Tujenge uthamini kuelekea vidio La Bible : le livre le plus ancien toujours d’actualité
Maulizo yafuatayo yanakazia mambo ambayo huenda umeona wakati ulipokuwa ukitazama vidio hii: (1) Ni mambo gani yanayotofautisha Biblia kuwa isiyoweza kulinganika? (2) Toa mfano wa jinsi Biblia, ingawa ni ya zamani, inakubaliana na sayansi ya kisasa. (3) Tunawezaje kuwa hakika kwamba Biblia ya sasa haikubadilika na kuwa tofauti na maandishi ya kwanza? (4) Ni nini alama kubwa ya maandishi inayopatikana katika hati za kale za Biblia, na jambo hilo linaingiza uhakika gani ndani yako? (5) Ni katika njia gani John Wycliffe, Johannes Gutenberg, William Tyndale, Mary Jones, na Charles Taze Russell walichangia katika kueneza Neno la Mungu ulimwenguni pote? (6) Kanisa lilipingaje vikali Biblia, lakini ni nini lililowezesha Biblia iokoke mpaka siku yetu? (7) Tengenezo la Yehova limetafsiri na kutokeza Biblia kwa kiasi gani? (8) Shauri lenye kutumika la Biblia limesaidiaje watu kushughulika na matatizo ya michezo ya fedha isiyozuilika (1 Kor. 13:4, 5; Efe. 5:28-33), na kujishughulisha sana na utajiri wa kimwili (Mt. 16:26)? (9) Kuna uhakikisho gani kwamba kutumikisha kanuni za Kimaandiko kunaweza kushinda chuki ya kitaifa, ya kikabila, na ya rangi ya ngozi katika ulimwengu? (10) Ni katika njia gani kujifunza yaliyomo ndani ya Biblia kumekuletea furaha kubwa zaidi? (11) Ni nani ambao unafikiri watafaidika na vidio hii, nawe utaitoaje kwao?