Je, Unaweza Kuingia Katika “Mlango Mkubwa Unaoongoza Kwenye Utendaji”?
1 Wakati ambapo “mlango mkubwa unaoongoza kwenye utendaji” ulifunguliwa kwa Paulo, yeye alitumia kwa bidii nafasi hiyo ili kuendelea katika kazi ya kuhubiri ijapokuwa alipingwa na watu wengi. (1 Kor. 16:9) Leo wahubiri wa Ufalme 642,000 ulimwenguni pote wameingia katika mlango mkubwa wa utendaji wakiwa mapainia wa kawaida.
2 Hali Zinabadilika: Hata ikiwa hali tunazo sasa zinaweza kutuzuia tusifanye mengi katika utendaji wetu, hali zinabadilika. Kwa hiyo, ni jambo lenye hekima kuchunguza hali yetu wenyewe mara kwa mara, na tusingoje tu hali zilizo nzuri zaidi. (Mhu. 11:4) Je, wewe ni kijana anayekaribia kumaliza masomo ya juu? Je, wewe ni mzazi mwenye watoto ambao wanakaribia kuanza masomo? Je, unakaribia kupata pansio katika kazi yako? Mabadiliko kama hayo yanaweza kukutolea wakati wa kutosha na kukuwezesha kuwa painia wa kawaida. Dada fulani aliyepatwa na matatizo ya afya hapo mbele alikusudia kuwa painia alipokuwa na umri wa miaka 89. Kwa nini? Kwa kuwa alifanya zaidi ya mwaka mmoja bila kuingia hospitalini, aliona kwamba afya yake ingemwezesha kufanya upainia.
3 Paulo alipanga kwanza kutembelea ndugu zake katika jiji la Korintho. Lakini alibadili mipango yake kwa sababu ya habari njema. Wengi ambao ni mapainia wa kawaida leo walihitaji kubadili mambo mengi katika maisha yao ili kufanya kazi ya upainia. Watu fulani wamefanya maisha yao kuwa mepesi mpaka kutafuta kazi isiyowachukua wakati wote, kazi ambayo inahitajiwa ili kupata feza kwa ajili ya mahitaji yao madogomadogo. Wamefurahia pendeleo lao la utumishi. (1 Tim. 6:6-8) Watu wengine ambao ni wenye kuoana wamefanya mabadiliko katika namna yao ya kuishi ili mume tu afanye kazi, hilo likitolea muke nafasi ya kuwa painia.
4 Usiondoe haraka akilini wazo la kufanya upainia ukiogopa kwamba hautaweza kutimiza saa zinazoombwa. Unahitaji kufanya tu zaidi kidogo ya saa mbili kwa siku. Ikiwa unawaza kwamba hautaweza kutimiza saa zinazoombwa, pima kufanya upainia msaidizi mwezi moja au mbili lakini ukiwa na mradi wa kufikia saa 70. Hilo litakusaidia kuonja furaha inayotokana na kazi ya upainia. (Zab. 34:8) Ongea na wale ambao sasa ni mapainia. Labda wengine wameshinda magumu yaliyo sawa na yako. (Met. 15:22) Omba Yehova abariki yote unayojikaza kufanya ili kupanua kazi yako ya kuhubiri.—1 Yoh. 5:14.
5 Kazi ya Maana ya Kufuatia: Kutumika kama painia wa kawaida kunaleta baraka nyingi. Kunakuwezesha kupata furaha nyingi zaidi inayotokana na kutoa kwa uwingi. (Mdo. 20:35) Kufanya kazi ya upainia kutasaidia uwezo wako wa kutumia sawasawa Neno la Mungu la kweli uwe mzuri zaidi. (2 Tim. 2:15) Kutakutolea nafasi nyingi za kukusaidia uone kwamba Yehova anakutegemeza. (Mdo. 11:21; Flp. 4:11-13) Kufanya kazi ya upainia kutakusaidia pia kukomalisha sifa za kiroho, kama vile uvumilivu na kutakuwezesha kumkaribia Yehova. (Yak. 4:8) Je, unaweza kuingia katika mlango huo mkubwa wa utendaji na kuwa painia wa kawaida?
[Maulizo ya Funzo]
1. Ni ‘mlango gani mkubwa unaoongoza kwenye utendaji’ ambao unafunguliwa kwetu?
2. Kwa nini ni jambo lenye hekima kuchunguza hali yetu mara kwa mara?
3. Ni mabadiliko gani ambayo wengine wamefanya ili kuwa mapainia wa kawaida?
4. Tunaweza kufanya nini ikiwa tunawaza kwamba hatuwezi kutimiza saa zinazoombwa?
5. Kwa nini kazi ya upainia wa kawaida ni kazi ya maana ya kufuatia?