Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 8/07 uku. 1
  • Kumwabudu Yehova Mkiwa Familia

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Kumwabudu Yehova Mkiwa Familia
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2007
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Msaada kwa Familia
    Huduma Yetu ya Ufalme—2011
  • Jinsi Washiriki wa Familia Wanavyofanya Kazi Pamoja ili Kushiriki Kikamili—Katika Huduma
    Huduma Yetu ya Ufalme—1999
  • Ibada ya Familia—Namna Gani Unaweza Kuifanya Ifurahishe Zaidi?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Ibada ya Familia Ni Nini?
    Ni Nani Wanafanya Mapenzi ya Yehova Leo?
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2007
km 8/07 uku. 1

Kumwabudu Yehova Mkiwa Familia

1 Katika nyakati za Biblia, washiriki wa familia walifanya mambo mengi pamoja. Walifanya kazi zao za nyumbani za kila siku na jambo la maana zaidi ni kwamba, walimwabudu Yehova wakiwa familia. (Law. 10:12-14; Kum. 31:12) Mahali pengi leo, washiriki wa familia wanafanya mambo machache sana pamoja. Hata hivyo, tukiwa Wakristo tunajua umaana wa kufanya kazi mbalimbali tukiwa familia, zaidi sana mambo yenye kuhusiana na ibada. Bila shaka, hilo linamfurahisha sana Mwanzilishi wa familia anapoona familia zikimwabudu katika umoja!

2 Kuhubiri Pamoja: Kuhubiri habari njema pamoja kunatia nguvu vifungo vya familia. Kwa hiyo, zaidi ya kusindikiza kwenye mahubiri washiriki wengine wa kutaniko, mzee atatumika pia kwa ukawaida pamoja na muke na watoto wake. (1 Tim. 3:4, 5) Hata ikiwa waangalizi wanaosafiri wana mambo mengi ya kufanya, wanapanga wakati ili kuhubiri na wake zao.

3 Wazazi wanaohubiri na watoto wao wana uwezo wa kuwasaidia wafanye maendeleo wakiwa waeneza-evanjeli. Si kwamba watoto wataona tu furaha na kutosheka ambako wazazi wao wanapata katika kazi ya kuhubiri, lakini wataona pia wazazi wao wanavyoonyesha upendo wao kwa Yehova na kwa wanadamu wenzao. (Kum. 6:5-7) Jambo hilo halipaswe kupuuzwa eti kwa sababu watoto wanaopatikana nyumbani wamekwisha kukomaa. Mume na muke fulani walio na watoto wanaume watatu wenye miaka kati ya 15 na 21 wanaendelea kuwasindikiza kwa ukawaida katika kazi ya kuhubiri. Baba anasema hivi: “Tunawafundisha jambo fulani kila mara. Na tunafanya tuwezavyo ili wakati huo uwe wenye kufurahisha na wenye kutia moyo.”

4 Kutayarisha Pamoja: Washiriki wa familia mbalimbali wameona kwamba ni jambo lenye faida kutayarisha pamoja yale watakayosema katika mahubiri. Kwa kawaida, watoto wanafurahia kufanya vipindi vya mazoezi kwa kubadilishana na washiriki wa familia; watoto wanakuwa ndio wenye kuhubiri ao wanakuwa wasikilizaji. Wengine wanatumia dakika chache mwishoni mwa funzo la familia ili kufanya vipindi hivyo vya mazoezi.

5 Furaha yetu ni yenye kuongezeka tunaposhiriki, katika kazi za maana na zenye kutosheleza, pamoja na wale tunaowapenda. Ni jambo lenye kufurahisha kabisa washiriki wa familia wanapotumika pamoja katika kazi ya kuhubiri nyumba kwa nyumba, kurudilia watu na kuongoza mafunzo ya Biblia! Unapomwabudu Yehova hivyo pamoja na familia yako, unaweza kusema kwa furaha hivi: “Mimi na nyumba yangu, tutamtumikia Yehova.”—Yos. 24:15.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine