Jinsi ya Kujitayarisha kwa Ajili ya Mkutano wa Utumishi
1. Kusudi la Mkutano wa Utumishi ni gani, na namna gani tunaweza kufaidika zaidi na mkutano huo?
1 Mkutano wa Utumishi unatusaidia tujue jinsi ya kuwahubiria watu vizuri. Mambo makuu yanayozungumziwa sana katika Mkutano wa Utumishi ni kuhusu kuhubiri habari njema ya Ufalme, kufanya wanafunzi, na kutangaza hukumu ya Mungu inayokaribia. (Mt. 28:20; Marko 13:10; 2 Pet. 3:7) Tunafaidika zaidi na mkutano huo wa maana tunapokuwa wenye kujitayarisha vizuri na tayari kutoa maelezo.
2. Namna gani tunaweza kujitayarisha ili kusikiliza sehemu inayotolewa kama hotuba?
2 Ikiwa Sehemu Itatolewa Kama Hotuba: Mara nyingi habari inaonyeshwa katika maagizo yanayotolewa msemaji. Tunaweza kuchunguza habari inayotolewa, kutia ndani maandiko yanayotajwa na kufikiri kuhusu jinsi tunavyoweza kutumia habari hiyo katika kazi yetu ya kuhubiri.
3. Tunaweza kufanya nini ili kujitayarisha kwa ajili ya sehemu ya mazungumzo ya maulizo na majibu?
3 Sehemu ya Mazungumzo ya Maulizo na Majibu: Sehemu hii itaongozwa sawasawa na funzo la Mnara wa Mlinzi. Msemaji ataanza kwa maneno machache ya utangulizi na kumalizia pia kwa maneno machache. Tunaweza kupiga kistari chini ya mawazo makuu ya kila fungu, na kujitayarisha kutoa maelezo mafupi yanayokazia mawazo makuu.
4. Namna gani tunaweza kujitayarisha kuhusu sehemu ya mazungumzo pamoja na wasikilizaji?
4 Sehemu ya Mazungumzo Pamoja na Wasikilizaji: Sehemu hii itatolewa kama hotuba, lakini msemaji ataomba wasikilizaji watoe maelezo fulani. Ikiwa unapiga kistari chini ya mawazo makuu na kusoma maandiko yanayotajwa, unaweza kutoa maelezo msemaji anapouliza maulizo. Ndugu anayeongoza sehemu hii atajikaza kabisa kufanya wasikilizaji watoe maelezo anapozungumzia mawazo makuu.
5. Ni nini kitakachotusaidia ili tufaidike zaidi na maonyesho?
5 Maonyesho: Sehemu fulani zinakuwa na maonyesho kuhusu hali tunazokutana nazo katika mahubiri, ili kutuonyesha jinsi tunavyoweza kutumia katika eneo letu habari inayozungumziwa. Wazee ao wahubiri wenye uzoefu mwingi ao mapainia wataombwa kufanya maonyesho. Unapotayarisha sehemu hii, unaweza pia kufikiria kimbele jinsi onyesho hilo litafanywa. Wakati onyesho linapofanywa kama linavyopendekezwa katika Huduma Yetu ya Ufalme, wewe unaweza kufikiri jinsi ya kuzungumza na mutu kwa kutumia maneno yako mwenyewe na jinsi ya kupatanisha habari hiyo na hali ya watu tofautitofauti unaohubiria. Usisahau kubeba kwenye mkutano kitabu ao gazeti litakalotumiwa kwa ajili ya onyesho. Katika Ibada ya Familia ya magaribi, unaweza kufanya mazoezi ya utoaji fulani unaopendekezwa, jambo hilo linaweza kusaidia.
6. Ni sababu fulani gani tulizo nazo za kujitayarisha kwa ajili ya Mkutano wa Utumishi?
6 Mkutano wa Utumishi unafurahisha zaidi ikiwa, mbele ya kwenda kwenye mkutano, tumejitayarisha na kufikiri kuhusu sehemu mbalimbali zitakazotolewa. Kwa kufanya hivyo, tutatiana moyo sana. (Rom. 1:11, 12) Ikiwa tunachukua wakati wa kujitayarisha kwa ajili ya Mkutano wa Utumishi, tutakuwa tayari kabisa kutimiza utumishi wetu.—2 Tim. 3:17.