Je, Una Jicho Rahisi?
1. Inamaanisha nini kuwa na ‘jicho rahisi’?
1 Mambo ambayo macho yetu yanakazia yanakuwa na matokeo fulani juu ya matendo yetu. Maneno haya ya Yesu ni ya kweli kabisa: “Basi, ikiwa jicho lako ni rahisi, mwili wako wote utakuwa mwangavu”! (Mt. 6:22) Ikiwa tuna jicho “rahisi” kiroho, litakazia jambo moja—kufanya mapenzi ya Mungu. Tunatafuta kwanza faida za Ufalme na hatukengeushwi na vitu vya kimwili visivyo vya lazima ao utendaji unaoweza kutuzuia tuhubiri.
2. Ni jambo gani linaloweza kupotosha mawazo yetu, lakini ni nini litakalotusaidia?
2 Tunahitaji Kujichunguza: Matangazo ya biashara (publicités) yanatuambia vitu tunavyohitaji ao vitu ambavyo wengine wanavyo. Matangazo hayo yanaweza kupotosha akili yetu. Mbele ya kutumia wakati, feza, ao nguvu ili kujikaza kupata kitu fulani ao kujikaza kununua kitu fulani, ni vizuri “kuhesabu gharama” kwanza kwa kujiuliza, ‘Je, kufanya hivyo kutanisaidia nimtumikie Yehova vizuri ao kutanizuia kufanya hivyo?’ (Luka 14:28; Flp. 1:9-11) Ni jambo la hekima pia kuchunguza kwa ukawaida jinsi tunaweza kurahisisha maisha yetu ili kuwa na wakati mwingi wa kuhubiri.—2 Kor. 13:5; Efe. 5:10.
3. Tunajifunza nini kutokana na dada mmoja aliyefanya mabadiliko ili kurahisisha maisha yake?
3 Wakati dada mmoja alianza kazi ya upainia wa kawaidia, aliamua kuendelea na kazi yake ya kimwili iliyomchukua wakati wote ijapokuwa kazi isiyomchukua wakati wote ingemsaidia apate feza za kutosha ili atimize mahitaji yake. Mwishowe alisema hivi: “Hakuna mutu anayeweza kuwatumikia mabwana wawili. Nilipaswa kuacha vitu ambavyo si mahitaji kabisa na kuhangaikia mahitaji yangu. Ninatambua kwamba vitu vya kimwili vinafikia kuharibika na kuvitafuta ni kujichokesha bure.” Hali yake ilimruhusu afanye mabadiliko ili kuwa na maisha rahisi ao mepesi, na kubadili kazi yake. Kufanya hivyo kulimsaidia aendelee na kazi yake ya upainia.
4. Kwa nini ni jambo la haraka kuwa na jicho rahisi?
4 Kwa kuwa tunaishi wakati unaoomba kutenda haraka, ni jambo la maana hata zaidi kuendelea kuwa na jicho rahisi. Kila siku inayopita inatufanya tukaribie sana mwisho wa ulimwengu huu na mwanzo wa ulimwengu mpya wa Mungu. (1 Kor. 7:29, 31) Kwa kutilia mkazo kazi ya kuhubiri, tunaweza kujiokoa sisi wenyewe na kuokoa wale wanaotusikiliza.—1 Tim. 4:16.