Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi 15/06/07
“Je, umetambua kwamba watu wengi leo wanajichagulia wao wenyewe kanuni zao za mema na mabaya? [Acha mtu ajibu.] Ona mfano wa mwongozo usio na mwisho unaopatikana katika Biblia. [Soma andiko moja katika kisanduku kwenye ukurasa wa 6-7.] Gazeti hili linaeleza jinsi tunavyopata faida tunapokubali kufuata kanuni za Biblia za mwenendo mwema.”
Amkeni! Mwezi wa 6
“Sisi wote tuna lazima ya feza ili kuishi. Je, unafikiri kwamba inawezekana mtu ajihangaishe sana ili kupata feza nyingi? [Acha mtu ajibu.] Ona jambo ambalo andiko hili linasema kuhusu matokeo ya kujitoa sana katika kufuatia sana mali. [Soma 1 Timotheo 6:10.] Gazeti hili linatoa mapendekezo fulani yenye kufaa kuhusu jinsi mtu anavyoweza kufanya maisha yake kuwa mepesi na kutosheka na feza kidogo.”
Mnara wa Mlinzi 01/07/07
“Je, umekwisha kujiuliza kwa nini watu wanatendewa vibaya kwa sababu ya rangi tofauti ya ngozi, inchi tofauti au kwa sababu wanasema luga tofauti? [Acha mtu ajibu.] Ona sababu inayotolewa hapa. [Soma 1 Yohana 4:20.] Gazeti hili linajibu ulizo hili: Je, inawezekana watu wa makabila tofauti wapatane?”
Amkeni! Mwezi wa 7
“Tofauti na wanyama ambao wanaongozwa na akili ya kisilika (instinct), wanadamu wana uwezo wa kuchagua kanuni ambazo watafuata katika maisha yao. Unafikiri tunaweza kupata wapi mwongozo unaostahili kutegemewa? [Acha mtu ajibu. Kisha soma Zaburi 119:105.] Gazeti hili linaeleza kwamba mwongozo unaopatikana katika Biblia ni mzuri sana kushinda miongozo yote.”