Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Juni 15
“Je, unafikiri kwamba inawezekana kuwa mwenye furaha ijapokuwa matatizo yanayotupata? [Acha mtu ajibu.] Gazeti hili linaonyesha ni wapi tunapoweza kupata mwongozo ambao unaweza kutusaidia tushindane vizuri na matatizo ya maisha. Linazungumzia pia namna tumaini la kweli linavyotutia nguvu.” Soma Ufunuo 21:3, 4.
Amkeni! Juni
“Je, haukubali kwamba misiba iliyowapata watu hivi karibuni inaonyesha ulazima wa kusikiliza maonyo? [Acha Mtu ajibu.] Habari hii inazungumzia wale waliookoka upepo mkali unaoitwa Katrina na yale waliojifunza kutokana na msiba huo. Habari hii inaonyesha pia onyo ambalo sisi wote leo tunahitaji kusikiliza.” Onyesha habari hiyo inayoanzia kwenye ukurasa wa 14.
Mnara wa Mlinzi Julai 1
“Katika ulimwengu wa leo wenye kuvurugika, watu wengi wanajiuliza: ‘Kwa nini maisha ya watu ni yenye kujaa matatizo hivi? Ikiwa Mungu yupo, kwa nini yeye hafanyi jambo lolote ili kuondoa mateso?’ Je, umekwisha kujiuliza hivyo? [Acha mtu ajibu.] Gazeti hili linajibu maulizo hayo. Majibu ya maulizo hayo yanatoka katika Biblia.” Soma 2 Timotheo 3:16.
Amkeni! Julai
“Leo, ndoa nyingi zina magumu sana. Je, unafikiri kwamba watu wenye kuoana wanaweza kuishi vizuri ikiwa wanafuata shauri hili lenye kuongozwa na roho ya Mungu? [Soma Waefeso 4:32. Kisha acha mtu ajibu.] Toleo hili la Amkeni! linazungumzia kanuni za Biblia zilizosaidia watu wenye kuoana, kanuni ambazo zinaweza kutusaidia kufanya maisha ya ndoa yawe yenye furaha.”