Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi 15/04/07
“Inaonekana kwamba vitendo vya ukatili, au kutendea wengine bila huruma, vinaenea sana. [Toa mfano mmoja wa eneo lenu au mfano mmoja katika gazeti.] Je, umekwisha kujiuliza kwa nini watu wamekuwa hivyo? [Acha mtu ajibu.] Biblia ilitabiri kuongezeka kwa hali hiyo ya kutendeana bila huruma. [Soma 2 Timotheo 3:1-5.] Gazeti hili linajibu ulizo hili: ‘Je, ukatili utakwisha wakati wowote?’”
Amkeni! Mwezi wa 4
“Watu wengi wanajidai kuwa Wakristo. Kwa maoni yako, kuwa Mkristo kunamaanisha nini? [Acha mtu ajibu.] Ona jambo ambalo Yesu alisema hapa. [Soma Yohana 15:14.] Habari hii inaonyesha kwamba kusema tu eti mtu ni Mkristo hakutoshi.” Onyesha habari inayoanzia kwenye ukurasa wa 26.
Mnara wa Mlinzi 01/05/07
“Kifo cha mtoto kinafanya wazazi wawe na uchungu mwingi na wenye kuendelea. Unafikiri wazazi wanaweza kupata kitulizo wapi? [Acha mtu ajibu. Kisha soma Waroma 15:5.] Gazeti hili linazungumzia njia fulani ambazo Mungu anatumia ili kuwatuliza wale wanaolia.”
Amkeni! Mwezi wa 5
“Watu fulani wana mali, wakati ambapo mamilioni ya watu wengine wanaishi katika umaskini. Je, unafikiri kwamba tofauti hizo zitakwisha kabisa wakati fulani? [Acha mtu ajibu.] Ona jinsi Mungu anavyowaona wale walio masikini. [Soma Zaburi 22:24.] Gazeti hili linazungumzia tumaini ambalo Biblia inatolea watu walio masikini.”