Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 1/08 uku. 3-6
  • ‘Toa Ushahidi Kamili Kuhusu Habari Njema’

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • ‘Toa Ushahidi Kamili Kuhusu Habari Njema’
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2008
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Tangazeni Mahali Pote Sifa Bora za Yehova
    Huduma Yetu ya Ufalme—2007
  • ‘Hubiri Neno la Mungu Kikamili’
    Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Endeleeni Kutangaza Kazi za Ajabu za Yehova
    Huduma Yetu ya Ufalme—2004
  • Kipindi cha Ukumbusho—Nafasi ya Kuhubiri Zaidi!
    Huduma Yetu ya Ufalme—2011
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2008
km 1/08 uku. 3-6

‘Toa Ushahidi Kamili Kuhusu Habari Njema’

1 Katika ulimwengu ambamo habari njema haipatikani mara nyingi, tuna pendeleo la “kutoa ushahidi kamili kuhusu habari njema ya fadhili zisizostahiliwa za Mungu.” (Mdo. 20:24) Hilo linatia ndani kujulisha watu kwamba ulimwengu mpya wa Yehova ambamo ‘mambo ya zamani yatakuwa yamepitilia mbali’ utachukua mahali pa “siku za mwisho.” (2 Tim. 3:1-5; Ufu. 21:4) Wakati huo magonjwa hayatakuwa tena. (Isa. 33:24) Wapendwa wetu waliokufa watatoka katika makaburi ya ukumbusho na kuungana tena na familia na marafiki zao. (Yoh. 5:28, 29) Dunia yote itafanywa kuwa paradiso nzuri. (Isa. 65:21-23) Hii ni mifano michache tu ya habari njema tunayopaswa kujulisha wengine!

2 Kutakuwa nafasi nzuri sana za kutangaza habari hiyo katika mwezi wa 3, wa 4 na wa 5. Katika miezi hiyo, hali ya hewa itakuwa nzuri na mchana utakuwa mrefu kupita usiku katika sehemu nyingi za dunia, hilo litafanya iwezekane kupitisha muda mrefu katika mahubiri. Kwa kuongezea, Ukumbusho ambao ni tukio la maana sana katika mwaka, utaazimishwa ulimwenguni pote Siku ya Posho tarehe 22 mwezi wa 3. Huu ndio wakati wa kuanza kujitayarisha ili kuongeza saa tunazotumia katika kazi ya kuhubiri.

3 Panga Kufanya Upainia Msaidizi: Je, unaweza kupanga wakati wako ili kufanya upainia msaidizi mwezi mmoja, miezi miwili, ao miezi hiyo yote mitatu? Munaweza kuchukua wakati fulani ili kuzungumzia jambo hili katika funzo lenu la familia linalofuata? Ikiwa munaelewana na kupanga kusaidiana, mshiriki mmoja wa familia ao zaidi anaweza kufanya upainia msaidizi. (Met. 15:22) Musali kuhusu jambo hilo, nanyi mutaona jinsi Yehova anavyobariki bidii yenu. (Met. 16:3) Hata ikiwa hakuna mshiriki mmoja wa familia anayeweza kufanya upainia msaidizi, wote wanaweza kujiwekea miradi ya kuongeza saa wanazotumia katika kazi ya kuhubiri wanapohubiri na wale walio na uwezo wa kufanya upainia msaidizi.

4 Ikiwa una kazi inayokuchuka wakati wote, kufanya programu nzuri kunaweza kukuwezesha kufanya upainia msaidizi. Labda unaweza kutumia wakati fulani wa mapumziko ya mchana ili kuhubiri. Ao unaweza kuomba eneo lako mwenyewe la kuhubiri lililo karibu na mahali unapoishi ao mahali pa kazi na kuhubiri karibu saa moja ao zaidi mbele ao kisha kazi. Unaweza kupata wakati mwingi zaidi kwa kupanga kufanya kazi zisizo za lazima katika mwezi mwingine na kuhubiri mchana mzima kila Siku ya Posho na Siku ya Yenga. Wakati wa mapumziko, wengine wamechukua siku moja ao mbili ili kuhubiri mchana mzima.

