Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi 01/10/08
“Watu wenye elimu wanajua umaana wa daraka la baba katika familia. Unafikiri ni nini kinachomfanya mtu kuwa baba mzuri? [Acha mtu ajibu.] Yesu alikazia jinsi mfano wa Baba yake ulimsaidia. [Soma Yohana 5:19.] Habari hii inazungumzia sehemu sita za maana kuhusiana na daraka la baba.” Onyesha habari inayoanzia kwenye ukurasa wa 18.
Amkeni! Mwezi wa 10
“Watu wa dini mbalimbali wana maoni yenye kupingana kuhusu jinsi Mungu alivyo. Lakini, namna gani Mwana wa Mungu alieleza kumhusu? Ona maneno ya Yesu kwenye Yohana 4:24. [Soma.] Habari hii inazungumzia, katika kurasa mbili tu, maoni ya Biblia kuhusu ulizo, ‘Utu wa Mungu ni gani?’” Onyesha habari iliyo kwenye ukurasa wa 24 na 25.
Mnara wa Mlinzi 01/11/08
“Watu wengi wanaona kwamba mambo wanayoamini kuhusu Mungu mwenye upendo na fundisho la mateso ya milele ni mafundisho mawili yasiyopatana. Wewe unawaza namna gani? [Acha mtu ajibu.] Biblia inafundisha waziwazi kwamba Mungu hatendei watu kwa uovu wala halipizi kisasi. [Soma Ezekieli 18:23.] Utapendezwa na wazo la Maandiko linaloonyeshwa katika gazeti hili.”
Amkeni! Mwezi wa 11
“Mara nyingi watu wanafikiri kwamba ili kupata matokeo mazuri maishani, inaomba kuwa mwenye kujulikana, kuwa na mali ao kuwa mwenye nguvu. Unafikiri matokeo mazuri maishani yanatokana na nini? [Acha mtu ajibu.] Ona jambo linaloleta matokeo mazuri kulingana na Biblia. [Soma Zaburi 1:1-3.] Habari hii inazungumzia mambo makuu sita yanayoleta matokeo mazuri maishani.” Onyesha habari inayoanzia kwenye ukurasa wa 6.