Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 11/07 uku. 4
  • Usisite Kuongoza Funzo la Biblia!

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Usisite Kuongoza Funzo la Biblia!
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2007
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Tuige Mufano wa Manabii—Amosi
    Huduma Yetu ya Ufalme—2013
  • Usijizuie Kuanzisha Funzo kwa Sababu Una Kazi Nyingi
    Huduma Yetu ya Ufalme—2012
  • Kuongoza Mafunzo ya Biblia Yenye Maendeleo
    Huduma Yetu ya Ufalme—2004
  • Fanya Namna Yako ya Kujifunza Ikuwe Muzuri Zaidi!
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2019
Huduma Yetu ya Ufalme—2007
km 11/07 uku. 4

Usisite Kuongoza Funzo la Biblia!

1 Kwa kushiriki kwa bidii katika kazi ya kutangaza habari njema ya Ufalme wa Mungu, ‘hatuwanyime mema’ watu walio katika maeneo tuliyogawiwa. (Met. 3:27) Hakuna habari nyingine iliyo nzuri sana kuliko ile ya kuelezea wanadamu kuhusu nyakati nzuri sana zinazokuja wakati wa utawala wa Ufalme wa Mungu. Ijapokuwa unaweza kuonyesha wema kwa kuelezea wengine kuhusu tumaini la Ufalme ukiwahubiria hata ikiwa haukupanga kufanya hivyo ao kuwatolea kitabu, unaweza kufanya mradi wako uwe kuongoza funzo la Biblia, ikiwa haujaanza kufanya hivyo.

2 Nyakati nyingine, moja ya vizuizi vikubwa zaidi vinavyotufanya tusite kuongoza funzo la Biblia, ni namna tunavyofikiri kuhusu jambo hilo. Watu fulani wanasita kuongoza funzo la Biblia kwa sababu wanakosa uhakika ao kwa sababu wana kazi nyingi. Mapendekezo yanayofuata yanaweza kukusaidia ili usisite kushiriki katika kazi ya kuongoza mafunzo ya Biblia.—Mt. 28:19; Mdo. 20:20.

3 Kukosa Uhakika: Labda haukusoma masomo mengi ao kwa sababu nyingine fulani hauna uhakika katika uwezo wako wa kuongoza funzo la Biblia. Katika karne ya kwanza, wahubiri Wakristo waliopata matokeo mazuri walikuwa “watu wasio na elimu na wa kawaida tu.” Ni nini kilichowawezesha kufundisha wengine kweli? “Walikuwa pamoja na Yesu.” (Mdo. 4:13) Walijifunza kutoka kwa Mwalimu Mkuu Yesu, ambaye mafundisho yake na njia zake vimeandikwa kwa ajili yetu katika Maandiko. Hata ikiwa haukusoma masomo mengi, unaendelea kupata elimu ya kiroho ambayo haiwezi kulinganishwa na elimu nyingine yoyote.—Isa. 50:4; 2 Kor. 3:5.

4 Nyakati fulani, Yehova alitumia manabii ili kukaripia watawala waliokosea ao watu wengine wenye cheo cha juu. Manabii fulani kama vile Amosi, walikuwa na maisha ya hali ya chini na hawakujiona kuwa wa maana. Amosi alieleza: “Mimi sikuwa nabii, wala sikuwa mwana wa nabii, bali nilikuwa mchungaji na mminyaji wa tini za mikuyu.” (Amo. 7:14) Hata hivyo, Amosi hakusita kutangazia kuhani Amazia aliyekuwa akiabudu ndama ujumbe wa hukumu wa Yehova. (Amo. 7:16, 17) Sikuzote, tunapaswa kukumbuka kwamba tunafanya kazi ya Mungu na kwamba atatuwezesha kabisa kutimiza kazi ambayo ametutolea.—2 Tim. 3:17.

5 Ikiwa Una Kazi Nyingi: Hata ikiwa una kazi nyingi, labda umekwisha kujipangia wakati ili kushiriki kikawaida katika kazi ya kuhubiri. Kuongoza funzo la Biblia kunaweza kuwa sehemu yenye kupendeza zaidi ya utumishi wetu. Ni pendeleo la pekee sana kuona Neno la Yehova likibadili maisha ya mtu. (Ebr. 4:12) Yehova anapendezwa tunapojitoa sana ili kusaidia mtu “kupata ujuzi sahihi wa kweli.” (1 Tim. 2:4) Hata malaika wanafurahi wakati mtu fulani anatubu makosa yake ya zamani na kufanya maendeleo ya kiroho.—Luka 15:10.

6 ‘Mapenzi ya Mungu ni kwamba watu wa namna zote waokolewe na kupata ujuzi sahihi wa kweli.’ (1 Tim. 2:4) Tunatimiza pendeleo la pekee sana la kutumika kulingana na mapenzi ya Mungu ikiwa hatusite kuongoza mafunzo ya Biblia.

[Maulizo ya Funzo]

1. Ni katika njia gani ‘hatuwanyime watu mema’?

2. Ni nini kinachoweza kutufanya tusite kuanzisha funzo la Biblia?

3. Kwa nini tunaweza kufundisha wengine Biblia?

4. Tunaweza kujifunza nini kutokana na mfano wa Amosi?

5. Kwa nini tunapaswa kujikaza kuanzisha funzo la Biblia hata ikiwa tuna kazi nyingi?

6. Ni pendeleo gani tulilo nalo katika kutimiza mapenzi ya Mungu?

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine