Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 11/08 uku. 3
  • Kisanduku Cha Maulizo

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Kisanduku Cha Maulizo
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2008
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Ndoa ya Mashahidi wa Yehova Inakuwaka Namna Gani?
    Maulizo Yenye Watu Wanaulizaka Sana Juu ya Mashahidi wa Yehova
  • Epuka Roho ya Ulimwengu Wakati Unatayarisha Siku ya Ndoa
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2019
Huduma Yetu ya Ufalme—2008
km 11/08 uku. 3

Kisanduku Cha Maulizo

◼ Ikiwa mume na muke wanataka kutumia Jumba la Ufalme kwa ajili ya hotuba ya ndoa yao, ni mambo gani wanahitaji kuzungumza na wazee?

Ndoa ambazo zimetayarishwa kulingana na kanuni za Biblia zinamletea Yehova heshima. Yeye anaheshimiwa zaidi kuhusiana na hotuba za ndoa zinazotolewa kwenye Jumba la Ufalme, kwa kuwa watu wanaona mikutano yote inayofanywa humo kuwa yenye kuonyesha hali ya tengenezo letu. Wakati mume na muke wanaomba Jumba la Ufalme kwa ajili ya hotuba ya ndoa, ni jambo lenye kufaa wazee wa kutaniko wazungumze pamoja nao mambo fulani yanayohusiana na ndoa yao, ili “mambo yote yatendeke kwa adabu na kwa mpango.”—1 Kor. 14:40.

Mume na muke wanaotaka kutumia Jumba la Ufalme kwa ajili ya hotuba ya ndoa yao, wanapaswa kuandikia halmashauri ya utumishi ya kutaniko linalotumia jumba hilo. Barua hii inapaswa kutumwa mbele ya wakati, na wataonyesha katika barua tarehe na saa ambayo watatumia jumba hilo. Wanapaswa kukumbuka kwamba wazee hawawezi kubadili programu ya mikutano kwa sababu ya hotuba ya ndoa yao. Pia, bibi-arusi na bwana-arusi wanapaswa kuwa katika hali nzuri, wenye kuishi kulingana na kanuni za Biblia na pia sheria za haki za Yehova.

Ili kuhakikisha kwamba ndoa itafanywa kwa njia inayomletea Mungu heshima, mume na muke wanapaswa kuzungumzia mipango ya ndoa yao pamoja na halmashauri ya utumishi mbele ya kuchukua maamuzi ya mwisho. Hata ikiwa wazee hawatajaribu kulazimisha mume na muke wafuate maoni yao, ikiwa kuna jambo lolote lisilokubalika lililopangwa, ni vizuri mume na muke wajitiishe kwa yale ambayo wazee watawaomba kufanya. Muziki wa Melodies du Royaume ao wa kitabu chetu cha nyimbo tu ndio unaoweza kutumiwa. Ni lazima pia kuomba ruhusa ya kupamba Jumba la Ufalme ao kubadilisha mpangilio wa kawaida wa viti. Ikiwa kuna mpango wa kupiga picha ao kutumia kamera (filmer), jambo hilo halipaswi kufanywa kwa njia yenye kupunguza heshima kuhusiana na tukio hilo. Wazee wanaweza kuruhusu mazoezi yafanywe kwenye Jumba la Ufalme ikiwa tu hayatazuia programu zingine za kutaniko. Kikaratasi hata kimoja cha mwaliko wa ndoa hakipaswi kubandikwa kwenye ubao wa matangazo. Hata hivyo, wazee wanaweza kutayarisha tangazo fupi litakalosomwa kwenye Mkutano wa Utumishi ili kujulisha kutaniko kuhusu hotuba ya ndoa itakayotolewa kwenye Jumba la Ufalme.

Ijapokuwa si lazima waandamani wote wa bibi-arusi na bwana-arusi kwenye Jumba la Ufalme wawe wenye kubatizwa, haifai kati yao kuwe watu walio na mwenendo unaopingana sana na kanuni za Biblia ao watakaofanya wahuzuriaji wawe na mashaka. Hotuba ya ndoa itatolewa na mzee, ikiwa anapatikana. Wazee ni wafundishaji wa Neno la Mungu walio na sifa za kustahili kufundisha, hivyo ni wao wanaostahili kabisa kuzungumzia kanuni za Biblia zinazohusiana na tukio hilo la maana.—1 Tim. 3:2.

Kwa kuwa mzee atakayetoa hotuba ya ndoa anahusika katika ndoa hiyo, yeye pia anapaswa kujulishwa mbele ya wakati kuhusu mipango inayohusiana na ndoa hiyo. Atakutana na mume na muke ili kupata habari kuhusu mwenendo wao wakati wa uchumba; mume na muke wanapaswa kumwelezea mambo yote waziwazi na kusema kweli. Ikiwa mume ao muke alikuwa mwenye kuoa ao kuolewa hapo zamani, anapaswa kutoa uhakikisho unaoonyesha kwamba kulingana na Maandiko na sheria ya kaisari, amekuwa sasa huru kuoa ao kuolewa. (Mt. 19:9) Hilo linamaanisha kwamba ataonyesha wazee cheti kinachoonyesha kwamba ndoa hiyo imevunjwa.

Mume na muke wanapozungumza na wazee na kuwaunga mkono kabisa, ndoa yao itakuwa kipindi cha furaha kwa wote.—Met. 15:22; Ebr. 13:17.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine