Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 8/00 uku. 8
  • Mikutano hufaidi vijana

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Mikutano hufaidi vijana
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2000
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Sababu Gani Tunapaswa Kukusanyika Pamoja Ili Kuabudu?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2016
  • Utapata Faida Gani Kama Unaenda ku Mikutano ya Mashahidi wa Yehova?
    Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
  • Jinsi ya kupata furaha nyingi zaidi kutokana na mikutano
    Huduma Yetu ya Ufalme—1999
  • Kufaidika Kabisa na Mikutano kwa Ajili ya Mahubiri
    Huduma Yetu ya Ufalme—2006
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2000
km 8/00 uku. 8

Mikutano hufaidi vijana

1 Msichana mmoja tineja alisema: “Nyakati nyingine ninafikiri kwamba vijana ndio huwa na wakati mgumu zaidi katika maisha. Tunazungukwa na watu ambao hufanya uasherati, ambao hutumia dawa za kulevya, na ambao hunywa vileo.” Je, ni hivyo unavyofikiri? Ikiwa ni hivyo, ni nini unawaza kitakusaidia kupiganisha uvutano huo mbaya? Unahitaji imani, imani yenye nguvu katika unyofu wa njia za Yehova, kwa kuwa bila hiyo “haiwezekani kumpendeza vema.” (Ebr. 11:6) Kuhudhuria mikutano ya kutaniko kutakusaidia kutia nguvu imani yako ya Kikristo na azimio lako la kuepuka lililo baya.

2 Mikutano ina mengi ya kukutolea: Ni nini kinachofanya chakula kizuri pamoja na marafiki wa karibu kiwe chenye kufurahisha? Je, si mchanganyiko wa chakula chenye afya na ushirika wenye kupendeza katika hali yenye kuburudisha? Mikutano yetu hufanya tujisikie hivyohivyo, lakini katika maana ya kiroho.

3 Mambo yanayozungumziwa kwenye mikutano ni yenye kujenga, kuanzia mambo yanayohusu matatizo ya maisha ya kila siku mpaka kwenye mafunzo ya unabii mbalimbali wa Biblia wenye kuvutia. Mafundisho yenye kutumika yanatolewa ambayo hukufundisha jinsi ya kuishi maisha bora na kukabiliana na matatizo unayokutana nayo. Washiriki wanaopatikana kwenye mikutano ndio washiriki bora wanaoweza kupatikana mahali popote, nayo hali ya kiroho ni yenye kupendeza na iliyo salama. (Zab. 133:1) Si jambo la kushangaza kwamba kijana mmoja alisema: “Ninakwenda shuleni mchana wote mzima, na jambo hilo linanichosha. Lakini mikutano ni kama chemchemi ya maji jangwani, ambako ninaburudishwa ili nipate nguvu kwa ajili ya siku ya shule ijayo.” Mwingine alisema: “Nime[tambua] kwamba ushirikiano wa karibu pamoja na wengine wanaompenda Yehova unanisaidia nibaki karibu na yeye.”

4 Kwa kuwa mwenye kujiandikisha katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi, unajifunza kukusanya habari ya Kibiblia, kuitayarisha kama vile hotuba, na kuitoa kwa namna ya mazungumzo mbele ya wasikilizaji kwenye Jumba la Ufalme. Fikiria faida ya kuzoezwa kufundisha kwa ufundi kweli zenye kuokoa uhai katika Neno la Mungu! Ni mahali gani pengine ambapo vijana wanaweza kupata mazoezi yenye thamani kama hayo?

5 Jinsi ya kufaidika kikamili zaidi na mikutano: Ili kufaidika kikamili zaidi na mikutano, kuna mambo matatu ya maana sana yenye kuhusika. Hayo ni matayarisho, kushiriki, na mazoezi.

6 Jitayarishe kwa ajili ya hiyo: Panga wakati wa kujitayarisha kikawaida kwa ajili ya mikutano. Usiache kazi ya shule, kazi yenye kuchukua nusu ya wakati, au utendaji wa kujiburudisha vichukue wakati ambao unahitaji ili kurudilia kimbele habari zitakazozungumziwa kwenye kila mkutano. Kuwa na mazoea mazuri ni jambo linalosaidia. Kwanza kabisa, fuata bila kuchelewa programu ya kila juma ya usomaji wa Biblia inayopangwa kwa ajili ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi. Inaomba dakika chache tu kila siku ili kusoma na kutafakari sura zilizotolewa kuwa mgawo. Weka kando wakati ili kujitayarisha kwa ajili ya Funzo la Kitabu la Kutaniko na Funzo la Mnara wa Mlinzi. Wengine hufanya hivyo siku moja au mbili hivi kabla ya mikutano hiyo. Kwa kadiri iwezekanavyo, fanya hivyohivyo kwa ajili ya sehemu zinazopangwa katika Mkutano wa Utumishi kila juma.

7 Shiriki katika hiyo: Biblia inasema kwamba alipokuwa na umri wa miaka 12, Yesu alikutwa katika hekalu akisikiliza, akiuliza maulizo, na akitoa majibu. (Luka 2:46, 47) Ni kusema kwamba alihusika kikamili. Utafaidika zaidi na mikutano ikiwa unajitahidi kuishiriki.—Mez. 15:23.

8 Unahitaji kutenda kwa kukaza akili juu ya yale yanayofundishwa kwenye mikutano. Nyakati nyingine, kusikiliza hotuba ni kugumu zaidi kuliko kuitoa. Kwa nini? Huenda akili yako ikatangatanga wakati mtu mwingine anapokuwa akisema. Unawezaje kupiganisha hilo? Kwa kuandika yale yanayosemwa. Andika mambo ya maana ambayo utachunguza baadaye. Jambo hilo litakusaidia kufanya akili yako iendelee kukazwa juu ya programu. Pia, tafuta maandiko, na ufuate kadiri hayo yanavyosomwa na msemaji.

9 Kwa kuongezea, jifanyie mradi wa kushiriki katika kila mazungumzo ya maulizo na majibu kwenye mikutano. Utafaidika hata zaidi ikiwa unafikiria kwa uangalifu yale unayotaka kusema. Andiko la Mezali 15:28 linasema: “Moyo wa mwenye haki unafikili namna utakavyojibu.”

10 Jizoeze kufanya yale unayojifunza: Hatua ya mwisho ni kuhakikisha kwamba yale unayojifunza ‘yanatenda kazi ndani yako.’ (1 Thes. 2:13, AJ) Kadiri unavyotumikisha mambo mazuri unayojifunza kwenye kila mkutano, utamkaribia zaidi Yehova Mungu. Yeye atakuwa halisi kwako, nawe utapata furaha kubwa na kutosheka kadiri ‘unavyoendelea kutembea katika kweli,’ ukiifanya kuwa mali yako mwenyewe.—3 Yn. 4.

11 Enyi ndugu na dada vijana, kadiri mnavyojitayarisha kikawaida kwa ajili ya mikutano, kadiri mnavyoishiriki, na kadiri mnavyojizoeza kufanya yale mnayojifunza, mtafurahia kikamili mikutano. Wakati huohuo, mtapata faida yote iwezekanayo kutokana na hiyo. Imani yenu na azimio lenu la kubaki waaminifu kwa Baba yenu wa mbinguni, Yehova, vitatiwa nguvu.—Zab. 145:18.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine