Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Julai 15
“Kwa maelfu ya miaka katika historia ya kibinadamu, watu wametokeza mafundisho mbalimbali. Je, unafikiri kwamba inawezekana kujua ni mafundisho gani yaliyo ya kweli na yasiyo ya kweli? [Acha mtu ajibu.] Gazeti hili linazungumzia mahali ambapo unaweza kupata mafundisho ya kweli yanayompendeza Mungu.” Soma 2 Timotheo 3:16.
Amkeni! Julai 22
“Ni jambo lenye kuhuzunisha tunapoona mateso yenye kusababishwa na misiba ya asili. [Taja mfano unaojulikana kwenu.] Je, unafikiri kwamba misiba kama hiyo ni yenye kuongezeka? [Acha mtu ajibu.] Gazeti hili linazungumzia ulizo hilo. Linatoa pia faraja kwa ajili ya wale ambao wamepoteza wapendwa katika misiba kama hiyo.” Soma Yohana 5:28, 29.
Mnara wa Mlinzi Ago. 1
“Leo watu wengi wanasumbuliwa na mawazo ya kujiona kwamba hawafai kitu. Unafikiri ni nini kinachoweza kufanywa ili kuwasaidia? [Acha mtu ajibu.] Gazeti hili linazungumzia jinsi Biblia inavyoweza kusaidia watu kama hao kupata furaha ya kweli.” Kazia maandiko yaliyochapishwa katika herufi nzito nyeusi katika makala ‘Biblia Inaweza Kukusaidia Kupata Shangwe.’
Amkeni! Ago. 8
“Watu wengi wanaishi kwa kawaida katika woga. Unafikiri ni nini kinachotokeza hali hiyo ya woga? [Acha mtu ajibu.] Gazeti hili linatoa mapendekezo yenye kufaa ili tujilinde na hatari za kawaida. Linazungumzia pia ahadi ya Biblia kuhusu ulimwengu usio na woga.” Soma Isaya 11:9.