Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi 01/03/09
“Inaweza kuwa vigumu sana kutenda mema wakati watu wanatusukuma kutenda mambo mabaya. Unafikiri ni jambo gani linaloweza kutusaidia tusishindwe? [Acha mutu ajibu. Kisha soma Methali 29:25.] Habari hii yenye kusaidia inazungumzia sababu tano zinazotufanya tuogope kumchukiza Mungu kuliko kuogopa kuwachukiza watu.” Onyesha habari inayoanzia kwenye ukurasa wa 12.
Amkeni! Mwezi wa 3
“Sisi wote tunataka kuwa na marafiki wazuri. Ni sifa gani unazofurahia sana rafiki yako awe nazo? [Acha mutu ajibu.] Ona maelezo haya ya Biblia. [Soma Methali 17:17.] Habari hii ina mapendekezo kuhusu jinsi ya kuchagua marafiki wazuri na jinsi ya kuwa rafiki mzuri ya wengine.” Onyesha habari inayoanzia kwenye ukurasa wa 18.
Mnara wa Mlinzi 01/04/09
“Ningependa kujua maoni yako kuhusu maneno haya ya Yesu. [Soma Yohana 3:3.] Unafikiri kuzaliwa tena kunamaanisha nini? [Acha mutu ajibu.] Kuelewa vizuri maelezo ya Yesu kutatusaidia katika maisha yetu na kutakaza sana matazamio yetu kuhusu wakati ujao. Gazeti hili linaeleza kwa nini hivyo.”
Amkeni! Mwezi wa 4
“Watoto wengi wanaokwenda kwenye masomo wanaonekana kuwa chini ya mikazo. Je, unafikiri kwamba mambo yamebadilika kwa kulinganisha na siku za wazazi wao? [Acha mutu ajibu.] Mkazo mwingi unaweza kuwa na matokeo mabaya. [Soma Mhubiri 7:7a.] Gazeti hili linazungumzia jinsi watu wazima wanavyoweza kusaidia vijana kushinda mikazo.”