Programu ya Familia—Mikutano ya Kutaniko
1 Ikiwa wewe ni mzazi Mkristo, unataka watoto wako wakomae katika kumpenda na kumtumikia Yehova na, mwishowe, wapate uzima wa milele katika ulimwengu mpya ulioahidiwa na Mungu. Unawezaje kuwasaidia watangulize ibada ya Yehova maishani mwao? Njia kuu ni kupitia mfano wako. (Met. 20:7) Dada moja, akikumbuka mfano wa mama yake aliye Shahidi, alisema: “Hakukuwa shaka yoyote ama tungeenda kwenye mkutano au la.” Hilo liliendelea kuwa na uvutano sana juu yake.
2 Je, familia yako inaelewa kusudi la mikutano ya kutaniko? Maagizo tunayopata kwenye makusanyiko hayo yanatutia nguvu ili tuendelee kufanya mapenzi ya Mungu, na ushirika ambao tunakuwa nao pamoja na ndugu zetu ni chanzo cha kitia-moyo chenye thamani kubwa. (Isa. 54:13; Rom. 1:11, 12) Hata hivyo, kusudi la kwanza la mikutano kama hiyo ni kumsifu Yehova “kati ya makundi yaliyokutanika.” (Zab. 26:12) Mikutano ya Kikristo inatutolea nafasi za kuonyesha upendo wetu kwa Yehova na kumwabudu.
3 “Endeleeni Kuangalia Sana”: Shukrani kwa kusudi takatifu la mikutano yetu itatuchochea ‘kuendelea kuangalia sana’ kwamba tusisitawishe hatua kwa hatua tabia ya kukosa mikutano kwa sababu ya mambo yenye umaana mdogo zaidi. (Efe. 5:15, 16; Ebr. 10:24, 25) Mnapofanya programu ya familia, mnaweza kuanza kwa kuonyesha wakati wa mikutano ya kutaniko. Kisha muwe waangalifu msiruhusu shughuli nyingine ziwazuie kuhudhuria mikutano. Muwe hakika kwamba kuhudhuria mikutano ni jambo la kutanguliza katika familia yenu.
4 Je, hatuchochewi tunaposoma kuhusu ndugu zetu wanaoshinda vizuizi ili kuhudhuria mikutano na mikusanyiko? Ijapokuwa hali zenu huenda ni afadhali kidogo, yaelekea nyinyi pia mnapambana na magumu. Shetani anazidi kufanya iwe vigumu kwa watu wa Mungu kumwabudu Yehova. Hata hivyo, muwe hakika kwamba watoto wenu hawatakosa kuona jinsi mnavyojitahidi kuazimia kwa bidii katika familia ili kuhudhuria mikutano ya kutaniko. Kwa kweli, kwa kufanya hivyo, mnaweza kuwapa zawadi ya kiroho ambayo haitasahauliwa kamwe.