Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 11/09 uku. 2
  • “Wakeni Roho”

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • “Wakeni Roho”
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2009
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Tuendelee na Bidii Yetu Katika Kazi ya Kuhubiri
    Huduma Yetu ya Ufalme—2007
  • Utaiga Bidii ya Yehova na ya Yesu Katika Kipindi Hiki cha Ukumbusho?
    Huduma Yetu ya Ufalme—2015
  • Je, Una “Bidii kwa Ajili ya Kazi Njema”?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
Huduma Yetu ya Ufalme—2009
km 11/09 uku. 2

“Wakeni Roho”

1. Ni jambo gani linalopaswa kuonekana katika kazi yetu ya kuhubiri?

1 Kila sehemu ya utumishi wetu wa Kikristo inahitaji maendeleo. Kwa hiyo, tunatiwa moyo: ‘kuwaka roho’ na ‘kumtumikia Yehova.’ (Rom. 12:11) Hata hivyo, kuna mambo mengi yanayoweza kufanya bidii yetu kwa ajili ya mahubiri ipunguke. Namna gani tunaweza ‘kuchochea kama moto’ bidii na shauku yetu kwa ajili ya kazi ya Ufalme?—2 Tim. 1:6, 7.

2. Funzo la pekee la Biblia lina matokeo gani kuhusu kazi yetu ya kuhubiri?

2 Funzo la Pekee la Biblia: Mhubiri anayepata matokeo mazuri ni yule anayependa sheria ya Mungu na kuguswa sana na kweli anazojifunza ndani yake. (Zab. 119:97) Tunapojifunza kweli za Biblia wakati wa funzo la pekee, hilo linachochea mioyo yetu na kutusaidia kuwa wenye bidii nyingi. Kumpenda Mtoaji wa kweli hizo na nia yetu ya kutangazia wengine habari njema vinatuchochea tumtukuze Mungu na kutangaza jina lake waziwazi. (Ebr. 13:15) Kwa kweli, kutangazia watu habari njema kwa bidii kunaonyesha kabisa kwamba tunaona kweli hizo kuwa za maana sana.

3. Namna gani roho ya Mungu inaweza kutusaidia katika mahubiri?

3 Tuombe Roho ya Mungu: Matokeo mazuri tunayopata katika kazi yetu ya kuhubiri hayatokani na nguvu yetu. Tunakuwa na bidii tunapoacha roho takatifu itende kwa uhuru ndani yetu. (1 Pet. 4:11) Kumkaribia Yule Anayetoa “nguvu zenye msukumo” kutatusaidia tuwe na nguvu ya kiroho ili kutoa ushahidi kwa ujasiri. (Isa. 40:26, 29-31) Mtume Paulo alipopatwa na matatizo katika kazi yake ya kuhubiri, ‘alipata msaada kutoka kwa Mungu.’ (Mdo. 26:21, 22) Roho takatifu ya Yehova yenye kutoa nguvu inaweza kutusaidia kuwaka roho katika mahubiri, hivyo tunapaswa kuiomba katika sala.—Luka 11:9-13.

4. Bidii inaweza kutusaidia kupata matokeo gani mazuri, lakini tunapaswa kuwa waangalifu kuhusu mambo gani?

4 Mara nyingi, kuwa na bidii nyingi katika kazi ya kuhubiri Ufalme kunachochea Wakristo wenzetu wawe pia wenye bidii zaidi. (2 Kor. 9:2) Katika eneo, watu wanakubali ujumbe unaotolewa kwa uchangamfu na usadikisho. Hata hivyo, tunapoonyesha bidii, tunapaswa sikuzote kutumia hekima na kuwa wapole. (Tito 3:2) Kila wakati, tunajikaza kuonyesha msikilizaji wetu heshima na kumwachia uhuru wa kuchagua.

5. Ni shauri gani lililoongozwa na roho ambalo tunapaswa kujikaza kufuata?

5 Sisi wahubiri wa Ufalme, acheni basi sikuzote ‘tuwake roho.’ Kwa hiyo, tuendelee kukomaza bidii yetu kupitia funzo la pekee la Biblia na tumwombe kwa bidii Yehova, yule anayeweza kututolea roho takatifu inayotoa nguvu. Kwa kufanya hivyo, tunaweza kutimiza kwa bidii kazi yetu ya kuhubiri kwa uwezo wa “roho takatifu na kwa usadikisho wenye nguvu.”—1 The. 1:5.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine