Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 5/06 uku. 3
  • Mfano wa Kuigwa na Watu wa Umri Zote

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Mfano wa Kuigwa na Watu wa Umri Zote
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2006
  • Habari za Kufanana na Zile
  • “Alitembea Pamoja na Mungu wa Kweli”
    Tuige Imani Yao
  • Kila Mmoja Anaweza Kujifunza Kutokana na Vidio Noé : il marchait avec Dieu
    Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Noa “Alitembea Pamoja na Mungu wa Kweli”
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Alilindwa “Akiwa Salama Pamoja na Wengine Saba”
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2006
km 5/06 uku. 3

Mfano wa Kuigwa na Watu wa Umri Zote

Noa alikuwa na uhusiano wa karibu sana na wa kirafiki pamoja na Mungu. Alijitoa ili kufanya mapenzi ya Yehova. “Alitembea pamoja na Mungu wa kweli” na kwa kufanya hivyo alibarikiwa. Alikuwa mfano unaostahili kuigwa na vijana pia wazee. (Mwa. 6:9) Video yenye kichwa Noé : il marchait avec Dieu (Noa—Alitembea Pamoja na Mungu) itakusaidia kuona maisha ambayo Noa alikuwa nayo, kwa nini alistahili baraka za Yehova, na jinsi unavyoweza kuiga sifa zake nzuri.

Tazama DVD ya Noa kisha ujiulize maulizo yafuatayo: (1) Malaika fulani walifanya jambo gani mbaya, na ni nani waliokuwa wanefili? (Mwa. 6:1, 2, 4) (2) Kwa nini watu walifikia kuwa waovu, na jinsi gani Mungu alijisikia kuhusu jambo hilo? (Mwa. 6:4-6) (3) Namna gani Noa alikuwa tofauti na watu wengine? (Mwa. 6:22) (4) Namna gani waovu waliharibiwa? (Mwa. 6:17) (5) Safina ilikuwa na ukubwa gani? (Mwa. 6:15) (6) Ni jambo gani lingine ambalo Noa alifanya, na je, watu walikubali? (Mt. 24:38, 39; 2 Pet. 2:5) (7) Kwa kila aina ya nyama, ni wanyama wangapi walioingizwa katika safina? (Mwa. 7:2, 3, 8, 9) (8) Mvua ilinyesha kwa muda wa siku ngapi, na dunia nzima ilifunikwa na maji kwa muda wa siku ngapi? (Mwa. 7:11, 12; 8:3, 4) (9) Kwa nini Noa na familia yake waliokoka? (Mwa. 6:18, 22; 7:5) (10) Safina ilitua wapi? (Mwa. 8:4) (11) Namna gani Noa alijua kwamba wakati ulifaa sasa ili kutoka katika safina? (Mwa. 8:6-12) (12) Noa alifanya nini alipotoka inje ya safina? (Mwa. 8:20-22) (13) Upinde wa mvua unaonyesha nini? (Mwa. 9:8-16) (14) ‘Kutembea pamoja na Mungu’ kunamaanisha nini? (Mwa. 6:9, 22; 7:5) (15) Ni jambo gani tunalopaswa kufanya ili kumwona Noa katika Paradiso? (Mt. 28:19, 20; 1 Pet. 2:21)

Hadisi hiyo ya Kibiblia ya Noa, aliyekuwa mtu mwaminifu na mtiifu, imekufundisha nini kuhusu jinsi wewe pia unavyoweza ‘kutembea pamoja na Mungu’ na kutegemea uwezo wa Yehova wa kuokoa watu wake wa siku hizi?—Mwa. 7:1; Met. 10:16; Ebr. 11:7; 2 Pet. 2:9.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine