Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
MNARA WA MLINZI Nov. 15
“Watu fulani wamekuwa wakijiuliza ikiwa tunahitaji makanisa na mahekalu ili kuabudu Mungu. Unafikiri nini? [Acha mtu ajibu.] Tazama yale ambayo Biblia inasema kuhusu jambo hilo. [Soma Matendo 17:24.] Kwa hiyo, mahali pa ibada pangepaswa kutumiwa kwa kusudi gani? Gazeti hili linatoa jibu la Kimaandiko kwa ulizo hilo.”
Amkeni! Nov. 22
“Je, unafikiri ya kwamba siku fulani sayansi itamaliza ugonjwa na maradhi? [Acha mtu ajibu.] Toleo hili la Amkeni! linazungumzia maendeleo fulani ambayo sayansi imefanya. Linaonyesha pia kwa nini ni Muumba tu ndiye anao uwezo wa kumaliza magonjwa na kifo.” Soma Zaburi 146:3-5, na tolea mtu magazeti.
MNARA WA MLINZI Des. 1
“Leo, karibu kila mtu ana magumu ya fedha ili kuishi. Tatizo hilo pia linagusa makanisa, na maombi ya fedha yamekuwa yenye kuendelea hata zaidi. Je, unaona jambo hilo kuwa lenye kusumbua? [Acha mtu ajibu. Kisha soma 1 Wathesalonika 2:9.] Mnara wa Mlinzi unazungumzia kile ambacho Biblia inasema kuhusu jambo hilo.”
Amkeni! Des. 8
“Kwa sababu ya maogopesho ya ugaidi, wengi wanajiuliza ikiwa kusafiri kwa njia ya ndege ni jambo lenye usalama. Je, jambo hilo linakutia wasiwasi? [Acha mtu ajibu.] Biblia inakubali kwamba mtu yeyote anaweza kufikiwa na msiba. [Soma Muhubiri 9:11.] Hata hivyo, toleo hili la Amkeni! linazungumzia jinsi unavyoweza kuwa na usalama zaidi pia starehe unaposafiri kwa njia ya ndege.”