Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 7/07 uku. 1-2
  • “Mwenye Furaha Ni Mtu Anayeendelea Kuvumilia Jaribu”

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • “Mwenye Furaha Ni Mtu Anayeendelea Kuvumilia Jaribu”
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2007
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Maulizo ya Wasomaji Wetu
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2017
  • Uvumilivu Unathawabishwa
    Huduma Yetu ya Ufalme—2004
  • Namna ya Kuendelea Kuwa na Furaha Wakati wa Majaribu
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2021
  • Endelea Kubakia mu Tengenezo ya Yehova
    Tengenezo Yenye Kufanya Mapenzi ya Yehova
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2007
km 7/07 uku. 1-2

“Mwenye Furaha Ni Mtu Anayeendelea Kuvumilia Jaribu”

1 Wakristo wote wanapaswa kukutana na majaribu. (2 Tim. 3:12) Majaribu hayo yanaweza kuwa ugonjwa, matatizo ya kukosa feza, kishawishi fulani, mateso au mambo mengine. Shetani anatuletea majaribu ili kutufanya tupunguze mwendo, tupuuze kazi yetu ya kuhubiri, au hata tuache kumtumikia Yehova. (Ayu. 1:9-11) Basi, jinsi gani kuvumilia majaribu kunaweza kutokeza furaha?—2 Pet. 2:9.

2 Jitayarishe Kuhusu Majaribu: Yehova ametutolea Neno lake la kweli, kutia ndani habari za maisha na mafundisho ya Yesu. Kwa kusikiliza maneno ya Yesu na kufanya yale anayosema, tunaweka msingi wenye nguvu na hivyo tunajitayarisha kuhusu majaribu. (Luka 6:47-49) Pia tunapata nguvu kupitia mipango mingine—ndugu na dada zetu Wakristo, mikutano ya kutaniko na vitabu vyenye kutegemea Biblia ambavyo jamii ya mtumwa mwaminifu na mwenye busara inatutolea. Tunatumia sana sala ambayo ni zawadi kutoka kwa Mungu.—Mt. 6:13.

3 Yehova ametupatia pia tumaini. Tunapojenga imani yenye nguvu katika ahadi za Yehova, tumaini letu linakuwa “nanga ya nafsi, likiwa hakika na imara.” (Ebr. 6:19) Katika nyakati za Biblia, mashua hazikuondoka kwenye bandari (port) bila nanga, hata ikiwa hali ya hewa ilikuwa nzuri. Upepo mkali ulipotokea kwa kushitukia, kushusha nanga kungezuia mashua isijigonge kwenye mawe makubwa. Vivyo hivyo, kujenga imani katika ahadi za Mungu sasa, kutatufanya tusimame imara wakati upepo wa majaribu utakapotokea. Matatizo yanaweza kutokea kwa kushitukia. Katika Listra, ijapokuwa watu walikubali kwanza mafundisho ya Paulo na Barnaba, hali ilibadilika kwa haraka wakati Wayahudi wenye kupinga walipofika hapo.—Mdo. 14:8-19.

4 Kuvumilia Kunaleta Furaha: Kubaki imara katika kazi ya kuhubiri ijapokuwa tunapingwa kunatutolea amani ya akilini. Tunafurahi wakati watu wanatuhesabia kuwa wenye kustahili kuvunjiwa heshima kwa ajili ya Kristo. (Mdo. 5:40, 41) Kuvumilia majaribu kunatusaidia kukomalisha unyenyekevu, utii na uvumilivu mwingi zaidi. (Kum. 8:16; Ebr. 5:8; Yak. 1:2, 3) Kunatufundisha kumtegemea Yehova, kutumaini ahadi zake na kumkimbilia.—Met. 18:10.

5 Tunajua kwamba majaribu ni ya muda. (2 Kor. 4:17, 18) Majaribu yanatutolea nafasi mbalimbali za kuonyesha upendo wetu mwingi kwa Yehova. Kwa kuyavumilia, tunaweza kuonyesha kwamba mashitaka ya Shetani ni ya uongo. Kwa hiyo, hatuvunjike moyo! “Mwenye furaha ni mtu anayeendelea kuvumilia jaribu, kwa sababu akiisha kukubaliwa atapokea taji la uzima.”—Yak. 1:12.

[Kisanduku kwenye ukurasa wa 1]

(Inaendelea kwenye uku. wa 2)

[Kisanduku kwenye ukurasa wa 2]

Kuvumilia Jaribu (kutoka ukurasa wa 1)

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine