Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi 01/09/08
“Unafikiri tunaweza kutafutia wapi mashauri yenye kutegemeka tunapochukua maamuzi ya maana? [Acha mtu ajibu. Soma Methali 3:5, 6.] Habari hii inakazia kwamba kufikiria matokeo mbele ya kufanya maamuzi ni hekima yenye kutoka kwa Mungu.” Onyesha habari iliyo kwenye ukurasa wa 8.
Amkeni! Mwezi wa 9
“Je, unafikiri kwamba Mungu alikusudia wanadamu wasumbuliwe na upungufu wa chakula wenye kuangamiza dunia leo? [Acha mtu ajibu.] Ona jinsi amepanga kumaliza tatizo hilo. [Soma Zaburi 72:16.] Habari hii inaeleza jinsi Mungu atakavyorudisha Paradiso duniani.” Onyesha habari iliyo kwenye ukurasa wa 8.
Mnara wa Mlinzi 01/10/08
“Katika nyakati hizi zenye machafuko, watu wengi wana wasiwasi kuhusu wakati ujao. Ni nini kinachokusaidia uendelee kuwa na maoni yenye kufaa? [Acha mutu ajibu.] Ona ahadi hii ya Biblia. [Soma Isaya 65:17.] Gazeti hili linatoa sababu nzuri ya kuwa na maoni yenye kufaa kuhusu wakati ujao.”
Amkeni! Mwezi wa 10
“Internet ni kifaa kizuri, lakini inatokeza hatari zaidi sana kwa watoto. Unafikiri tunaweza kuwalinda namna gani? [Acha mutu ajibu.] Tafazali ona wazo la andiko hili. [Soma na kutumia Methali 18:1.] Hii ni moja kati ya kanuni sita za Biblia zinazoonyeshwa katika habari hii ili kusaidia wazazi walinde watoto wao.” Onyesha habari iliyo kwenye ukurasa wa 7.