Mavazi Yenye Mpangilio Mzuri Yanaonyesha Kwamba Tunamheshimu Mungu
1 Karibuni tutakuwa na pendeleo la kuwa waalikwa wa Yehova kwenye Mkusanyiko wa Wilaya wa 2003, wenye kichwa “Mtukuzeni Mungu.” Sisi ni wenye shukrani kama nini kwa Yehova kwa kutualika kwenye karamu hiyo ya kiroho yenye kutajirisha! Tunaweza kuonyesha kwamba tunamheshimu na tunathamini maandalizi yake ya kiroho kwa jinsi tunavyovaa na kujipamba.—Zab. 116:12, 17.
2 Safi na Wenye Utaratibu: Sura yetu inapaswa kuonyesha viwango vya Mungu, ambaye ni safi na mwenye utaratibu. (1 Kor. 14:33; 2 Kor. 7:1) Utu wetu, nywele zetu, na makucha yetu yanapaswa kuwa safi, na tunapaswa kujipamba vizuri. Kujipamba ovyoovyo ni jambo la kawaida leo. Hata hivyo, jambo la kwamba mchezaji wa sinema au bingwa wa michezo anavaa na kujipamba ovyoovyo halimtolei Mkristo sababu ya kufanya hivyo. Ikiwa tunafuata mitindo ya sasa, inaweza kuwa vigumu kwa watu kutofautisha kati ya wale wanaomtumikia Mungu wa kweli na wale wasiomtumikia.—Mal. 3:18.
3 Mavazi Yanayofaa Wahudumu Wakristo: Mtume Paulo alipoandikia mwangalizi Mkristo Timotheo, alitia moyo “wanawake wajirembe wenyewe katika mavazi yenye mpangilio mzuri, pamoja na kiasi na utimamu wa akili, . . . katika njia inayofaa wanawake wanaodai kumstahi Mungu, yaani, kupitia kazi zilizo njema.” (1 Tim. 2:9, 10) Kuhakikisha kwamba mavazi yetu ni yenye mpangilio mzuri kunaomba kufikiri kwa uangalifu. Mavazi yanapaswa kuwa safi na yenye kiasi—si yenye rangi nyinyi kupita kiasi, yenye kuamsha nyege, au yenye kuchochea mawazo mabaya.—1 Pet. 3:3.
4 Paulo alionya pia dhidi ya kupita kiasi katika “mitindo ya kusuka nywele na dhahabu au lulu au mvao ulio ghali sana.” (1 Tim. 2:9) Kuwa wenye kusawazika katika matumizi ya johari, vipodozi, na mapambo mengine ni mwendo wa hekima kwa wanawake Wakristo kufuata.—Mez. 11:2.
5 Shauri ambalo Paulo alitolea wanawake Wakristo linatumika pia likiwa kanuni kwa wanaume Wakristo. Akina ndugu wanapaswa kuepuka mitindo inayoonyesha mafikiri ya ulimwengu. (1 Yn. 2:16) Kwa mfano, katika nchi fulani mavazi makubwa-makubwa ni yenye kupendwa na watu wengi, lakini mtindo huo hautoi sura inayofaa mhudumu wa Mungu.
6 Katika Shughuli za Wakati wa Mapumziko: Wanapohudhuria programu, ndugu na dada wengi hutoa mfano bora katika mambo ya kuvaa na kujipamba. Lakini ripoti zinaonyesha kwamba wengine wanakosa kuwa waangalifu wanaposafiri kwenda au kutoka kwenye mkusanyiko au wanaposhiriki katika shughuli za wakati wa mapumziko baada ya vipindi vya mkusanyiko. Kwa kweli, sura yetu binafsi—iwe kwamba ni muda wa programu au nyakati nyingine—ina uvutano juu ya jinsi wengine wanavyoona watu wa Mungu. Kwa kuwa tunavaa kadi zetu za utambulisho kwa ajili ya mkusanyiko, tunapaswa wakati wote kuvaa kwa namna inayofaa wahudumu Wakristo. Mara nyingi hilo linachochea wengine kutupongeza na linatutolea nafasi ya kutoa ushahidi.—1 Kor. 10:31-33.
7 Kama vile tabasamu ya kirafiki inavyoboresha jinsi sura yetu inavyoonekana, vivyo hivyo mavazi na kujipamba kwenye mpangilio mzuri kunatukuza ujumbe tunaopeleka na tengenezo tunalowakilisha. Watu fulani watakaotuona mwaka huu wakati wa Mkusanyiko wa Wilaya wenye kichwa “Mtukezeni Mungu” wanaweza kuchochewa waulize kwa nini tuko tofauti, na wanaweza mwishowe kusema: “Tutakwenda pamoja nanyi, kwa maana tumesikia [na kuona] ya kuwa Mungu ni pamoja nanyi.” (Zek. 8:23) Kila mmoja wetu na aonyeshe kwamba anamheshimu Yehova kupitia mavazi yetu na kujipamba kwetu.
[Study Questions]
1. Tunawezaje kuonyesha kwamba tunathamini mkusanyiko wetu wa wilaya unaokuja?
2. Kwa nini ni jambo la maana kwetu kuwa safi na wenye kujipamba vizuri?
3. Tunawezaje kuhakikisha kwamba sura yetu itapatana na shauri linalopatikana kwenye 1 Timotheo 2:9, 10?
4, 5. Ni mambo gani yanayoomba kuwa waangalifu ambayo waunaume na wanawake Wakristo wanapaswa kutii?
6. Kwa nini tunapaswa kudumisha kiwango cha juu katika mavazi yetu na kujipamba kwetu tunaposafiri kwenda au kutoka kwenye mkusanyiko, tunapokuwa kwenye mkusanyiko, na baada ya vipindi vya mkusanyiko kila siku?
7. Mavazi yetu na kujipamba kwetu kwenye mpangilio mzuri kunaweza kuwa na uvutano gani juu ya wengine?
[Picture on page 5]
Sura Yako na Ilete Heshima
▪ Unaposafiri
▪ Kwenye mkusanyiko
▪ Wakati wa shughuli za mapumziko