kuhubiri habari njema, atakapozungumzia ulizo “Unaonaje Kule Kuhubiri Ufalme?”

Wazazi wanawezaje kusaidia watoto wao wachimbe mbali katika Neno la Mungu? Madokezo yenye mafaa yatatolewa katika hotuba “Kazeni Kikiki Neno la Mungu Katika Watoto Wenu.” Kushirikiana na watu wakomavu kiroho katika kutaniko huwa na uvutano mzuri juu ya vijana Wakristo. Mifano ya jinsi wanavyopatwa na uvutano mzuri itaonyeshwa katika hotuba “Vijana Wanaojifunza Kutoka kwa Watu Wenye Umri Mkubwa Kuliko Wao.”

Yehova ni Mfunuaji wa siri. Kwa wakati huu, kwa nini tungepaswa kutafuta kwa bidii hazina ya kiroho yenye kufichwa? Katika hotuba “Yehova Hufunua Mambo Yenye Kina Kirefu Hatua kwa Hatua,” msemaji mgeni atafasiria mambo ambayo Yehova amefunua wakati uliopita na wakati wa sasa. Hilo litatia nguvu azimio letu la kuendelea ‘kuchunguza ndani ya mambo yenye kina kirefu ya Mungu.’

Pangeni sasa kuhudhuria. Wale wanaotaka kuonyesha wakfu wao kwa Yehova kupitia ubatizo wangepaswa kujulisha mwangalizi msimamizi mapema iwezekanavyo. Tamaa yetu kubwa ya kuchunguza katika Neno la Mungu itaimarishwa na mambo tutakayosikia. Kwa hiyo, usikose siku hiyo ya pekee ya maagizo ya kiroho!

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine