Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 8/03 uku. 7
  • Programu Mpya ya Kusanyiko la Pekee la Siku Moja

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Programu Mpya ya Kusanyiko la Pekee la Siku Moja
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2003
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Endelea Kuwa na Moyo Usiogawanyika Kumuelekea Yehova
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Programu Ya Kusanyiko La Pekee La Siku Moja Lijalo
    Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Programu Mpya ya Kusanyiko la Pekee la Siku Moja
    Huduma Yetu ya Ufalme—2005
  • Programu mpya ya kusanyiko la pekee la siku moja
    Huduma Yetu ya Ufalme—2000
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2003
km 8/03 uku. 7

Programu Mpya ya Kusanyiko la Pekee la Siku Moja

Leo, kuna habari nyingi kuhusu kulinda moyo wetu halisi katika hali nzuri ili kuwa na maisha marefu na yenye furaha zaidi. Hali ya moyo wetu wa mfano ni ya maana hata zaidi. Kwa hiyo, programu ya kusanyiko la pekee la siku moja litakaloanza mnamo Septemba 2003 itakuwa na kichwa chenye kufaa: “Tutumikie Yehova kwa Moyo Kamili.” (1 Nya. 28:9) Tunaweza kutazamia kujifunza nini?

Mwangalizi wa mzunguko atazungumzia habari “Tusaidie Wengine Wamtumikie Yehova kwa Furaha.” Mahojiano yatakazia shangwe inayotokana na kusitawisha kupendezwa na kujifunza Biblia na watu wanaotaka kumtumikia Yehova. Bila shaka, wahudhuriaji wote watapata faraja na kitia-moyo kutokana na hotuba ya kwanza ya msemaji mgeni, “Tulinde Mioyo Yetu Katika Ulimwengu Wenye Taabu.” Kipindi cha asubuhi kitamalizika kwa hotuba ya ubatizo.

Kisha mchana-kati, sehemu “Tutoe Msaada” itazungumzia jinsi tunavyoweza kusaidia wengine. Wazazi wanaweza kufanya nini ili kulinda mioyo ya watoto wao isipatwe na uvutano mbaya na kuwasaidia wamkaribie Yehova? Sehemu “Saidia Watoto Wako Wampende Yehova” itatoa mapendekezo yanayofaa na itaonyesha jinsi hilo linavyoweza kufanywa.

Je, tunafaidika na kila uandalizi ambao Yehova anafanya ili kulinda moyo wetu wa mfano ukiwa wenye afya na wenye nguvu? Hotuba ya mwisho ya msemaji mgeni, “Dumisha Moyo Kamili Katika Kutumikia Yehova,” itakazia sehemu nne za maana za programu yetu ya udumishaji wa kiroho. Ni kiasi gani cha wakati na jitihada tunachotumia katika sala yenye bidii, funzo la Neno la Mungu, kuhubiri kwa bidii, na kushirikiana na Wakristo wenzetu? Je, tunaweza kufanya maendeleo katika yoyote ya sehemu hizo?

Yehova anatoa mwaliko huu: “Weka moyo wako kusikiliza mafundisho, na masikio yako kwa maneno ya maarifa.” (Mez. 23:12) Panga sasa kuhudhuria siku hiyo yenye kuthawabisha ya fundisho hilo la Kimaandiko. Kufanya hivyo kutakutia nguvu uendelee kumtumikia Yehova kwa moyo kamili na kwa furaha.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine