Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 12/07 uku. 8
  • Fariji Waliovunjika Moyo

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Fariji Waliovunjika Moyo
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2007
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Namna Mungu Anatolea Watu Kitulizo
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2016
  • ‘Wafariji Wote Wanaoomboleza’
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Namna ya Kufariji Wale Wenye Wametendewa Mubaya Kingono
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2019
  • Mtegemee Yehova, “Mungu wa Faraja Yote”
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2007
km 12/07 uku. 8

Fariji Waliovunjika Moyo

1 Wakati huu kuna uhitaji mkubwa wa kufariji wengine kuliko wakati mwingine wowote katika historia ya wanadamu. Kwa kufuata mfano wa Mfalme wetu Kristo Yesu, sisi pia tunatumika ili “kufunga majeraha ya waliovunjika moyo.”—Isa. 61:1.

2 Jinsi ya Kufariji: Ili kufariji watu, mahubiri yetu yanapaswa kuwa yenye kusawazika vizuri na yenye kutia moyo. Tunapozungumzia mambo mabaya ya ulimwengu na mafundisho ya uongo kwa kiasi fulani, kweli ya Maandiko na tumaini letu nzuri kuhusu ahadi za Mungu vinachukua nafasi ya kwanza katika mazungumzo yetu. Hilo halimaanishi kwamba hatupaswi kuzungumza kuhusu Har-magedoni. Kazi yetu inahusu kutangaza “mwaka wa nia njema upande wa Yehova na siku ya kisasi upande wa Mungu wetu,” na “kumwonya mwovu aache njia yake ya uovu.” Hata hivyo, tunapowaonya watu kuhusu Har-magedoni na kuwaelezea kuhusu matokeo yake ya kuharibu, hatutakazia hayo sana hivi kwamba watu wasahau kichwa cha habari njema ya Ufalme wa Mungu.—Isa. 61:2; Ezek. 3:18; Mt. 24:14.

3 Nyumba kwa Nyumba: Ni jambo la kawaida kukutana na watu waliovunjika moyo kwa sababu ya magonjwa, kifo cha mpendwa, ukosefu wa haki, au matatizo ya feza. Tukiwa waigaji wa Kristo, ‘tunawasikitikia’ wale tunaokutana nao katika kazi yetu ya kuhubiri na pia tunawasikilia huruma. (Luka 7:13; Rom. 12:15) Ijapokuwa tunamsomea mtu andiko moja au maandiko mawili kuhusiana na tatizo lake, tunapaswa kujionyesha kuwa ‘wepesi kuhusu kusikia,’ ili kumtolea mtu nafasi ya kutoa mawazo yake. (Yak. 1:19) Kisha kumsikiliza kwanza, tutakuwa katika hali nzuri ya kumfariji.

4 Kwa wakati unaofaa katika mazungumzo, tunaweza kusema hivi, “Ninapenda kuzungumza nawe kuhusu maneno fulani yenye kutia moyo kutoka Biblia.” Inaomba kutumia utambuzi ili tusipinge maoni yote yasiyofaa ambayo mtu anatoa, badala yake, kusudi letu kuu ni kumtia moyo na kumfariji tukitumia Maandiko. Kwa hiyo, unaweza kuchunguza kitabu Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko ukurasa wa 106-110 chini ya kichwa “Kitia-Moyo.” Ao unaweza kutolea msikilizaji wako trakti Faraja kwa Walioshuka Moyo na kuzungumzia mawazo yenye kutia moyo yaliyo ndani ya trakti hiyo.

5 Tafuta Nafasi za Kuwafariji Wengine: Je, unajua jirani fulani, mfanyakazi mwenzako, mwanafunzi mwenzako, au mshiriki wa familia anayehitaji kufarijiwa? Kwa nini usijikaze kuwatembelea nyumbani mwao ukiwa na kusudi la kuwafariji kwa kutumia Maandiko? Ukijua jambo linalowavunja moyo, unaweza kujitayarisha kuhusu jambo hilo. Ili kufariji, ndugu fulani wameandika barua au wanafanya hivyo kwa njia ya telefone. Upendo wa kweli kwa jirani utatuchochea kuonyesha huruma na kuwatolea faraja wanayohitaji kupitia Maandiko.—Luka 10:25-37.

6 Ndiyo, tuna daraka la kufariji wale wanaoomboleza, kutia moyo walio na huzuni, na kuwatolea tumaini la wakati ujao ulio mzuri. Hiyo ndiyo faraja ambayo watu wote ulimwenguni wanahitaji. Kuzungumza kwa furaha kuhusu mambo mengi mazuri ambayo Mungu ameahidi kutafariji na kutolea tumaini watu wanao lazima ya mambo hayo kabisa. Siku zote na tukumbuke uhitaji wa kufunga majeraha ya waliovunjika moyo.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine