Je, wewe ni mwenye kuitikia upendo wa Kristo?
1 Akitafakari juu ya mwendo wa maisha wa Bwana-mkubwa wake, mtume Yohana aliandika: “Yesu, akiisha kuwa amependa walio wake mwenyewe waliokuwa ulimwenguni, aliwapenda hadi mwisho.” (Yn. 13:1) Mnamo kipindi hiki cha Ukumbusho, tutafikiri juu ya wonyesho mkubwa zaidi wa upendo wa Kristo. Tunaweza kuitikia upendo huo kwa kuonyesha imani katika dhabihu ya ukombozi, kwa kuwa na ushirika wenye bidii katika kazi ya kuhubiri na, kama Yesu, kwa kuvumilia “hadi mwisho.”—Mt. 24:13; 28:19, 20; Yn. 3:16.
2 Kuitikia upendo wa Kristo: Yesu alikuwa mwenye shughuli sana mnamo juma la mwisho la maisha yake duniani. (Mt. 21:23; 23:1; 24:3) Tukiwa waigaji wa Kristo, sisi pia tunachochewa na upendo ‘kufanya nguvu’ katika utumishi wa Yehova. (Luka 13:24, ZSB) Je, unaweza kufaidika na mipango kwa ajili ya utendaji wenye kuzidishwa wa kutoa ushahidi mnamo Aprili kwa kuongeza wakati unaopitisha katika huduma?
3 Mwaka huu, Chakula cha Jioni cha Bwana kinaanguka Siku ya Tatu jioni, Aprili 19. Ni watu wangapi watakaokuwa tayari kwa ajili ya tukio hilo la maana? Kwa kadiri kubwa, hilo lategemea sisi. Je, umefanya orodha ya wale unaopanga kualika—wanafunzi wako wa Biblia na watu wengine wenye kupendezwa, watu wa jamaa, watu unaojuana nao katika biashara, na washiriki wenzako wa shule? Je, umekwisha kuwaona na kuwatolea mwaliko wenye shauku? Je, utawakumbusha siku chache kabla ya Ukumbusho? Je, wanahitaji msaada wako ili kufika huko? Wazee pia ni wenye kualika wowote ambao wamekuwa wasiotenda katika huduma. Jambo la kwamba Ukumbusho utafanywa usiku wa katikati ya juma badala ya mwisho-juma halifanyi kuhudhuria kwa wote kuwe jambo lenye maana ndogo.
4 Uje ukiwa mwenye kujitayarisha: Ni jambo la maana kwetu kuwa wenye kujitayarisha na kuwa katika hali nzuri ya akili wakati tunapohudhuria Ukumbusho. Paulo aliwahimiza waamini wenzake walinde akilini uzito wa tukio hilo. (1 Kor. 11:20-26) Mnaweza kusoma sura 13 mpaka 17 za Injili ya Yohana wakati wa funzo lenu la Biblia la familia na kisha kuomba kila mshiriki wa familia aeleze kile ambacho dhabihu ya Yesu inamaanisha kwake. Pia, msisahau kufanya usomaji wa Biblia wa kila siku kwa ajili ya juma la Ukumbusho!
5 Upendo wetu kwa Kristo unakuwa wenye kina kirefu, na huo hauishii kwenye Aprili 19. Sisi ni wenye kuazimia kuonyesha upendo wetu kwake milele! Mwadhimisho wa Ukumbusho wa mwaka huu utatusaidia kutia nguvu azimio hilo.