Uwe Mwenye Kusadikisha Unapofundisha
1. Mara nyingi kutumia Neno la Mungu vizuri katika mahubiri kunamaanisha nini?
1 Kama mtume Paulo, wahubiri wenye matokeo wanajua kwamba ‘kulitumia sawasawa neno la kweli’ kunamaanisha mengi zaidi ya kurudilia tu maneno ya Maandiko. (2 Tim. 2:15) Tunapotumia Neno la Mungu, namna gani tunaweza kuwa wenye ‘kushawishi’ ao kusadikisha tunapofundisha?—Mdo. 28:23.
2. Namna gani tunaweza kusaidia watu waliheshimu zaidi Neno la Mungu?
2 Acha Neno la Mungu Liseme: Jambo la kwanza, elekeza uangalifu wa mutu kwenye Biblia kwa njia ambayo itamfanya aiheshimu na aone kwamba ina hekima kutoka kwa Mungu. Tunapolitegemea Neno la Mungu, hilo linaweza kumchochea msikilizaji wetu asikilize kwa uangalifu tunaposoma andiko. (Ebr. 4:12) Tunaweza tu kusema: “Nimeona kwamba ni jambo lenye faida ujue maoni ya Mungu kuhusu jambo hili. Ona jinsi Neno lake linavyosema.” Inapowezekana, acha Neno la Mungu liseme kwa kulisoma moja kwa moja.
3. Kisha kusoma andiko, unaweza kufanya nini ili kumsaidia msikilizaji aelewe maana yake?
3 Jambo la pili, fasiria andiko unalosoma. Watu wengi wana magumu ya kuelewa andiko linaposomwa kwa mara ya kwanza. Mara nyingi, tunahitaji kufasiria andiko ili kuonyesha jinsi linavyopatana na habari tunayozungumzia. (Luka 24:26, 27) Onyesha mawazo makuu ya andiko. Kumuuliza msikilizaji wako ulizo kunaweza kukusaidia ujue ikiwa anaelewa vizuri wazo la andiko.—Met. 20:5; Mdo 8:30.
4. Ni jambo gani la mwisho tunalopaswa kufanya ili tuwe wenye kusadikisha tunapofundisha watu?
4 Fikiri na Mutu kwa Kutumia Maandiko: Jambo la tatu, ujikaze kugusa akili na moyo. Saidia msikilizaji aone jinsi anavyoweza kutumia andiko katika maisha yake. Kufikiri na mutu kwa kutumia maandiko kunaweza kumchochea abadili maoni yake. (Mdo 17:2-4; 19:8) Kwa mfano, kisha kusoma andiko la Zaburi 83:18 unaweza kufikiri naye ili aone kwamba ni jambo la maana kujifunza jina la mutu ili kufanya urafiki pamoja naye. Kisha, labda unaweza kumuuliza hivi, “Je, unafikiri kwamba kujua jina la Mungu kutafanya sala zako ziwe na maana zaidi?” Kufanya andiko lipatane na maisha ya mutu kwa njia hiyo kutamsaidia ajue jinsi anavyoweza kulitumia. Tunaposadikisha watu kwa kutumia Neno la Mungu kwa njia hiyo, hilo litafanya wenye mioyo ya haki wamwabudu Yehova, Mungu wa kweli na aliye hai.—Yer. 10:10.