“Hatuwezi kuacha kusema”
1 Yesu Kristo ni mwenye kuchunguza kwa ukaribu jinsi kazi ya kuhubiri inavyoendeshwa. (Mt. 28:20; Mk. 13:10) Ingawa kuna watangazaji wenye kutenda karibu milioni sita wanaotoa ushahidi katika mabara 234, hatupaswi kufikiri kwamba kutoa ushahidi kwetu kumemalizika. Mpaka Mungu atakaposema kwamba kazi imekwisha, “hatuwezi kuacha kusema” kuhusu mambo ambayo tumejifunza.—Mdo. 4:20, ZSB.
2 Tegemea roho ya Mungu: Shetani anatumia mikazo mikubwa ili kutuvunja moyo. (Ufu. 12:17) Mwili wetu wenyewe usiokamilika pia hutuletea matatizo mengi. Mambo kama hayo yanaweza kukengeusha uangalifu wetu kutoka kwenye ile kazi ya maana sana ya kuhubiri. Hata hivyo, ikiwa tunamtumaini Yehova, roho yake itatusaidia kupambana na kizuizi chochote kile.
3 Wakati kutaniko la Kikristo la karne ya kwanza lilipoteswa vikali, akina ndugu walimwomba Mungu katika sala awasaidie waendelee kusema neno lake kwa uhodari wote. Yehova alijibu sala yao, akiwapa roho yake na bidii na azimio vilivyohitajiwa ili kuendelea kuhubiri. Kama tokeo, waliendelea bila kuacha kutangaza habari njema kwa uhodari.—Mdo. 4:29, 31; 5:42.
4 Usiogope maneno yasiyofaa: Huenda maoni ya watu walio wengi na uvumishaji wa habari wenye uchongezi vikaelekea kuwa na matokeo yenye kutuogopesha. Hata hivyo, kumbuka maneno yenye uhodari ya Petro na mitume wengine mbele ya Mahakama kuu ya Wayahudi, maneno yanayoandikwa kwenye Matendo 5:29-32. Kama alivyokubali mwalimu wa Sheria Gamalieli, kazi ya Mungu haiwezi kupinduliwa. Kazi hiyo haitimizwi kwa nguvu zetu. Kazi hii kubwa inategemezwa na Mungu, naye peke yake ndiye anayeweza kuitimiza!—Zek. 4:6.
5 Acheni tumsihi Yehova kila siku atupatie roho yake ili kutusaidia kutangaza kwa bidii habari njema. Na tuseme, kama alivyosema Yeremia, kwamba ujumbe wa Ufalme ni kama moto wenye kuwaka katika mifupa yetu. (Yer. 20:9) Hatuwezi kubaki kimya!