5 Ikiwa wewe ni mzeemzee ao mlemavu ao mzaifu, unaweza kufanya upainia msaidizi kwa kuhubiri saa chache kila siku. Umuombe Yehova akupe “nguvu zinazopita zile za kawaida.” (2 Kor. 4:7) Dada mmoja aliweza kufanya upainia msaidizi akiwa na miaka 106! Kupitia msaada wa Wakristo walio washiriki wa jamaa yake na wengine katika kutaniko, alihubiri nyumba kwa nyumba, alirudilia watu, alisindikiza wengine kwenye mafunzo ya Biblia na alishiriki katika sehemu zingine za kazi ya kuhubiri. Alitoa msaada wake katika kuanzisha mafunzo kumi ya Biblia. Anasema hivi: “Ninapofikiri kuhusu pendeleo la ajabu nililopata kwa kutumika nikiwa painia msaidizi, moyo wangu unajaa upendo na shukrani kwa Yehova, kwa Mwana wake na kwa tengenezo Lake lenye upendo. Kwa kweli, ninataka kumwambia Yehova ‘asante!’”

6 Ikiwa wewe ni kijana mwenye kubatizwa, hata ikiwa ungali mwanafunzi, unaweza pia kujaza ombi la upainia. Kama vile wale walio na kazi inayowachukua wakati wote, labda unaweza kupanga kuhubiri kila Siku ya Posho na kila Siku ya Yenga. Labda siku fulani katika juma, unaweza pia kuhubiri karibu saa moja ao zaidi kisha masomo. Je, kuna siku ambayo hakuna masomo unayoweza kutumia kwa ajili ya kazi ya kuhubiri? Ikiwa unataka kufanya upainia msaidizi, unaweza kuzungumza na wazazi wako kuhusu jambo hilo.

7 Wachochee Wengine: Katika kutaniko, wazee wanaweza kufanya mengi ili kuchochea wengine kupitia mfano wao. (1 Pet. 5:2, 3) Wanaweza kupanga mikutano ya zaidi kwa ajili ya mahubiri ili wale wanaotaka kuhubiri asubuhi sana, kisha masomo ao kisha kazi, washiriki. Mwangalizi wa utumishi atahakikisha kwamba wahubiri wenye kustahili wamepewa mgawo wa kuongoza mikutano hiyo na kwamba kuna eneo, magazeti na vitabu vya kutosha vya kutumia muda wa miezi hii mitatu ya utendaji wa pekee.

8 Katika kutaniko moja, wazee walianza miezi mingi mbele ya wakati kutia watu moyo wafanye upainia msaidizi. Kila juma, walitangazia kutaniko hesabu ya wahubiri ambao walikubaliwa kufanya upainia msaidizi. Hilo lilihakikishia wengine ambao walitaka kufanya kazi ya upainia msaidizi kwamba watapata watu wengi wa kuhubiri nao. Walipanga mikutano ya zaidi kwa ajili ya mahubiri asubuhi sana ao magharibi. Matokeo ni kwamba wahubiri 53 walifanya kazi ya upainia msaidizi katika mwezi wa 4, karibu nusu ya wahubiri katika kutaniko!

9 Wasaidie Wengine Kuhubiri: Wakati wapya na vijana wanastahili kuwa wahubiri, wanaweza kualikwa kutumika na wahubiri wenye uzoefu. Nafasi kama hiyo inaweza kupatikana katika kipindi cha Ukumbusho wakati ambapo wahubiri wengi katika kutaniko wataongeza saa wanazotumia katika kazi ya kuhubiri. Je, una mwanafunzi wa Biblia ambaye amepatanisha maisha yake na kanuni za haki za Yehova? Je, una watoto walio na mwenendo mzuri wanaofanya maendeleo lakini hawajakuwa wahubiri? Ikiwa watu kama hao wamesema kwamba wanataka kuwa wahubiri wasiobatizwa na unaona kwamba wanastahili, julisha mzee mmoja katika kutaniko. Mwangalizi msimamizi atafanya mpango ili wazee wawili wazungumzie jambo hilo pamoja nawe na mtoto ao mwanafunzi wako.

10 Miezi ijayo inaweza kuwa pia wakati wa pekee kwa ajili ya wale ambao wameacha kutenda ili waanze tena kuhubiri na kutaniko. Waangalizi wa Funzo la Kitabu la Kutaniko na wazee wengine watajikaza sana kutembelea watu kama hao na kualika kwa shauku kila mmoja wao atumike nao katika mahubiri. Ikiwa wameacha kutenda kwa muda mrefu, wazee wawili watazungumza nao kwanza ili kuona ikiwa wangali wanatimiza matakwa ili kuhubiri.—km 11/00 uku. 3.

