Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 4/08 uku. 3
  • ‘Fuata Hatua Zake kwa Ukaribu’

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • ‘Fuata Hatua Zake kwa Ukaribu’
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2008
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Unatimiza kwa Ukamili Utumishi Wako?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2019
  • ‘Njoo Uwe Mfuasi Wangu’
    Huduma Yetu ya Ufalme—2010
Huduma Yetu ya Ufalme—2008
km 4/08 uku. 3

‘Fuata Hatua Zake kwa Ukaribu’

1 Ijapokuwa Yesu hakupata elimu katika masomo ya Wayahudi, alikuwa Mhubiri mkubwa zaidi aliyejulikana. Jambo lenye kufurahisha sana ni kwamba mambo yanayohusu mahubiri ya Yesu yaliandikwa na kulindwa kwa faida yetu. Ili tuwe wahubiri wenye matokeo mazuri, tunapaswa “kufuata hatua zake kwa ukaribu.”—1 Pet. 2:21.

2 Onyesha Kwamba Unapenda Watu: Kuhangaikia watu kwa upendo ndilo jambo ambalo lilimchochea Yesu. (Marko 6:30-34) Watu wengi katika eneo letu wana “maumivu” na wanahitaji sana kujua kweli. (Rom. 8:22) Kufikiria hali yao yenye hatari na jinsi ambavyo Yehova anawahangaikia kwa upendo kutatuchochea kuendelea kuhubiri. (2 Pet. 3:9) Zaidi ya hiyo, watu watakuwa tayari kusikiliza ujumbe wetu ikiwa wanatambua kwamba tunawahangaikia kwelikweli.  

3 Zungumza na Watu Kila Mara Nafasi Inapojitokeza: Yesu alitumia kila nafasi iliyojitokeza ili kuhubiria wengine habari njema (Mt. 4:23; 9:9; Yoh. 4:7-10). Vivyo hivyo, tunataka tuwe tayari kuzungumza kuhusu kweli tunapofanya kazi zetu za kila siku. Wahubiri fulani wanachukua Biblia na vitabu ili waweze kuhubiria watu kwenye kazi, kwenye masomo, wanaposafiri na wanaponunua vitu na mahali pengine.

4 Kazia Ufalme Katika Mahubiri: Habari njema ya Ufalme ndiyo iliyokuwa kichwa kikuu cha mahubiri ya Yesu. (Luka 4:43) Ijapokuwa tunamhubiria mtu bila kuzungumzia Ufalme moja kwa moja, tukumbuke kwamba tutamsaidia aone uhitaji wa Ufalme. Hata ikiwa tunazungumzia hali mbaya za ulimwengu zinazoonyesha kwamba tunaishi katika siku za mwisho, kusudi letu kubwa ni ‘kutangaza habari njema ya mambo mema.’—Rom. 10:15.

5 Tegemea Neno la Mungu: Katika mahubiri yake, Yesu alitegemea Maandiko. Hakuna jambo fulani alilofundisha ambalo lilitokana na mawazo yake. (Yoh. 7:16, 18) Alijilisha kutokana na Neno la Mungu na alilitumia alipojaribiwa na Shetani. (Mt. 4:1-4) Ili kufundisha watu kwa matokeo, tunapaswa kusoma Biblia kila siku na kutumia mambo tunayojifunza. (Rom. 2:21) Tunapojibu maulizo katika mahubiri, tunapaswa kutaja Maandiko yanayounga mkono mambo tunayosema na kuyasoma moja kwa moja katika Biblia ikiwezekana. Tunataka msikilizaji aone kwamba hatutokezi mawazo yetu wenyewe lakini tunashikamana kabisa na mawazo ya Mungu.

6 Fanya Mafundisho Yako Yaguse Mioyo ya Watu: “Mtu mwingine hajapata kamwe kusema kama huyu.” (Yoh. 7:46) Hayo ni maneno ambayo askari walisema kumhusu Yesu walipoulizwa na makuhani na mafarisayo kwa nini walikosa kumkamata. Kuliko kueleza tu habari, Yesu alifundisha kwa njia iliyogusa mioyo ya wale waliomsikiliza. (Luka 24:32) Alitumia mifano iliyohusu maisha ya watu ya kila siku ili kuwasaidia waelewe mambo aliyofundisha. (Mt. 13:34) Yesu hakusumbua wasikilizaji wake kwa kuwatolea habari nyingi sana. (Yoh. 16:12) Alipohubiria watu, alielekezea fikira zao utukufu wa Yehova kuliko kujitukuza yeye mwenyewe. Kama vile Yesu, tunaweza kuwa walimu wema ikiwa tu tunafikiria ‘daima mafundisho yetu.’—1 Tim. 4:16.

7 Endelea Kuhubiri Ijapokuwa Unakutana na Wasiopendezwa na Wanaopinga: Ijapokuwa Yesu alifanya miujiza, watu wengi hawakumsikiliza. (Luka 10:13) Hata washiriki wa familia yake mwenyewe walifikiri kwamba alikuwa “amerukwa na akili.” (Marko 3:21) Hata hivyo, Yesu aliendelea kuhubiri. Aliendelea kuwa na maoni yenye kufaa kwa kuwa alikuwa na uhakika kabisa kwamba alikuwa na kweli ambayo ingeweka watu huru. (Yoh. 8:32) Kwa msaada wa Yehova, sisi pia tunakusudia kuendelea kuhubiri bila kuacha.—2 Kor. 4:1.

8 Jinyime Mambo Fulani Ili Kushiriki Sana Katika Kazi ya Kuhubiri: Yesu alijinyima mambo ya kimwili ili kuhubiria watu. (Mt. 8:20) Alihubiri bila kuchoka, nyakati nyingine mpaka usiku. (Marko 6:35, 36) Yesu alijua kwamba alikuwa na wakati mfupi ili kutimiza kazi yake. Kwa kuwa “wakati uliobaki umepungua,” sisi pia tunahitaji kutumia wakati wetu, nguvu zetu na mali yetu ili kumwiga Yesu.—1 Kor. 7:29-31.

9 Wakristo wa karne ya kwanza walikuwa wahubiri wenye matokeo kwa kuwa walijifunza kutoka kwa Yesu. (Mdo. 4:13) Sisi pia tunaweza kutimiza kabisa kazi yetu ya kuhubiri ikiwa tunamwiga Mhubiri mkuu zaidi anayejulikana katika historia. —2 Tim. 4:5.

[Maulizo ya Funzo]

1. Tunaweza kufanya nini ili tuwe wahubiri wenye matokeo mazuri?

2. Ni nini kitakachotusaidia kuwapenda watu kama vile Yesu alivyowapenda?

3. Yesu aliwahubiria watu katika nafasi gani?

4. Namna gani tunaweza kufanya Ufalme uwe kichwa kikuu cha mahubiri yetu?

5. Namna gani Biblia inapaswa kusaidia ili mahubiri yetu yawe yenye matokeo?

6. Yesu alifanya nini ili kugusa mioyo ya wasikilizaji wake?

7. Kwa nini Yesu aliendelea kuhubiri bila kuacha?

8, 9. Namna gani tunaweza kumwiga Yesu kwa kujinyima mambo fulani kwa ajili ya habari njema?

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine