Kusudia Kuongoza Funzo la Biblia
1 “Inueni macho yenu myatazame mashamba, kwamba ni meupe kwa ajili ya kuvunwa.” (Yoh. 4:35) Hali ambayo wahubiri Wakristo wanakutana nayo leo inalingana kabisa na maneno hayo ya Yesu Kristo.
2 Watu wanaotamani kwelikweli kufundishwa njia za Yehova wangali wanapatikana. Jambo hilo linaonekana wazi katika hesabu ya wanafunzi wapya wanaobatizwa kila mwaka. Ikiwa unapenda kwelikweli kuongoza funzo la Biblia, itakuomba ufanye nini?
3 Kusudia Kuongoza Funzo la Biblia: Jambo la kwanza, inakuomba ukusudie kuanzisha funzo la Biblia na kuliongoza kwa ukawadia. Unapohubiri, endelea kukumbuka kusudi lako. Kwa kuwa sisi Wakristo tulipewa kazi si ya kufundisha tu, lakini pia ya kuhubiri, sisi sote tunapaswa kuendelea kutafuta nafasi zaidi za kushiriki katika kazi ya kuongoza mafunzo ya Biblia.—Mt. 24:14; 28:19, 20.
4 Mambo Mengine ya Kukumbuka: Kusali sana ni jambo la lazima sana kwa kila mhubiri wa Ufalme. Nyakati fulani tunakutana na watu ambao walikuwa wameomba Mungu ili awasaidie wapate kuelewa Biblia. Ni baraka kabisa kutumiwa na Yehova ili kukutana na watu kama hao na kuwafundisha!—Hag. 2:7; Mdo. 10:1, 2.
5 Dada mmoja alisali ili apate funzo la Biblia, na kisha kwenye mahali pake pa kazi, alitolea watu trakti Je, Ungependa Kujua Mengi Zaidi Kuhusu Biblia? Mwanamke mmoja alipochukua trakti moja, aliisoma yote, na akaanza kujaza kuponi. Dada alizungumza naye na aliweza kuanzisha funzo la Biblia.
6 Wahubiri wenzako ambao wanapata matokeo mazuri kwa kuanzisha na kuongoza mafunzo ya Biblia wanaweza kukusaidia ili ufikie kuongoza funzo la Biblia kama ulivyokusudia. Sali kwa Mungu kuhusu bidii yako ya kutafuta mtu wa kujifunza naye Biblia, na ukubali msaada wowote utakaotolewa ili kutimiza kusudi lako. Kwa kufanya hivyo, labda wewe pia hivi karibuni utakuwa na furaha ya kuongoza funzo la Biblia.