11 Jitayarishe kwa Ajili ya Ukumbusho: Fidia ni njia kuu zaidi inayoonyesha “fadhili zisizostahiliwa za Mungu.” (Mdo. 20:24) Mamilioni ya watu wenye shukrani ulimwenguni pote watakusanyika Siku ya Posho tarehe 22 mwezi wa 3, kisha jua kutua, ili kuazimisha Ukumbusho wa kifo cha Kristo. Tunataka kualika na kusaidia watu wote walio na mioyo yenye haki wahuzurie tukio hili la maana linalotoa ushahidi kuhusu fazili zisizostahiliwa za Yehova kuelekea wanadamu.

12 Andika kwenye karatasi majina ya wale wote ambao unataka kualika. Bila shaka, kati ya majina hayo, kutakuwa majina ya watu wa jamaa yako, majirani wako, watu unaofahamiana nao kwenye kazi ao kwenye masomo, wanafunzi wa Biblia wa zamani na wa sasa, na wengine wote unaotembelea kwa ukawaida. Ikiwa watu fulani unaoalika wana maulizo kuhusu Ukumbusho, linaweza kuwa jambo lenye kusaidia kutumia nyongeza inayohusu Mlo wa Jioni wa Bwana kwenye ukurasa wa 206-208 wa kitabu Biblia Inafundisha. Hilo linaweza hata kukusaidia kuanzisha funzo la Biblia, kwa kuwa litakutolea nafasi ya kumwonyesha mtu kitabu hicho tunachotumia ili kuongoza mafunzo ya Biblia.

13 Dada mmoja aliandika kwenye karatasi familia 48 za kualika. Alipoalika familia hizo, alitia alama kwenye majina ya washiriki wa familia hizo na kuandika tarehe ambayo aliwaalika. Alifurahi sana kuona kwamba watu 26 alioalika walihuzuria Ukumbusho! Ndugu mmoja aliye na duka kubwa (magazin) alialika mfanyakazi wake aliyekuwa padri hapo mbele. Mtu huyo alihuzuria na kisha alisema hivi: “Mambo niliyojifunza kuhusu Biblia kwa muda wa saa moja yalipita yale niliyojifunza kwa miaka 30 katika dini ya Kikatoliki.” Kisha tu Ukumbusho, alikubali funzo la Biblia katika kitabu Biblia Inafundisha.

14 Shiriki Katika Kampanye: Kuanzia Siku ya Posho tarehe 1 mwezi wa 3 na kuendelea mpaka tarehe 22 mwezi wa 3, tutagawia watu ulimwenguni pote vikaratasi vya mwaliko wa pekee kuhusu Ukumbusho. Wahubiri wote watafanya yote wawezayo ili kushiriki katika kampanye hiyo ya maana. Ni vizuri zaidi kumpatia mtu mkononi kikaratasi hicho cha mwaliko kuliko kukiacha tu mlangoni. Hata hivyo, ikiwa muna eneo kubwa, wazee wanaweza kuamua ikiwa munaweza kuachia wale wasiokuwa nyumbani vikaratasi vya mwaliko; mukifanya hivyo bila kuonwa na wapita-njia. Kila Siku ya Posho na Siku ya Yenga, tutatolea pia watu magazeti mapya.

15 Kwa kuwa hatuna wakati mwingi wa kugawia watu vikaratasi vya mwaliko, ni vizuri zaidi kufanya utoaji wetu uwe mfupi. Mufanye hivyo kwa njia ya kirafiki na kwa uchangamfu. Munaweza kusema hivi: “Tunapenda kukualika wewe, washiriki wa familia yako, na marafiki zako kwenye tukio la maana sana litakalofanywa tarehe 22 mwezi wa 3. Chukua kikaratasi chako cha mwaliko. Maelezo yote yanaandikwa katika kikaratasi hiki.” Msikilizaji wako anaweza kuwa na maulizo. Ao anaweza kukubali kikaratasi cha mwaliko na hata kusema kwamba atakuja. Andika mambo fulani kuhusu mtu mwenye kupendezwa, na upange kumrudilia.

