Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 6/04 uku. 1
  • Yehova Anasaidia Wale Wanaomtegemea

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Yehova Anasaidia Wale Wanaomtegemea
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2004
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Tutumainie Ndugu na Dada Zetu
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2022
  • Mtegemee Yehova Kadiri Mwisho Unavyokaribia
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Programu Mpya ya Kusanyiko la Mzunguko
    Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Unatumainia Njia ya Yehova ya Kufanya Mambo?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2022
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2004
km 6/04 uku. 1

Yehova Anasaidia Wale Wanaomtegemea

1 Watu wengi wanaona kuwa fedha, nguvu, na uwezo wa kibinadamu ndio ufunguo wa kufanikiwa maishani. (Zab. 12:4; 33:16, 17; 49:6) Hata hivyo, wale wanaomwogopa Yehova na kumtegemea wanahakikishiwa na Biblia kwamba “yeye ni msaada wao na ngao yao.” (Zab. 115:11) Acheni tuchunguze sehemu mbili katika hizo tunahitaji kuonyesha kwamba tunamtegemea Yehova.

2 Tukiwa Wahudumu Wakristo: Tunaposhughulika na migawo ya kufundisha katika kutaniko au katika huduma ya shambani, tunapaswa kumtegemea Mungu wetu. Fikiria mfano wa Yesu. Ingawa alikuwa Mwana wa Mungu, hakutegemea hekima yake mwenyewe au uwezo wake lakini alimtegemea kabisa Baba yake wa mbinguni. (Yoh. 12:49; 14: 10) Sisi tunahitaji kufanya hivyo hata zaidi. (Met. 3:5-7) Ni kupitia baraka ya Yehova tu ndipo jitihada zetu za unyenyekevu zitamheshimu na kuletea wengine faida.—Zab. 127:1, 2.

3 Tunaonyesha kuwa tunamtegemea Yehova kwa kusali ili kupata mwongozo wake na msaada wa roho takatifu yake. (Zab. 105:4; Luka 11:13) Zaidi ya hilo, tunaonyesha kuwa tunamtegemea Mungu kwa kufanya mafundisho yetu yategemee neno lake, Biblia. Ujumbe walo una nguvu ya kugusa mioyo na kubadili maisha ya watu. (Ebr. 4:12) ‘Tunapohudumu kwa kutegemea nguvu ambazo Mungu anatoa,’ Yehova anatukuzwa.—1 Pet. 4:11.

4 Tunapopambana na Matatizo: Tunahitaji pia kumwomba Yehova msaada tunapopambana na mikazo na matatizo. (Zab. 46:1) Kwa mfano, mkubwa wa kazi anaweza kusita kutupatia likizo ili tuhudhurie mkusanyiko fulani, au tunaweza kupambana na hali ngumu katika maisha ya familia yetu. Tunaonyesha kwamba tunamtegemea Yehova kwa kumwomba kwa bidii na kufuata mwongozo anaotoa kupitia Neno na Tengenezo lake. (Zab. 62:8; 119:143, 173) Kwa kufanya hivyo, watumishi wa Yehova wanaona mkono wake wenye kusaidia katika maisha yao.—Zab. 37:5; 118:13, 16.

5 Yehova mwenyewe anatuhakikishia: “Amebarikiwa yule mtu hodari anayemtegemea Yehova, na ambaye Yehova amekuwa uhakika wake.” (Yer. 17:7) Na tuonyeshe kuwa tunamtegemea yeye katika yote tunayofanya!—Zab. 146:5.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine