Tujibu Namna Gani?
1. Kwa nini tufuate mfano wa Yesu tunapoulizwa ulizo?
1 Mpaka leo, watu wanashangazwa na majibu ya Yesu alipoulizwa maulizo. Tunapoulizwa maulizo mbalimbali katika kazi yetu ya kuhubiri, ni vizuri tumwige Yesu kuhusu jinsi ya kujibu.—1 Pet. 2:21.
2. Ni nini kinachoweza kutusaidia tutoe jibu lenye kufaa kwa ulizo fulani?
2 Tusikilize Kwanza: Yesu alifikiria maoni ya mutu aliyemwuliza ulizo. Nyakati nyingine kufanya hivyo kunaomba kuuliza mutu maulizo ili kutambua mawazo yake. Mutu mwenye kuuliza hivi: “Je, ninyi munamwamini Yesu?” labda kile anachopenda kujua ni kwa nini hatuazimishe kuzaliwa kwa Yesu. Ikiwa tunatambua kabisa nia ya mutu anayeuliza ulizo, tunaweza kufikiri pamoja naye na kumtolea jibu linalomfaa.—Luka 10:25-37.
3. Ni vifaa gani tulivyo navyo vitakavyotusaidia kupata majibu yenye kusadikisha yanayotegemea Maandiko?
3 Tutumie Neno la Mungu Tunapojibu: Kwa kawaida, ni vizuri zaidi tutumie Biblia ili kujibu ulizo. (2 Tim. 3:16, 17; Ebr. 4:12) Kitabu Kutoa Sababu na pia sehemu “Vichwa vya Mazungumzo ya Biblia” iliyo katika Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya vitatusaidia ili kutoa jibu lenye kufaa. Hata ikiwa mutu mwenye kuuliza ulizo hakubali kwamba Biblia ni kitabu cha maana, tunaweza kutumia ufundi ili kumwonyesha yale ambayo Maandiko yanafundisha. Tumtie mutu moyo afikirie sana hekima iliyo katika Biblia, hekima isiyo na kosa. Tunapomwiga Yesu, majibu yetu yatakuwa “kama matunda ya mtofaa ya dhahabu kwenye chombo cha fedha kilichopambwa”—yatakuwa ya heshima, mazuri, na ya maana.—Met. 25:11.
4. Ni wakati gani ambapo si vizuri kujibu kila ulizo?
4 Je, Tunapaswa Kujibu Kila Ulizo? Ikiwa haujui jibu la ulizo fulani, usisikie haya kusema: “Sijui jibu, lakini ninaweza kwenda kutafuta katika vitabu habari kuhusu ulizo lako na nitarudi ili kukueleza habari ambayo nitapata.” Kujishusha kama hivyo na kupendezwa kabisa na mutu kunaweza kumchochea atuombe tumrudilie. Tukitambua kwamba ulizo linatokezwa na wapinzani ambao labda wanajaribu kuanzisha mabishano, tumwige Yesu kwa kukatiza mazungumzo. (Luka 20:1-8) Vivyo hivyo, ikiwa mutu fulani asiyependezwa kabisa na kweli anajaribu kubishana nasi, tukatize mazungumzo kwa heshima na tutumie wakati wetu ili kutafuta wale wenye kupendezwa kwa moyo wote.—Mt. 7:6.
5. Ni mfano gani ambao Yesu alituwekea kuhusu kujibu maulizo?
5 Yesu alijua kwamba kumtegemea Yehova kulikuwa kwa lazima ili kutimiza kazi yake aliyopewa ya ‘kutoa ushahidi juu ya ile kweli,’ kazi hiyo ilimaanisha pia kujibu maulizo ya watu ambao walitaka kabisa kupata majibu. (Yoh. 18:37) Tuna pendeleo kubwa sana la kumwiga Yesu tunapojibu maulizo ya wale walio na “mwelekeo unaofaa kwa ajili ya uzima wa milele”!—Mdo. 13:48.