16 Mwaka uliopita, askari mmoja alikuta mlangoni pake kikaratasi cha mwaliko kwenye Ukumbusho. Aliamua kuhuzuria lakini alihitaji kumwomba ruhusa mkubwa wake wa jeshi. Alipomwonyesha kikaratasi cha mwaliko, mkubwa huyo alibaki kimya na kusema kwamba wazazi wake ni Mashahidi na kwamba alikuwa akiwafuata kwenye mikutano. Zaidi ya kumruhusu kuhuzuria Ukumbusho, mkubwa huyo wa jeshi alienda pia pamoja na askari wake kwenye Ukumbusho!

17 Onyesha Shukrani: Kwa kuwa kipindi cha Ukumbusho wa 2008 kinakaribia, kila mmoja wetu na afikiri kuhusu fazili zisizostahiliwa za Yehova kutuelekea. Mtume Paulo aliandika: “Tunawasihi ninyi pia msipokee fadhili zisizostahiliwa za Mungu kisha mkose kusudi lake.” (2 Kor. 6:1) Namna gani tunaonyesha kwamba hatukukosa kusudi la fazili zisizostahiliwa za Mungu? Paulo aliandika hivi: “Bali katika kila njia tunajipendekeza kuwa wahudumu wa Mungu.” (2 Kor. 6:4) Kwa hiyo, tunaonyesha shukrani yetu kuhusu zawadi ya Yehova kupitia mwenendo wetu mzuri na kwa kuhubiri kwa bidii habari njema. Katika kipindi hiki cha Ukumbusho, tutakuwa na nafasi nzuri sana ya kuongeza saa tunazotumia katika kazi ya kuhubiri, tukitoa ushahidi kamili kuhusu habari njema.

[Maulizo ya Funzo]

1. Ni habari njema gani tunayopaswa kujulisha wengine?

2. Kwa nini kipindi cha Ukumbusho kinatoa nafasi nzuri zaidi ili kutoa ushahidi kuhusu habari njema?

3. Tukiwa familia, ni nini kitakachotusaidia kuongeza saa tunazotumia katika kazi ya kuhubiri?

4. Ikiwa tuna kazi inayotuchukua wakati wote, namna gani tunaweza kupanga mambo yetu ili kufanya upainia msaidizi?

5. Namna gani unaweza kusaidia wazeewazee ao wazaifu ili wafanye kazi ya upainia msaidizi?

6. Vijana wenye kubatizwa ambao wangali wanafunzi wanaweza kufanya nini ili kufanya kazi ya upainia msaidizi?

7. Wazee wanaweza kufanya nini ili kuchochea wengine wahubiri sana katika kipindi cha Ukumbusho?

8. Tunajifunza nini kutokana na jambo lililoonwa katika kutaniko moja?

9. Kwa nini kipindi cha Ukumbusho ni nafasi nzuri kwa ajili ya wale wanaostahili kuanza kuhubiri habari njema?

10. Wazee wanaweza kufanya nini ili kusaidia wale ambao wameacha kutenda?

11. Ni nini iliyo njia kuu zaidi inayoonyesha “fadhili zisizostahiliwa za Mungu?”

12. Ni nani tunaoweza kualika kwenye Ukumbusho?

13. Namna gani Yehova alibariki bidii ya wahubiri wawili ambao waliamua kualika wengine kwenye Ukumbusho?

14. Ni kampanye gani itakayofanywa ulimwenguni pote kuanzia tarehe 1 mwezi wa 3?

15. Tunaweza kusema nini tunapomtolea mtu kikaratasi cha mwaliko kwenye Ukumbusho?

16. Ni jambo gani lililoonwa linaloonyesha umaana wa kufanya kampaye ya kualika watu wa eneo letu kwenye Ukumbusho?

17. Namna gani tunaonyesha kwamba hatukukosa kusudi la fazili zisizostahiliwa za Mungu?

[Kisanduku kwenye ukurasa wa 3]

Ni Nani Wanaoweza Kufanya Kazi ya Upainia Msaidizi?

◼ Washiriki wa familia

◼ Wale walio na kazi inayowachukua wakati wote

◼ Wazeewazee na wazaifu

◼ Wanafunzi

[Kisanduku kwenye ukurasa wa 4]

Munapogawia Watu Vikaratasi vya Mwaliko Kwenye Ukumbusho:

◼ Mufanye utoaji wenu uwe mfupi na kuongea kwa uchangamfu

◼ Muandike mambo fulani kuhusu watu wenye kupendezwa na muwarudilie

◼ Mutolee watu magazeti kila Siku ya Posho na Siku ya Yenga

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine