Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • wp20 na. 1 uku. 12-13
  • Kweli Kuhusu Ufalme wa Mungu

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Kweli Kuhusu Ufalme wa Mungu
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2020
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Ufalme wa Mungu Ni Nini?
    Mungu Anataka Nini Kwetu?
  • Ufalme wa Mungu Ni Nini?
    Biblia Inatufundisha Nini?
  • Ufalme wa Mungu Ni Nini?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2020
  • Ufalme Wa Mungu
    Amuka!—2013
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2020
wp20 na. 1 uku. 12-13
Dunia, kama vile inaonekana katika anga, inaangaziwa na jua

Kweli Kuhusu Ufalme wa Mungu

Yesu alifundisha wafuasi wake kusali hivi: “Baba yetu mwenye kuwa mbinguni, jina lako litakaswe. Ufalme wako ukuje. Mapenzi yako yafanyike duniani kama mbinguni.” (Matayo 6:9, 10) Ufalme wa Mungu ni nini? Uko unafanya nini? Na juu ya nini tunapaswa kusali ukuje?

Yesu Ni Mufalme wa Ufalme wa Mungu.

Luka 1:31-33: “Utamupatia jina Yesu. Huyo atakuwa mukubwa na ataitwa Mwana wa Mwenye Kuwa Juu Zaidi; na Yehova Mungu atamupatia kiti cha ufalme cha Daudi baba yake, na atatawala akiwa Mufalme juu ya nyumba ya Yakobo milele, na Ufalme wake hautakuwa na mwisho.”

Ufalme njo ilikuwa kichwa kikubwa cha mahubiri ya Yesu.

Matayo 9:35: “Yesu akatoka ili kutembelea miji na vijiji vyote, akifundisha katika masinagogi yao na kuhubiri habari njema ya Ufalme na kuponyesha kila namna ya ugonjwa na kila namna ya uzaifu.”

Yesu alipatia wanafunzi wake alama yenye ingewasaidia kujua kama Ufalme uko karibu kuja.

Matayo 24:7: “Kwa maana taifa litasimama kupigana na taifa na ufalme kupigana na ufalme, na kutakuwa upungufu wa chakula na matetemeko ya inchi mahali pamoja kisha pengine.”

Leo, wanafunzi wa Yesu wanahubiri katika dunia yote kuhusu Ufalme.

Matayo 24:14: “Na hii habari njema ya Ufalme itahubiriwa katika dunia yote yenye kuikaliwa na watu ili kuwa ushahidi kwa mataifa yote, na kisha ule mwisho utakuja.”

Ufalme wa Mungu Ni Serikali ya Kweli Kabisa

Fasi kwenye unapatikana. Ufalme wa Mungu ni serikali ya kweli yenye Mungu amesimamisha mbinguni.​—DANIELI 2:44; MATAYO 4:17.

Kusudi. Ufalme wa Mungu utafanya dunia kuwa paradiso, kwenye wanadamu wote wataishi kwa amani na umoja na hawatagonjwaka tena wala kufa.​—ZABURI 37:11, 29.

Watawala. Mungu amemuweka Yesu kuwa Mufalme ili atawale mbinguni pamoja na watawala wenzake 144000, wenye wamenunuliwa kutoka katika dunia.​—LUKA 1:30-33; 12:32; UFUNUO 14:1, 3.

Raia. Raia wa Ufalme wataishi katika dunia na watajitiisha kwa kupenda chini ya utawala wa Yesu na watatii sheria za Ufalme.​—MATAYO 7:21.

Juu ya Nini Yesu Anastahili Kabisa Kutawala Wanadamu?

Wakati alikuwa ku dunia, Yesu alionyesha kama atakuwa mutawala mwenye uwezo na mwenye upendo kwa sababu

  • Alihangaikia maskini.​—LUKA 14:13, 14.

  • Alichukia rushwa na ukosefu wa haki.​—MATAYO 21:12, 13.

  • Alizuia nguvu za asili.​—MARKO 4:39.

  • Alikulisha maelfu ya watu.​—MATAYO 14:19-21.

  • Alisikilia wagonjwa huruma na aliponyesha wote wenye walikuwa wagonjwa.​—MATAYO 8:16.

  • Alifufua wafu.​—YOHANA 11:43, 44.

Faida Zenye Ufalme wa Mungu Unaweza Kukuletea Kuanzia Leo

Unaweza kuwa na maisha yenye furaha zaidi kuanzia leo kama unakuwa raia wa Ufalme wa Mungu. Kwa mufano, raia wa Ufalme

  • ‘Wanafuatia amani pamoja na watu wote.’​—WAEBRANIA 12:14.

  • Wanaishi kwa amani na umoja kwa sababu bibi na bwana wanapendana na kuheshimiana.​—WAEFESO 5:22, 23, 33.

  • Wako na maisha ya muzuri na yenye furaha kwa sababu “wanatambua uhitaji wao wa kiroho.”​—MATAYO 5:3.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine