Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 10/07 uku. 1
  • Amkeni! ya Pekee ya Kutolea Watu Katika Mwezi wa 11!

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Amkeni! ya Pekee ya Kutolea Watu Katika Mwezi wa 11!
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2007
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Jinsi ya Kuanzisha Mafunzo ya Biblia na Watu Tuliotolea Magazeti
    Huduma Yetu ya Ufalme—2007
  • Tukomalishe Ufundi Wetu wa Kuhubiri—Tuwatolee Watu Kitabu Biblia Inafundisha
    Huduma Yetu ya Ufalme—2015
  • Amkeni! ya Pekee Itakayokaziwa Katika Mwezi wa Kenda
    Huduma Yetu ya Ufalme—2006
  • Tukomalishe Ufundi Wetu wa Kuhubiri—Kuonyesha Namna Funzo la Biblia Linafanywa kwa Kutumia Kitabu Biblia Inafundisha
    Huduma Yetu ya Ufalme—2014
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2007
km 10/07 uku. 1

Amkeni! ya Pekee ya Kutolea Watu Katika Mwezi wa 11!

1 Watu wengi wana maulizo yanayotoka moyoni mwao kuhusu umaana wa Biblia. Ikiwa ni watu ndio waliandika Biblia, kwa nini inaitwa Neno la Mungu? Kuna sababu gani zinazonifanya niitegemee ili iongoze hatua zangu? Ikiwa ninajikaza na kutoa wakati wangu ili kusoma na kujifunza Biblia, nitapata faida gani? Ni Biblia gani ambayo ninapaswa kutumia? Hayo ni maulizo fulani yanayojibiwa katika Amkeni! hii ya pekee ya mwezi wa 11 yenye kichwa “Je, Unaweza Kuitegemea Biblia?”

2 Tutapenda kutolea watu wengi sana Amkeni! hii ya pekee katika eneo letu. Ikiwezekana, shiriki katika mahubiri ya nyumba kwa nyumba pamoja na kutaniko lenu kila Siku ya Posho ya mwezi wa 11. Onyesha gazeti hii watu wa jamaa yako, majirani wako, wafanyakazi wenzako, walimu wenu, wanafunzi wenzako na watu unaowarudilia katika mahubiri. Chukua magazeti fulani ya Amkeni! hii unapokwenda kununua vitu ao unaposafiri. Wazee wamefanya ombi la magazeti zaidi ya Amkeni! hiyo ili kutaniko liwe na kiasi cha kutosha.

3 Anzisha Funzo la Biblia: Ikiwa unamtolea mtu gazeti, unaweza kuweka msingi wa funzo la Biblia mbele ya kumalizia mazungumzo yenu. Kwa mfano, unaweza kusema hivi: “Nitakaporudi tena, nitakuonyesha jibu ambalo Biblia inatoa kuhusu ulizo hili: ‘Mungu ana kusudi gani kwa dunia?’” Kisha utarudi na kitabu Biblia Inafundisha na kuonyesha mtu uliyezungumza naye ukurasa wa 4-5, ao mtazungumzia fungu la 1-3 katika sura ya 3. Ao unaweza kusema hivi: “Nitakaporudi tena, nitapenda tuzungumzie unabii wa Biblia wenye kutimizwa sasa.” Unaporudi, onyesha mtu unayezungumza naye sura ya 9 ya kitabu hicho na mzungumzie fungu la 1-3. Ao unaweza tu kumwambia hivi: “watu wengi wanaona kuwa vigumu kuelewa mambo wanayosoma katika Biblia. Nitakaporudi tena, nitapenda kukuonyesha jinsi unaweza kuelewa vizuri Biblia yako.” Unaporudi, umwonyeshe kitabu Biblia Inafundisha, na kuonyesha jinsi funzo la Biblia linavyofanywa.

4 Biblia tu ndiyo iliyo na “maandishi matakatifu,” yanayoweza kutufanya tuwe ‘wenye hekima kwa ajili ya wokovu.’ (2 Tim. 3:15) Kwa hiyo, sisi wote tutataka kushiriki kwa bidii katika kutolea watu Amkeni! hii ya pekee ili kuwasaidia wategemee Biblia!

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine