Mkusanyiko wa Mzunguko Ambao Utatusaidia Kulinda Hali Yetu Njema ya Kiroho
1. Ni njia gani moja ambayo Yehova anatumia ili kutusaidia tutimize kazi ambayo ametutolea ya kueneza habari njema?
1 Yehova anatoa kwa uwingi habari, mazoezi na vitia moyo; hayo ni mambo tunayohitaji ili kutimiza kazi ambayo ametutolea ya kueneza habari njema. (Mt. 24:14; 2 Tim. 4:17) Mkusanyiko wetu wa mzunguko unaofanywa kila mwaka ni moja kati ya njia anazotumia ili kututolea mambo kama hayo. Programu mpya ya mkusanyiko wa mzunguko ya mwaka wa utumishi wa 2010 itazungumzia kichwa “Tulinde Hali Yetu Njema ya Kiroho,” kichwa hicho kinategemea andiko la Waroma 8:5 na Yuda 17-19. Programu hiyo inapangwa kuanza juma tokea tarehe 31 mwezi wa 8, 2009.
2. (a)Mkusanyiko wa mzunguko utatusaidia katika njia gani mbalimbali? (b) Namna gani mikusanyiko ya mzunguko iliyopita imekusaidia katika kazi ya kuhubiri?
2 Jinsi Ambavyo Mkusanyiko Huo Utatusaidia: Programu hiyo itatuonya kuhusu hatari mbalimbali, kama vile mambo ya kujifurahisha yenye kutukula wakati na kutukengeusha ili tusikazie uangalifu wetu mambo yaliyo ya maana kabisa. Tutajifunza jinsi ya kushinda tabia ya kuachilia mambo yasiyofaa, pia tutaona maana ya kuwa mutu wa kiroho. Hotuba-mfululizo ya Siku ya Yenga itaonyesha jinsi watu mmoja mmoja na watu wa familia mbalimbali wanavyoweza kutia nguvu hali yao ya kiroho wanapopambana na mikazo inayoendelea kuongezeka na wanapopatwa na majaribu makali ya imani. Programu hiyo itatusaidia kulinda mioyo yetu, hali yetu njema ya kiroho na kukumbuka baraka nyingi zinazowangojea wale wenye kulinda hali yao njema ya kiroho.
3. Mkusanyiko wetu wa mzunguko unaokuja utafanywa wakati gani, na tunapaswa kukusudia kufanya nini?
3 Mara tu tunapojua wakati na mahali ambapo mkusanyiko wetu wa mzunguko utafanywa, tuanze kujitayarisha ili kuwa hapo na kusikiliza kwa uangalifu vipindi vyote vya siku mbili. Tuwe hakika kwamba Yehova anabariki mikono ya mwenye bidii.—Met. 21:5.
4. Tunahakikishiwa kupata nini kwenye mkusanyiko wa mzunguko unaokuja?
4 Kwa kweli, Yehova ndiye Mtoaji wa zawadi hiyo njema. Programu hiyo iliyotayarishwa na mtumwa mwaminifu itakuwa ile tunayohitaji kabisa ili kuendelea katika utumishi wa Kikristo. Sisi ni wenye shukrani kwa Yehova kwa ajili ya mambo yote anayotutolea kwa upendo ili kutusaidia “tushike imara tangazo la hadharani la tumaini letu bila kuyumba-yumba.”—Ebr. 10:23-25; Yak. 1:17.